Tumeshuhudia juzi tu mfanyabiashara Mohammed Dewji akipitishwa kama mwekezaji atakayepatiwa Hisa 49% za klabu hivyo kuwa mwanachama mwenye hisa nyingi.
Lakini kabla hata hajakabidhiwa timu rasmi tayari tumeshuhudia na kuona sura Halisi ya Mo
1.Kauli aliyotoa Jana Mo kupitia ukurasa wake wa Twitter imeonyesha chembe chembe za u-Dictator ,hapo bado hajaanza kazi rasmi je akianza si ataonea wafanyakazi wa klabu ,
2.Wafanyakazi wa klabu ya simba watakuwa na uoga na furaha kuwaondoka sababu bosi mkuu akikasirika basi ataweza kuwaadabisha na kuwadhalilisha kupitia mitandao ya kijamii
3.Mwalimu Omog kateleza mechi moja lakini mwanahisa huyu kaamua kumtolea povu kupitia Twitter na haikupita masaa 3 viongozi walioshika hatamu simba wakajawa na hofu na kuamua kumtimua mwalimu
Hapa Dewji hajakabidhiwa rasmi Hisa na kuanza kufanya kazi tayari tumeshaona sura yake je akikabidhiwa Hisa si itakuwa hapatoshi hapa mitaa ya msimbazi