Mo Dewji Bilionea aliyegeuza soka la Africa kuwa Biashara

Mo Dewji Bilionea aliyegeuza soka la Africa kuwa Biashara

Manyanza

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
16,464
Reaction score
35,629
IMG-20240912-WA0040.jpg

IMG-20240912-WA0041.jpg

Rais wa klabu, Mohammed Dewji ametajwa na jarida la Face2Face Africa lenye makao makuu yake jijini New York, Marekani kuwa mmoja kati ya mabilionea wawili ambao wamesaidia kukuza biashara ya mpira wa miguu barani Afrika.

Kutajwa kwa Mo kumetokana uwekezaji na mafanikio ambayo Simba imeyapata tangu alipoanza kufanya uwekezaji katika klabu hii kubwa zaidi kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Baadhi ya mafanikio ambayo yamepatikana ni pamoja na kushinda ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara mara nne mfululizo na kucheza mara tano hatua ya robo fainali ya michuano ya CAF jambo ambalo limeiwezesha klabu kushika nafasi ya saba kwa ubora wa vilabu. Lakini pia Mo amekuwa akitoa pesa za usajili na gharama zingine pindi zinapohitajika.
 
GSM Akitwajwa kwenye jarida la nipashe inatosha au umnasemaje wana utopolo
 
Mo Dewji kaajiri Wafanyakazi 37,000 hizo ni ajira binafsi achana na vibarua.

GSM Kaajiri hata Wafanyakazi hawafiki 3000 mara ya mwisho kwenye tovuti ya www.gsmgroup.africa ilionesha kaajiri wafanyakazi 2000 tu. Sasa hivi hata haipo tena
 
Back
Top Bottom