sasa tunaweza kuwa na kujadiliana. hapa umeandika kitu. naheshimu mtizamo wako ingawa naamini pia uliandika ukitegemea kuwa watakuja watu na mawazo tofauti na si wote watasema ... hewala au tawile.
1. laudit mavugo
huyu ni mchezaji mzuri lakini tatizo lake kubwa limekuwa ni kisaikolojia na hasa ni imani hizi za kiswahili ambazo watu wamemlisha au yeye mwenyewe kwa fikra zake. anaamini amerogwa, anaamini anahujumiwa na wenzie au mwenzie.tayari hapa ameshashindwa... angepata mtalaamu wa kisaikolojia ana akapewa mechi nyingi kucheza angekuwa mchezaji mzuri sana. na ikiwa ataenda team nyingine hapa tanzania utakuja kumwona ni mchezaji mzuri. ana kosa tu kuwa aggressive kutokana na aina ya uchezaji wake ule wa kunata na huo woga kweli anao. hapa anatakuwa kujengwa kisaikolojia. ila nakubali kwa sasa aachwe tu.
2. blagnon fredrick namkubali na nlikuwa namkubali toka mwanzo ni moja ya washambuliaji ambao nilishangaa kwa nini waliachwa na simba. alikuwa ni aina ya mshambuliaji kama john boko. yaani analazimisha kufunga hata kwa tumbo au makalio ili mradi afunge. kutokana na kuwa na nguvu kweli ukabaji wake ulikuwa mgumu. aangaliwe ana umri gani ikiwezekana arudishwe.
3. adam salamba na marcel kaheza ni wazuri.
tambwe hakuwa mchezaji mwenye nguvu sana au mkwara kwa mabeki. ni mviziaji ,ambaye unaweza kutomsikia kwa karibia dakika 20 ila ukaja msikia akiwa amefunga. hakuwa akitisha kama hao wengine akina blagnon au boko. so aina hii ya wachezaji pia ni wazuri maana wanasahaulika na hapo ndo huja kuwakumbusha mabeki kuwa wapo. salamba akipewa maelekezo ya kutulia na kuwa makini anaweza kuwa mzuri zaidi sababu nguvu anazo na umri unaruhusu.
marcel ni aina ya washambuliaji kama tambwe pia anaweza fundishwa na kupewa mazoezi ya kukaba.. but si lazima sana.. kuna washambuliaji wanaiwa goal poachers ndo alivyo huyu kijana... yeye ingekuwa ile miaka yetu tunacheza chandimu basi angekuwa ana uwezo hata wa kukaa na goal keeper wanapiga stories ila ukiipata mpira mpigie huko huko mbele..atainuka na kufunga.. huyu mnapokuwa mmezidiwa anakaa mbele standby nanyi mnamrushia mipira mirefu.kwa hiyo anafaida yake la msingi awe na pumzi na mbio basi.
ukitoa blagnon nani wengine kwa ndani na nje ya nchi wanafaa? viwango vya wachezaji wetu sometime havika constant unamkumbuka mbaraka mwaka jana? leo yupo wapi? aliweza msuva,tambwe,boko n.k kudumu kwa muda mrefu nadhani sababu ya nidhamu.
Naomba maoni yangu yaheshimiwe kama ambavyo nami pia nitayaheshimu yenu ambayo mtayatoa katika Kuchangia hili ambalo naenda kuligusia hapa kwani naona kuna ' Wapuuzi ' fulani ndani ya Simba SC wanadhani mpira wa miguu walicheza Wao pekee na kwamba wengine hatukucheza na hatuujui.
Nimepokea kwa masikitiko makubwa mno baada ya kusikia Klabu yangu ya Simba imewasajili Wachezaji Adam Salamba na Marcel Kaheza kwa ajili ya kuwatumia katika msimu ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom.
Kama hii taarifa ni ya kweli basi nakuwa wa Kwanza kabisa kuidharau na kuipuuuza Kamati ya Usajili ya Simba SC na namwomba ' Tajiri ' Mo Dewji asipoteze muda wake kukubali usajili wa hawa Wachezaji wawili.
Ukweli ni kwamba kwa jinsi nilivyowaona hawa Wachezaji wawili Adam Salamba na Marcel Kaheza hawana hadhi ya kuichezea Simba SC labda kama wanasajiliwa kuchezea Kikosi chetu cha Simba B naweza nikaunga mkono usajili wao huu.
Hoja yangu ni fupi tu na ya Kiufundi zaidi….
Adam Salamba
Ni mchezaji ambaye ufanisi wake uwanjani unaonekana katika mechi kama siyo nne au tano ambazo zinahusisha Timu za Simba,Yanga, Azam, Singida na Mtibwa Sugar lakini katika mechi zingine huwa anacheza hovyo sana. Simba SC haiitaji mchezaji wa msimu bali inataka mchezaji wa mechi zote na mwenye tija kwa Timu.
Pia umakini wake awapo uwanjani siyo ule ambao mshambuliaji wa sasa anatakiwa awe nao na kuna mechi kadhaa nimeshuhudia na kugundua kuwa anapenda sana kutumia nguvu nyingi sehemu ambayo hata haiitaji nguvu sana bali inataka tu akili kidogo hali ambayo mara nyingi imekuwa ikimfanya achoke haraka na kupoteza hovyo mipira na pasi zake.
Marcel Kaheza
Ni mchezaji ambaye nikiri kuwa amefanya vyema kwa msimu huu hasa katika Kufunga magoli / mabao ambavyo haikutarajiwa na wengi wetu. Hata hivyo mchezaji huyu ana mapungufu kadhaa ambayo ni kutokujua Kukaba kama akipoteza mipira na pia ana ushambuliaji wa kizamani wa kusubiri atengenezewe ndipo afunge.
Pia Marcel Kaheza ana uvivu na siyo myumbulifu hali ambayo inamfanya basi asiweze kuwa mchezaji tegemeo na mwenye msaada ndani ya Kikosi cha Simba SC ambacho kwa sasa kina jukumu kubwa la kudhihirisha umwamba wake Kimataifa.
MTIZAMO WANGU
Simba SC ya sasa haiitaji ‘ Schoolboys Strikers ‘ kama akina Adam Salamba na Marcel Kaheza bali inahitaji ‘ Clinical Finishers ‘ au ‘ Bull Strikers ‘ ambao wataifanya Simba SC iwe na kati ya 75% hadi 99% ya ushindi kila inapocheza na kwa ‘ uchunguzi ‘ wangu kwa hapa Tanzania kwa sasa bado sijaona aina hii ya Washambuliaji bali nawaona sana wakiwepo Ghana, Zambia na Zimbabwe.
Kama kweli Simba SC inataka kuyaenzi vyema yale maneno ya Mwanasimba mwenzetu Rais wa JMT Dr. Magufuli kwa kufanya vyema basi haina budi kuvunja ‘ Kibubu ‘ na kufanya Usajili kabambe ili tukafanye vizuri huko Kimataifa.
NANI WABAKI NA NANI WAACHWE?
Kama ambavyo huko nyuma niliwahi kusema, kuonya na kupinga usajili wa Kipa Said Nduda na Kuongezewa mkataba kwa Mshambuliaji Laudit Mavugo lakini kwakuwa nilishawaona na kuwasoma kuwa hawana jipya na hawatokuja kuwa na msaada Simba leo tena naendelea kusema kwamba Kipa Nduda na Mshambuliaji Mavugo waachwe kwani hawatufai.
Kwakuwa kunaonekana kuna matatizo kati ya Beki Mganda Juuko Murshid na Uongozi basi nashauri angeachwa tu ili nafasi yake na ile ya Mavugo Simba SC tuitumie katika kuwasajili Washambuliaji wawili tu ‘ mahiri ‘ na ‘ hatari ‘ ambao watakuwa wakisaidiana na akina Emanuel Robert Okwi na John Raphael Boko.
Hata hivyo kama Uongozi wa Simba SC bado una mawasiliano na Mchezaji Mshambuliaji Raia wa Ivory Coast ambaye nilimpenda, nilimkubali na niliumia nilipoona ameachwa aitwae Fredrick Blagnon halafu akaachwa mchezaji mbovu na asiyekuwa na faida Laudit Mavugo basi wafanye nae mazungumzo ili arudi Msimbazi kwani ni aina ya wale Washambuliaji ‘ Bull Strikers ‘ ambao nimewasema.
Mechi zote ambazo niliwahi kumshuhudia Blagnon akicheza Mabeki wa Timu pinzani walikuwa wakikiona cha moto na wengi wao walikuwa wakilala na Viatu vyao baada ya mechi kwani shughuli yake si ya Kitoto.
Nakumbuka kuna siku moja Rafiki yangu wa Siku nyingi na Beki wa Yanga ‘ Mtukutu ‘ Kelvin Yondan a.k.a Cotton aliwahi kuniambia kuwa hakuna Mshambuliaji anayemuogopa kama Fredrick Blagnon kwani ana nguvu sana na hakabiki kiurahisi halafu anajua kucheza rafu za akili ambazo kama ukienda kichwakichwa anaweza akakuumiza vibaya.
Na kama kuna Mshambuliaji ambaye Yondan amekuwa akiniambia kuwa ni mwepesi kukabika basi ni Laudit Mavugo na akasema mara nyingi sana kila akikutana nae katika hizi ‘ derby ‘ zetu za Simba na Yanga Yeye ( Yondan ) huwa anampiga ‘ mkwara ‘ Mavugo mapema tu na Mavugo humuogopa hadi kutoka kabisa mchezoni ila anasema aliwahi kufanya hivyo kwa Blagnon na kilichofuatia alishtukia anapigwa Kiwiko / Kipepsi ambacho kilimuumiza na ikambidi awe mpole na akawa anacheza nae Kiheshima kama siyo Kiutiifu zaidi.
Simba SC hatuna haja ya Kusajili Mabeki kwani tayari tunao wa kutosha na naanza sasa kumtabiria makubwa sana Beki Paul Bukaba kwani anacheza aina ya Beki ile ya ‘ Kazi Kazi ‘ ambayo ilikosekana sana katika Klabu ya Simba na hata Tanzania kwa ujumla. Kutokana na majeraha ya Beki Salim Mbonde nadhani huyu hatotufaa tena hivyo angeachwa tu.
Katika nafasi ya Kiungo sioni haja ya Kuongeza mchezaji yoyote yule kwani kumetosheleza ila nimesikia taarifa kuwa James Kotei anataka kuondoka hivyo niuombe tu Uongozi kumalizina nae mapema kwani ana msaada mkubwa sana katika Kikosi chetu kama ambavyo wote tumeweza kuuona alipocheza karibia katika mechi zake zote alizocheza.
Yangu ni hayo tu GENTAMYCINE.
Nawasilisha.
Cc: Ngushi , MSAGA SUMU , Komeo Lachuma , Gide MK, MACHONDELA