Mohammed Deif: Kamanda wa Majeshi ya Hamas mwenye jicho moja, mkono mmoja na roho tisa

Mohammed Deif: Kamanda wa Majeshi ya Hamas mwenye jicho moja, mkono mmoja na roho tisa

Pellman

Senior Member
Joined
Feb 13, 2017
Posts
195
Reaction score
220
1622427655786.png


Alizaliwa kwenye kambi za wakimbizi ukanda wa Gaza mwaka 1965

Aliwahi kufungwa kwenye majela ya Israel miaka ya mwanzo ya tisini

Ndie kamanda mkuu wa kikundi cha kijeshi, Qassam Brigades, cha Utawala wa Hamas wa Palestina

Anatafutwa kwa udi na uvumba na vyombo vya kijasusi na kijeshi vya Israel

Ni maarufu na hajulikani, infamous and anonymous

Akikatisha leo hii kwenye mitaa ya Wapalestina anaopigania uhai, uhuru na hazi zao si wengi watakaomtambua

Ana jicho moja na mkono mmoja, alikatwa miguu

Amenusurika kufa mara tisa

Hashobokei simu wala computer wala camera, vigumu kumdukua na kujua aliko

Moja ya kombora alilodondoshewa mwaka 2006 lilimuua mkewe Widad, binti yake wa miaka mitatu na kijana wake mchanga, Ali, yeye hakuwepo nyumbani

Kihistoria ni mkuu wa pili wa kikosi cha Qassam Brigades, majukumu aliyopokea kutoka kwa mkuu wa kwanza, Salah Shehadeh, aliyeuliwa mwaka 2002

Yeye ndio aliye dizaini mfumo wa makombora ya roketi ya Palestina na mifumo ya maandaki wanakojificha wapiganaji

Ana kura ya veto dhidi ya maamuzi ya Hamas japo ni mtiifu kwa viongozi wa kisiasa wa Hamas

Kabla ya machafuko ya Gaza Deif alikubali kusitisha mpango kabambe wa mashambulizi na utekaji wa raia na wanajeshi wa kiyahudi baada ya viongozi wa kisiasa wa Hamas kuliasa jeshi lao kufuta mpango huo

Israel wanakiri kwamba Muhammed Deif ni kamanda mzuri wa majeshi
 
Kamanda mkuu ila yamemsib maswala kibao mpaka unamshusha vyeo...Kamanda kaktwa miguu halaf bado unamwita hatar.Yan kiwete kawa tishio
kukatwa miguu ilikuwa ni tiba baada ya kushambuliwa, amputation

angekataa labda asingepona, kama ambavyo Bob Marley alikataa kukatwa kidole cha mguu, tatizo likasambaa mwili mzima, akafariki
 
Kuwa kiwete haikuondolei hadhi, heshima na uwezo wako wa kutenda.
Hata Moshe Dayan wa Israel alikuwa na jicho moja lkn alikuwa tishio vitani.

Vita mipango
 
Kamanda mkuu ila yamemsib maswala kibao mpaka unamshusha vyeo...Kamanda kaktwa miguu halaf bado unamwita hatar.Yan kiwete kawa tishio
Mkuu usishangae kiwete kua tishio,Hapo Parestana kulikua kuna mtu anaitwa.

SHEKHE AHMED YASSIN

alikua mremavu wa miguu toka akiwa na umri 12 yrs alipata ktk michezo,pia alikua Haoni vizuri. Israel walimuua kwa rocket 22/3/2004.alfajir akitokea msikitini, coz huyu kiumbe japoni mlemavu laki alikua ni hatari kwa usalama wa Israel.

Na ni moja ya waasisi wa kundi la HAMAS Na ndio kiumbe alikua na wafuasi wengi Palestina.
 
Kuwa kiwete haikuondolei hadhi, heshima na uwezo wako wa kutenda.
Hata Moshe Dayan wa Israel alikuwa na jicho moja lkn alikuwa tishio vitani.

Vita mipango
huyo ameaninishwa kwamba vita ni kujiandaa kwa kupasua mawe kwenye vifua, ndo maana anadhani kamanda mwenye jicho moja na mkono mmoja hawezi kuongoza majeshi

1622448769095.png
 
Kamanda mkuu ila yamemsib maswala kibao mpaka unamshusha vyeo...Kamanda kaktwa miguu halaf bado unamwita hatar.Yan kiwete kawa tishio
Spiritual leader Sheikh Ahmed Yassin aliyekua Hamas leader and founder of Hamas militant palestinian group alikua nearly blind na alikua akitumia wheel chair toka apate ajali akiwa na umri wa miaka 12 tu,

Lakini aliiongoza Hamas kwa ueledi wa hali ya juu mpaka akaja kuuawa tarehe 22.3.2004 akiwa kishakua mzee tena,Israel walitumia Helicopter kumpiga missile alipokua akitoka kusali sala ya alfajiri,

Sasa kwa akili yako kama unadhani mtu akiwa na ulemavu ndio hawi hatari unadhani Israel wao ni wajinga kumuwinda mpaka kumuua?
 
Kwenye picha ana macho mawili.... 😀 😀
picha hiyo ni ya mara ya mwisho alipoonekana mwaka 2000, kwa mujibu wa Associated French Press

jamaa ni wa mwaka 1965, unadhani atakuwa na baby face mpaka leo?

kwa sasa anaongoza majeshi mezani, lakini ukuu wake wa majeshi unaheshimiwa kwa taadhima na utii kwa sababu hakuna mwanajeshi wa Qassam Brigade aneyeamrishwa kuruka kiunzi cha moto ambacho kamanda Deif hajakiruka mara tatu zaidi...

amefungwa jela, amepewa kichapo, amepigwa mabomu, ameuliwa watoto wake, amekatwa miguu, amepoteza jicho, ameuliwa mkewe, amekwepa risasi... na bado anaongoza mapambano. Hawakubaliani nae kiitikadi na wanamuwinda wamtoe roho lakini Israeli imesema imemkubali kwa uwezo wa kikamanda.
 
Kamanda mkuu ila yamemsib masuala kibao mpaka unamshusha vyeo. Kamanda kakatwa miguu halafu bado unamwita hatar. Yani kiwete kawa tishio.
Hivi ikitokea ukamfumania mkeo yupo na kiwete au mtu mwenye jicho moja au kipofu kabisa au kiziwi hutofanya chochote kwa sababu ni mlemavu?
 
Back
Top Bottom