MOI kufanya upasuaji kwa kutumia Robot

MOI kufanya upasuaji kwa kutumia Robot

Mjanja M1

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2018
Posts
4,058
Reaction score
14,382
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI), Profesa Abel Makubi amesema Taasisi hiyo inatarajia kuanza kutoa huduma za kitabibu kwa kutumia roboti ndani ya miaka mitatu ijayo.

Akiongea kwenye mahojiano maalum Prof. Makubi amesema “Sasa hivi tunafanya evaluation tuweze kujua kwani tayari tuna vitu vingi tunafikiria kuvifanya lakini tunawaangalia wenzetu walifanya vitu gani ili kufikia hapa kwa haraka, kwahiyo tunafanya hiyo evaluation itatusaidia kutochukua muda mrefu kufikia hapo kama wenzetu”

“Kuna timu inafanya assignment kwenye suala la kutumia roboti na mitambo mingine zaidi ya kiteknolojia ya kisasa ambayo inatumia akili za kibinadamu (Artificial Intelligence) kufanya yenyewe badala ya kumtumia Binadamu ili kurahisisha kazi na kupunguza muingiliano na kumfanya Binadamu mwenyewe akifanyiwa oparesheni awe na matokeo mazuri zaidi, kwahiyo maandalizi yanafanyika tunategemea ndani ya miaka miwili ama mitatu ijayo tuweze kufanya oparesheni hiyo hapa MOI na hiyo itasaidia kwa asilimia 99 kupunguza oparesheni za Wananchi kwenda nje”

Source - AyoTv
 
R.i.P Classmate Daniel Arap Moi😥😪
 
Back
Top Bottom