Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) imezindua mafunzo ya kimataifa ya matibabu ya Saratani ya Mifupa na Misuli yanayofanyika kwa siku tatu ambapo zaidi ya madaktari 200 kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Uingereza, Australia, Malaysia wanashiriki.
Pia, Dkt. Mchome amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Prof. Abel Makubi kwa kuhakikisha mafunzo haya ya kimataifa yanafanyika hapa nchini ili kuwajengea uwezo wataalamu wa Tanzania na mataifa mengine barani Afrika na kuwa chachu ya utalii wa matibabu hapa nchini.
Naye, Daktari Bingwa wa Mifupa, Dkt. Violeth Lupondo amesema anajivunia kushiriki Mkutano wa kwanza wa Kitaifa wa Saratani ya Mifupa na Misuli Tanzania na mafunzo yatakuwa endelevu lengo ikiwa ni kuhakikisha huduma za kibingwa na bobezi zinapatikana MOI.