Molinga Kaadhibiwa, Bangala Kaachwa. TFF iache kuiogopa Yanga SC.

demigod

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2015
Posts
8,292
Reaction score
15,250
Nimeona David Molinga akihukumiwa kwa kosa la kuonyesha kidole chake kati

Kosa hilo hilo amelifanya Yannick Bangala game na Simba SC, sijajua ni utaratibu gani umetumika

Lakini Bangala alistahili adhabu kwa kitendo kile.

Kwanini TFF inaogopa hizi timu Kibwa...?

Sisi wanajangwani ni wapenda Fair Competition timeumizwa na kitendo cha Bangala kufanya uhuni pasi na kuadhibiwa.

Vitendo kama vile vina fifisha heshima na taswira njema ya klabu kubwa kama Dar es salaam Young Africans SC.
 
Aliyethibitisha kwamba ukionesha kidole cha kati ni uhuni ni nana? Na kwanini kidole cha kati? Mbona Chadema na CCM hutumia alama ya vidole kusalimiana na hakuna anayesema ni uhuni?
 
Kwani kitendo kile bangala alikifanya kwenye ligi ipi tuanzie apo kwanza, ilikuwa ligi kuu au ngao ya hisani, ngao ya hisani inao utaratibu wake ni tukio la siku moja na kila kitu kinaishia apo ndo maana lazima mshindi apatikane siku iyo iyo, kwaiyo ulitegemea wangemfungia kucheza ngao za hisani zinazofuata au ulifikiliaje? Kwamba angefungiwa mechi za ligi kuu? Brother kila jambo lina kanuni zake kawaulize tff watakupa majibu mazuri ya icho unachokifikilia, ata kama angepata kadi nyekundu ingeishia pale pale kwenye iyo mechi na si vinginevyo
 
Sasa itakuaje
 
🤔🤔🤔🤔 Unamaanishaa au limekutoka tu kwa bahati mbaya?
Kaka Jambo Kama hulijui ukikausha tu unapungukiwa Nini?
 
Sheria za kipuuz ET wanasema ngao ya hisan haisimamiwi na bodi ya ligi kwahiyo kwenye ngao ya hisan unaweza Fanya kitu chochote usichukuliwe hatua shirthole country
 
Kama hapa hajaelewa basi atamuwa pimbi
 
🤔🤔🤔🤔 Unamaanishaa au limekutoka tu kwa bahati mbaya?
Kaka Jambo Kama hulijui ukikausha tu unapungukiwa Nini?
Ebu tupe ufafanuzi wewe unaejua, hoja upingwa kwa hoja na sio kihoja! Tuambie sisi tusiojua ili tuelewe basi
 
Kama kafanya kosa kweli adhabu inamhusu haijalishi ilikuwa ngao ya hisani Kwa kuwa zote chini ya bodi ya ligi ndo hata mukoko hakucheza pia Morison
 
Kama kafanya kosa kweli adhabu inamhusu haijalishi ilikuwa ngao ya hisani Kwa kuwa zote chini ya bodi ya ligi ndo hata mukoko hakucheza pia Morison
Wewe usichanganye mambo, adhabu ya mukoko na morrison ilikuwa ni ya kombe la FA msimu ulioisha na sio ngao ya jamii, na unapopata kadi nyekundu kombe la FA adhabu inaendelea mpaka kwenye mechi zinazofuata tofauti na ngao ya hisani!
 
Makorokocho FC unyonge hausaidii
 
Irudie video utagundua kuna ujanja alitumia bangala ni kama alikua anaesabu madhambi
 
Lwanga alikula umeme ile mechi ila aliadhibiwa kwa kukosa mechi za Ligi kuu, kama ingekuwa siku moja adhabu ingeisha siku ileile. Unatakiwa ujue ngao ya jamii ni ufunguzi wa ligi na ina uhusiano nayo, usiwe shabiki bendera tu
 
Lwanga alikula umeme ile mechi ila aliadhibiwa kwa kukosa mechi za Ligi kuu, kama ingekuwa siku moja adhabu ingeisha siku ileile. Unatakiwa ujue ngao ya jamii ni ufunguzi wa ligi na ina uhusiano nayo, usiwe shabiki bendera tu
Acha ujinga pamoja na kula umeme lwanga aliumia goti mpaka sasa ndo maana aonekani angekuwa fiti angerndelea kucheza kama kawaida akuna kinachomzuia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…