Monaco yakubali kumuuza Tchouameni kwa R. Madrid

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610

Inadawa Real Madrid imekubaliana na AS Monaco kumnunua Aurelien Tchouameni (22) kwenye usajili utakaogharimu jumla ya zaidi ya Paundi Milioni 85 (Tsh. 249,405,355,250).

Klabu za Liverpool, Manchester United na PSG zilikuwa zinamuwania pia mchezaji huyo aliyejiimarishia nafasi katika kikosi cha timu ya taifa ya Ufaransa kwa miezi tisa iliyopita.

Kiungo huyo alianza maisha ya soka katika Klabu ya Bordeaux, na kisha kujiunga na AS Monaco Januari 2020 na kuweza kushinda tuzo ya Mchezaji Bora Mdogo katika Ligi Kuu ya Ufaransa.

Kwa usajili huu, timu gani itaweza kufikia ubora wa Kiungo cha R. Madrid?
 
Uyu dogo namuona Kama anakwenda kupokea mikono ya kina modric na kroos wanaoelekea mwishoni
 
Monaco anauza wachezaji wazuri
 
Madrid wangesajiri winga ya kulia ningefurahi sana
Mpira wa kisasa hautegemei Sana winga wakulia Wala kushoto wanatazama Sana katikati pakoje .......nishabiki wa Madrid bekitatu yao kaziyake huoni mkuu ......(maselo)

Au unataka anakwenda anakwenda anakwenda bado anakwenda ........
 
Mpira wa siku hizi ni siasa sana. Kwa mpira wa huyu kijana ni wa kuuzwa kwa £85mil (€100mil) kweli??

Acha tu tuwape hongera Monaco.
Umeshawahi muona akicheza?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…