Monitoring thread: John Pombe Magufuli katika Awamu ya Nne

Monitoring thread: John Pombe Magufuli katika Awamu ya Nne

Wakuu, tujaribu kuupitia utendaji wa Magufuli katika awamu ya nne na kwa kuanzia naanza na makala hii kutoka gazeti la Tanzania Daima


JANA vyombo vya habari nchini vimechapisha taarifa za ajabu. Taarifa hizi zinasema Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, John Pombe Magufuli, ametishiwa kuuawa na waandishi wa habari.

Waandishi anaowatuhumu ni Mhariri Mtendaji wa Habari Corporation, John Bwire, Mhariri wa Rai, Muhingo Rweyemamu na mwandishi wa Rai, Neophitius Kyaruzi.
Ametoa taarifa polisi Dodoma Julai, mwaka huu na kupewa RB namba DO/IR/3085/2006.

Katika mashitaka yake, anasema wahariri hao na mwandishi huyo wamemtishia kwa kutumia SMS kuwa watamuua.

Wao katika utetezi wanasema waliwasiliana naye kupata ufafanuzi juu ya
taarifa za barabara ya Usagara hadi Geita, zilizoonyesha kuwa kuna mahali hakutenda kwa usahihi, hali iliyoitia serikali hasara.



Source: Tanzania Daima


Alafu watu wanashika pango eti jembe? Waziri mzima andanganya ilikuwazima Waandishi wasiripoti upotefu wa Mapesa yetu. Jeuri hiyo na bado yuko nayo ''Wasio na Pesa wapige mbizi''-Kigamboni Dsm
 
Gazeti la Rai la Alhamisi [Oct 5 - Okt 11] limekuja na habari yenye kichwa hicho hapo juu.

Dondoo ni kuwa:

Wakala wa majengo, taasisi iliyo chini ya wizara ya Miundo mbinu, imemuuzia nyumba bwana Musa Joseph Magufuli (mdogo wake waziri Magufuli) huku akiwa na mkataba ambao unaonyesha angefanya kazi kwa miezi mitatu tu (26/09/2005 - 31/12/2005). Nyumba aliyouziwa iko ubungo, na ameuziwa kwa Tshs. 1.5M (!). Wakati anapewa ajira hiyo (Afisa tawala, business support unit), bwana Musa alikuwa na bado ni mwanafunzi wa masters UDSM. Alipoanza kazi tu akaanza kushughulikia ununuzi wa nyumba na within one month akawa na nyaraka zote muhimu za kumiliki nyumba hiyo. Wahadhiri wake UDSM wamesema kwa ratiba ya masomo yake ilivyokuwam masomo na kazi visingewezekana. Bwana Musa Magufuli aliacha kazi siku mbili kabla ya mkataba kwisha, akiwa na nyumba!

Mpo hapo? Sijui waziri atatuambiaje katika hili. Otherwise makeke yoote yale ya nyumba za NHC etc itakuwa anatuzuga tu.. nae yumo. ... labda aseme huyu ndugu alichakarika kivyake katika hili suala na yeye hakuhusika.

ni hatari sana. kweli ccm ni ccm tu wala hakuna jipya
 
Mussa Magufuli ni mdogo wake na JP Magufuli ambaye aliuziwa nyumba ya serikali na kaka yake mwezi mmoja baada ya kumaliza chuo kikuu. Pia aliajiriwa na serikali akiwa bado hajahitimu chuo kikuu bila diploma wala certificate.

Huyu ndio muadilifu mnayetaka apewe ikulu. Wananchi wanalala kwenye nyumba za tembe, polisi wanalala kwenye nyumba za suti. Wao wanagawana keki ya taifa. Huyu ndiye aliyesimamisha mradi wa barabara geita akaupindisha ili upite kijijini kwao.

Huyu ndiye aliyeweka taa za barabarani Chato jirani na baa yake. Mnamtaka ikulu

1444559903736.jpg

1444559915132.jpg


Source: Gazeti Rai Novemba 7, 2008
 
Mussa Magufuli ni mdogo wake na JP Magufuli ambaye aliuziwa nyumba ya serikali na kaka yake mwezi mmoja baada ya kumaliza chuo kikuu. Pia aliajiriwa na serikali akiwa bado hajahitimu chuo kikuu bila diploma wala certificate. Huyu ndio muadilifu mnayetaka apewe ikulu
Source: Gazeti Rai Novemba 7, 2008


Unalipwa kiasi gani na lowasa umekurupuka huko kuja kupost pumba inamaana watu wote waliouziwa nyumba ni wadogo zake Mh rais magufuli au?

Za kuambiwa changanya na za kwako
 
Hivi uadilifu hauhusiani na kuivunja amri ya 6? kwanini nisiamini Lowassa ni mwadilifu?
 
Mussa Magufuli ni mdogo wake na JP Magufuli ambaye aliuziwa nyumba ya serikali na kaka yake mwezi mmoja baada ya kumaliza chuo kikuu. Pia aliajiriwa na serikali akiwa bado hajahitimu chuo kikuu bila diploma wala certificate. Huyu ndio muadilifu mnayetaka apewe ikulu
Source: Gazeti Rai Novemba 7, 2008

Mshezi kweli huyu jamaa,Watumishi wa Umma hawana nyumba yeye amegawa kama peremende mpaka kwa kimada wake Sundi Malomo!!
 
Unalipwa kiasi gani na lowasa umekurupuka huko kuja kupost pumba inamaana watu wote waliouziwa nyumba ni wadogo zake Mh rais magufuli au?

Za kuambiwa changanya na za kwako

Ndio maana Lowassa akasema elimu elimu elimu. Kwa akili zako za kijani unaamini nimeambiwa? Huoni na ushahidi umewekwa na hajawahi kukanusha. Huoni nineweka source. Sasa nimeambiwa na nani? Kweli we mburula Dada yangu. Elimu elinu elimu inatakiwa kwa kweli ili Vilaza kama nyie angalau mfufuke
 
Kuna ile aliyomuuzia girl friend wake ambae hakua mtumishi wa umma, wamezaa nae tu akamuuzia nyumba ya serikali wakati masharti yalitaka wauziwe senior civil servants.

Nyumba ya bilioni 1.5 akamuuzia girl friend wake milioni 22. Nyumba ya bilioni moja akamuuzia rafiki yake Hosea wa Takukuru milioni 52.

Alafu huyo mdogo wake alikua wizara ya maliasili na utalii, mwaka jana magufuri akamhamishia wizara ya ujenzi bila kufuata utaratibu huku magufuri mwenyewe akibeba makalabrasha kwenda utumishi kushughulikia uhamisho na kutisha wafanyakazi wa utumishi wamhamishe mdogo wake kwa nguvu.

Ni wenye iq ya 20 tu ndio wanaweza kumsapoti magufuri, yaani mataahira.
 
Watu kwa kukosa ufahamu Wa mambo ndio utawasikia wakisema Magufuli ni muadilifu, ukweli unapingana na uhalisia
 
Mussa Magufuli ni mdogo wake na JP Magufuli ambaye aliuziwa nyumba ya serikali na kaka yake mwezi mmoja baada ya kumaliza chuo kikuu. Pia aliajiriwa na serikali akiwa bado hajahitimu chuo kikuu bila diploma wala certificate. Huyu ndio muadilifu mnayetaka apewe ikulu
Source: Gazeti Rai Novemba 7, 2008
 
Back
Top Bottom