Monopoly and Expansion za Kanisa ni Tishio kwa Nchi


Heshima kwako Shamu,

Mkuu umezungumzia mambo mawili makubwa.

Moja Kanisa linafanyabiashara wakati hawalipi kodi,Jibu Mradi wa kuzalisha umeme kwa vyovyote lazima uendeshwe na kampuni ambayo itafuata taratibu zote za uendeshaji wa kampuni eg,kulipa kodi zote zinazotakiwa kulipwa na makampuni mengine ambayo hayamilikiwi na mashirika ya dini eg PAYE,VAT,SDL na Corporate tax.kampuni hatakuwa na tofauti na makampuni mengine unayoyajua pengine tofauti kubwa ni umiliki "Kanisa katoliki.

Mbili, Makanisa mengi Tanzania hasa RC,KKKT na Anglican wana structure nzuri sana kiasi kwamba kuanzisha miradi mkubwa kama vyuo vikuu,Mahospital makubwa ni jambo rahisi sana.Mfano ukitembelea dayosisi ya Arusha utakuta uongozi umepangwa sawa sawa eg mkuu wa dayosisi ni askofu then anakuwepo mtendaji mkuu [Katibu mkuu] lazima awe na degree ya masuala ya utawala na uongozi,then mweka hazina lazima awe na CPA au sifa inayolingana na hiyo then mwanasheria lazima awe na degree ya sheria,afisa mipango na uchumi lazima awe na degree ya uchumi au sifa zinazolingana na hizo then utakuta mkuu wa afya au elimu nao lazima wawe na sifa zinazolingana na wajibu wa kazi zao.

Mkuu wangu ebu chungulia BAKWATA au kamati ya kutetea mali za waIslam au Shura ya maImamu au Ulamaa hakika utakutana na viongozi wasiokuwa na vision wala mission.Utakumbana na viongozi wanopigania umiliki wa misikiti,utakumbana na viongozi wanauza mali zilizoachwa na waIslam [wakfu],utakutana na viongozi wadanganyifu na wenye lugha za kichonganishi eg Mfumo kristo,waIslam tunaonewa na nk.

Hakika waIslam wa Tanzania ukiondoa Aghakhan wamelala hawana fikra za maendeleo hawatoi nafasi kwa waIslam wasomi,badala yake wamejikita kwenye mihadhara isiyo na tija kwao na kwa taifa.



 


Ngongo,

Swala usiliangalie katika dini bali liangalie kidemokrasia na sovereignity of this country. Ijapokuwa umezungumza mengi ya dharau na lawama kwa waislamu but that is same issue tunaipigia kelele. Sikutaka kuchangia hii topic but naona ni vizuri nikachangia kwasababu ndio jambo nalopigia kelele kila siku mimi na Mkandara kuwa taasisi za kidini zikijiiingiza katika uendeshaji wa biashara na utendaji wa serikali ni hatari kwa demokrasia ya nchi. Chukulia mfano Ngongo wewe umeasi kanisa ni mfano na kanisa likaamua likutenge. Unadhani kanisa likiwa limeshika kila kitu utakuwa na pa kutokea? Vile kanisa na misikiti inatakiwa kuwa waangalizi wa jamii kukosoa pale haki, dhuluma inapotokea but kama kanisa lina interest katika uwekezaji fulani na vitega uchumi fulani unafikiria watakosoa kitu?

Nitakupa mfano dhahiri majuzi tumeona Church of England lilivyoyumba pale waandamanaji wanaopinga ubepari walipoweka kambi nje ya kanisa jijini london. Kanisa likataka kuwafukuza lakini wakuu wa juu wa kanisa wakapinga. Mwishoe wakuu wa kanisa wawili wakajitoa kwani wamesema kanisa limekosa morality badala ya kutetea haki linatetea vitega uchumi. Sababu kubwa ni kwamba Church of England wanted to disassociate themselves with the protesters. Sasa imagine ishu ndogo kama hii wakuu wa kanisa wameresign kupinga church of England decision ya kuwa wafanyabiashara badala ya kutoa huduma ya kiroho.

Mfano mwengine spanish civil war was the aftermath battle between catholic conservatives na spanish republicans. Catholic church after the 6th century of conquest that saw the fall of Ottoman empire (Dola ya kiislamu ilyokuwa ikitawala Spain) waliwekeza sekta mbali mbali. Kanisa katoliki likawa na sauti kama serikali na kufikia hadi maaskofu wa kanisa katoliki kuwa wanalipwa mshahara na serikali. Republicans and other democratic reformist wakaona kuna hatari kubanwa kwa demokrasia hasa kwa wale ambao wanaona kuna mambo serikali inakwenda kinyume na serikali ya kidemokrasia. Mgongano huu ndio ulipelekea vita ya wenyewe kwa wenyewe baina ya republicans and catholic conservatives.

Tuje Rwanda genocide the same crisis and dilema. Kama mwandishi anavyosema hapa:-

The most detailed discussion of the role of religion in the Rwandan genocide is Timothy Longman's Christianity and Genocide in Rwanda.[SUP][5][/SUP] He argues that both Catholic and Protestant churches helped to make the genocide possible by giving moral sanction to the killing. Churches had longed played ethnic politics themselves, favoring the Tutsi during the colonial period then switching allegiance to the Hutu after 1959, sending a message that ethnic discrimination was consistent with church teaching. The church leaders had also long had close ties with the political leaders, and after the genocide began, the church leaders called on the population to support the new interim government, the very government that was supporting the genocide.

Hatupingi kanisa wawe na vitega uchumi au misikiti iwe na uwekezaji lakini visijiendeshe kibiashara kwani that very very dangerous to the stability and democracy of the country. Shauri yenu.
 
Hivi kuna dini yoyote iliyokatazwa kuwekeza kwenye huduma za jamii? Vinginevyo kama mimi mvivu nisiyejituma, jirani yangu akiwa na maendeleo, dawa sio kumpiga fitna na majungu...ni kufanya kazi na kuongeza maarifa
 
Waislam tumelala sana, tuache kulalama, tuinuke.

Zile thread zako uko visiwani sijui na jibaba... ukifanya zinaa... leo unajiita muislam... weye ndiye uliye lala

What an idiot!!

what a looser

kj (kubwa j) keshaiuza nchi yako!

since na weye umo ndani ya hiyo nchi basi na wewe utakuwa umeuzwa

madrasa na misikiti ya waumini watatu watatu kila mtaa, maendeleo hayo!

makubwa tena sanaa tu !
 


Mbona waislam mmemonopoly UFUGAJI WA MAJINI wakristo hawalalamiki?

haha! si mmemonopoly katika ugawaji wa vikombe sikuhizi .. dawa ukihamishwa haifanyi kazi .... sijui inatumia nguvu gani ile dawa ... mwaenda kunywa kikombe na mapambio kabisa ati mpone ukimwi ... hehehe!
 
Mkuu Ngongo nimeipenda tathmini yako ingawaje kwa namna moja imejaribu kuukwepa ukweli fulani.
Naomba nitofautiane na wewe kwenye red, shirika lolote la kidini halilipi kodi mkuu, iwe shule, hospitali, vyuo, mahotel, mabenk nk, kumbuka mjadala mkali uliotokea bunge lililopita na kuleta tafrani baada ya kuambiwa wataanza kulipia kodi, na moja ya mambo yaliyopigiwa sana kelele na wabunge ni kuwa iweje miradi ya kibiashara isilipiwe kodi? ikiwemo mabenk, hoteli vyuo nk.

Tunaweza kuona ni kweli kuwa kanisa lina miradi mingi kwa jamii lakini tukumbuke pia wanaagiza kila kitu bila kodi na wanaendesha biashara bila kodi na ni ukweli usiopingika wanatoza bei kubwa sana kwa huduma zao na hawalipi kodi, sasa kwa mwendo huo ni lazima wawe na miradi mingi maana hawajui hasara,wanahesabu faida tu.

Kuna safari moja nilikwenda dodoma nikalala hotel moja ya kanisa yaani bei nikubwa utadhani wanalipa kodi, leo hii vyuo vyao ndio vinaongoza kwa ada kubwa kabisa kuliko hata vyuo vinavyo lipa kodi.

Na bahati ni kwamba makanisa haya yameja wasomi waliobobea na wanajua ni aina gani ya biashara ya kufanya ambayo haita sumbua, mfano biashara ya vyuo, ada sio tatizo tena bodi ya mikopo ipo na soko ni kubwa, wanajipangia tu ada eti "gharama za uendeshaji zimepanda".
Hospitali ni biashara nzuri maana ugonjwa bana utauza hata mashamba kama umebanwa na sasa biashara ya mabenki nayo imeingiliwa na taasisi za dini.

Hoja hii imekosa nguvu kwakuwa mleta hoja ameileta kishabiki na kidini zaidi kwa kuona hili ni tatizo la wakristo, na ameonyesha kilio cha siku zote cha waislamu kuwa wakristo wanapendelewa, lakini kwa hili nashukuru umelijibu vyema kabisa kwamba tatizo ni waislamu wenyewe wamelala usingizi wa pono, chances are there wao wamekodoa macho tu, na wenzao wanapozichangamkia wanaona wanapendelewa.
Kama waisalamu wa tz hawata amka kwa kuwa na viongozi wa style ya Shekh Ponda wanaojua Koran, Hadith na suna za Mtume wataishia kununua vispika vya kizamani na kuendesha mijadala ya mara Yesu si Mungu na malalamiko kuwa tunaonewa

Na katika hili la kanisa kufanya sana biashara sitaki kulilaumu kanisa kabisa, anayepaswa kuhakikisha haya yanabadilika ni serikali, sheria inaruhusu hivyo hata hao waislamu kwa namna moja au nyingine nawao wanafanya biashara sema tu kutokana na upeo mdogo wa elimu dunia wa viongozi wao wanashindwa kutambua fursa zilizopo na kuzitumia na sasa wanaishia kulalama tu bila mpango baada ya kuwaona wenzao wamefanikiwa sana.

Pamoja na yote hayo lakini hii haiondoi ukweli kuwa taasisi za kidini kwa mfumo wetu wa kutokulipa kodi zina athari kubwa sana kiuchumi, kuna bilions of money inazunguka bila kulipiwa kodi kwa mgongo wa taasisi za kidini, hawa wanafanya biashara jamani sio "wanatoa huduma" kama wengi wetu tunavyojaribu kuumba, jaribu kufikiri hatua kadhaa mbele after ten yrs unadhani watakuwa na vyuo,hospitali,mabenk, hoteli ngapi kwa mwendo huu, na sasa wanaanza kuingia kwenye umeme na wataendele zaidi na zaidi, kiuchumi hii haikubaliki kabisa
Hakuna anayepinga wasifanye biashara bali walipe kodi, kuna vitu wanaweza kusamehewa kodi lakini si biashara, tunapoteza mapesa mengi sana kwenye hili bila sababu ya msingi.

Nimejaribu kupitia komenti kwenye hii sredi kiukweli wengi wamejibu kishabiki zaidi kama mleta mada mwenyewe alivyo ileta mada yake lakini pia ukiangalia upande wa pili wa shilingi kwa maana ya kiuchumi, panatatizo kubwa na litakuwa kubwa zaidi pale shughuli za kiuchumi zinazo involve a lot of money ambayo hailipi kodi


 


Je kama dini zote za TZ Wapagani, Wakristo, Waislamu, Wahindu, nk, wakiwa na biashara ambazo zinacontrol asilimia 60 au 50 ya uchumi wa nchi, je Serikali itajiendesha vipi? bila ya kukusanya kodi??
 

Ngongo,

Issue inayojitokeza si ya ufanisi au comparison kati ya Waislamu na Wakristo. Issue ninayozungumzia ni growth ya nchi inayotokana na mapato. Chukulia mfano, sera za Ujamaa tulizokuwa nazo baada ya Uhuru. Moja ya masharti ya kubadilisha mfumo huo wa Ujamaa to market economy ilikuwa ni kubinafsisha kampuni ktk private sectors.

Moja ya tatizo kubwa lililotokea kipindi hicho cha Ujamaa ilikuwa ni serikali ku subsidize ktk hizo kampuni za serikali. Matokeo yake, kampuni nyingi za serikali zilishindwa kufanya kazi kwa sababu hazikuwa na growth strategy za kumaximize profit zaidi ya kutegemea serikali.

Sasa hivi Kanisa na (Mashirika mengine ya dini) linafanya biashara likiwa na strategy za expansion lakini bado linategemea serikali ktk hiyo growth kama vile ruzuku, na misamaha ktk kodi.

Sasa chukulia mfano, ktk kipindi kinachokuja lets assume, hii expansion ya Kanisa na Mashirika ya dini imekuwa mpaka ikafikia kucontroll asilimia 60 au 50 ya uchumi wa nchi. Je unajua matokeo yake? Nchi itakollapse.

Kusolve hii issue, serikali inabidi ibadilike sasa hivi kabla ya hii hatari kutokea. Au haya Mashirika ya dini yanabidi yawe kama kampuni zengine ambazo zinalipa kodi, also ziwe zinajiendesha bila ya kutegemea ruzuku kutoka serikalini.
 
Je kama dini zote za TZ Wapagani, Wakristo, Waislamu, Wahindu, nk, wakiwa na biashara ambazo zinacontrol asilimia 60 au 50 ya uchumi wa nchi, je Serikali itajiendesha vipi? bila ya kukusanya kodi??


1. achana na mawazo ya kimasikini [magamba], why govt owns 40/50? poor management? lack of resources??

2. nipe hizo biashara za kanisa zinazofanywa [business type .. products/services, church involved, location] their prices compared to tax payers
 
1. achana na mawazo ya kimasikini [magamba], why govt owns 40/50? poor management? lack of resources??

2. nipe hizo biashara za kanisa zinazofanywa [business type .. products/services, church involved, location] their prices compared to tax payers

Kama ukisoma article zangu utaona hizo business ninazozisema. Also, Serikali haina haja ya kuown hizo 40/50 percent, zinaweza zikawa zinamilikiwa ktk private sectors. Lakini siyo ktk religion institutions ambazo haziingizi serikali mapato yoyote zaidi ya kutegemea ruzuku kutoka serikalini.
 
Je kama dini zote za TZ Wapagani, Wakristo, Waislamu, Wahindu, nk, wakiwa na biashara ambazo zinacontrol asilimia 60 au 50 ya uchumi wa nchi, je Serikali itajiendesha vipi? bila ya kukusanya kodi??

hiyo serkali mbona inaown 100% ya uchumi na bado nchi iko gizani? wahuni wanao jiita serkali ?
 

Kilimo ndio uti wa mgongo wa nchi yetu, Je, kanisa limejihusisha sana na Kilimo? Mimi nilifikiri utalisifu kanisa kwa kuwakomboa watanzania kifikra kupitia elimu! Hata hivyo naona elimu ya madrasa imekufanya uwe mentally incapacitated kwa kushindwa au ku-ignore kwa makusudi tatizo la uchumi wa nchi yetu - UFISADI!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…