Morocco: Mwanaharakati aachiwa huru baada ya kugoma kula gerezani kwa siku 19

Morocco: Mwanaharakati aachiwa huru baada ya kugoma kula gerezani kwa siku 19

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Mwanahistoria na Mwanaharakati nchini Morocco Maati Monjib aliyekuwa jela na kugoma kula kwa siku 19 ameachiliwa huru baada ya kushikiliwa kwa kipindi cha miezi mitatu.

Msomi huyo mwenye umri wa miaka 60 amekaribishwa uraiani na marafiki na wafuasi wake hapo jana baada ya kuachiwa kutoka jela ya El Arjat karibu na mji wa Rabat alikokuwa akizuiliwa tangu alipokamatwa.

Monjib anayefahamika kwa msimamo wake wa kuzikosoa waziwazi mamlaka nchini Morocco alikamatwa Desemba 29 kama hatua ya uchunguzi wa awali kuhusu tuhuma za kuhusishwa na utakatishaji fedha.

Mwanaharakati huyo anasema tuhuma dhidi yake zimetengenezwa na sasa kwakuwa ameachiwa huru atapigania uhuru wa wafungwa wengine wanaoshikiliwa kutokana na mitizamo yao.

Tuhuma dhidi ya Monjib zimehusishwa na usimamizi wa kituo alichokianzisha cha kusaidia kuunga mkono uandishi habari za uchunguzi.
 
Bongo ukigoma kula polisi wanafurahia ili ukufe kabisa haraka usiwape kazi ya kutafuta cha kusema pindi watakapokuua
 
Duh wengine siku moja tu chali sembuse 19
Migomo myengine inahitaji ujasili wa hali ya juu mi naweza kugoma kunyoa nywele tu kula si nitatesa minyoo yangu..🤣🤣
 
Mwanahistoria na Mwanaharakati nchini Morocco Maati Monjib aliyekuwa jela na kugoma kula kwa siku 19 ameachiliwa huru baada ya kushikiliwa kwa kipindi cha miezi mitatu.

Msomi huyo mwenye umri wa miaka 60 amekaribishwa uraiani na marafiki na wafuasi wake hapo jana baada ya kuachiwa kutoka jela ya El Arjat karibu na mji wa Rabat alikokuwa akizuiliwa tangu alipokamatwa.

Monjib anayefahamika kwa msimamo wake wa kuzikosoa waziwazi mamlaka nchini Morocco alikamatwa Desemba 29 kama hatua ya uchunguzi wa awali kuhusu tuhuma za kuhusishwa na utakatishaji fedha.

Mwanaharakati huyo anasema tuhuma dhidi yake zimetengenezwa na sasa kwakuwa ameachiwa huru atapigania uhuru wa wafungwa wengine wanaoshikiliwa kutokana na mitizamo yao.

Tuhuma dhidi ya Monjib zimehusishwa na usimamizi wa kituo alichokianzisha cha kusaidia kuunga mkono uandishi habari za uchunguzi.
 
Inawezekanaje kwa siku zote 19 pasipo kula? utumbo unjejikunja... natathmini kwa kina
 
Mwanahistoria na Mwanaharakati nchini Morocco Maati Monjib aliyekuwa jela na kugoma kula kwa siku 19 ameachiliwa huru baada ya kushikiliwa kwa kipindi cha miezi mitatu.

Msomi huyo mwenye umri wa miaka 60 amekaribishwa uraiani na marafiki na wafuasi wake hapo jana baada ya kuachiwa kutoka jela ya El Arjat karibu na mji wa Rabat alikokuwa akizuiliwa tangu alipokamatwa.

Monjib anayefahamika kwa msimamo wake wa kuzikosoa waziwazi mamlaka nchini Morocco alikamatwa Desemba 29 kama hatua ya uchunguzi wa awali kuhusu tuhuma za kuhusishwa na utakatishaji fedha.

Mwanaharakati huyo anasema tuhuma dhidi yake zimetengenezwa na sasa kwakuwa ameachiwa huru atapigania uhuru wa wafungwa wengine wanaoshikiliwa kutokana na mitizamo yao.

Tuhuma dhidi ya Monjib zimehusishwa na usimamizi wa kituo alichokianzisha cha kusaidia kuunga mkono uandishi habari za uchunguzi.

Huyu nae atakua ametokea chadema
 
Back
Top Bottom