View attachment 3215103
Jamani CCM ifike pahala muwe na huruma na nchi hii hata kama mna mpango wa kutawala milele. Itafika kipindi jamii ya nchi hii iwe kama jamii ya mazombi, maana hawa mazezeta mnaowaandaa ndio mtakuja kuwaachia nchi, na kipindi hicho jamii nzima itakuwa ya namna hiyo.
Wakati gen z wa Kenya wakizidi kujitambua hadi rais wao si tu anawaheshimu bali anawaogopa kabisa, kwa upande wa Tz gen z ndio kwanza wanazidi kuwa mazezeta wakitopea kwenye uchawa uliovuka mipaka.
Hebu fikiria, vyeti vya kushiriki matembezi na maombi vitawasaidia nini vijana wetu?
Sasa hao ni wale wa kujiita wasomi, je wale walioikosa hata hiyo elimu yetu ya 'hovyohovyo' hali itakuwaje? Huko mbeleni itafika kipindi watu watakuwa tayari hata kuramba makalio ya wengine ili wapate kupewa vyeti!
Kwa akili hizi akina Trump wafute tu misaada kwa 100%