Morogoro: Hujuma Mchana Kweupe Ujenzi wa Mitaro ya Barabara

Morogoro: Hujuma Mchana Kweupe Ujenzi wa Mitaro ya Barabara

Faana

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2011
Posts
38,657
Reaction score
44,759
Wadau mada inajieleza; nimeshitushwa sana nimepita Morogoro eneo la Mkundi ambako mwaka jana tu miezi ya mwishoni ulifanyika ujenzi wa mitaro ya maji ya mvua kandokando ya Highway ya Morogoro - Dodoma. Mvua iliyonyesha siku chache zilizopita imesomba mawe yote yaliyojengwa kwa cement na mchanga na kuiacha mitaro wazi kabisa. Kiukweli ile ni hujuma na ubadhirifu wa wazi kabisa uliofanywa na Mamlaka zilizopewa dhamana ya kusimamia fedha za kodi zetu.

Kumradhi nimeshindwa kupiga picha kwakuwa nilikuwa kwenye usafiri wa public, naamini wapo wana-Morogoro humu walioona ubadhirifu huo wanaweza kutusaidia kupost picha humu kama kielelezo.

Angalizo:
Habari hii haijalenga kumchafua mtu, nimeileta hapa ili wahusika wajitathimini kama kweli wanaitendea haki fedha ya kodi tunayolipa. Waandishi wa habari mnaweza kusaidia kuifikishia taarifa serikali kuu, kwakweli inasikitisha, inahuzunisha na kuumiza sana.

Nawasilisha
 
Ubadhirifu upi maana umeeleza maji yamesomba sasa ubadhirifu umefanywaje na maji yenyewe au watu na kivipi?
 
Ubadhirifu upi maana umeeleza maji yamesomba sasa ubadhirifu umefanywaje na maji yenyewe au watu na kivipi?
Swali zuri Mkuu, ubadhirifu ni katika ujenzi uliofanywa inaonekana dhahiri viwango vya cement vilivyowekwa ni hafifu na huenda usimamizi haukuwepo, kuna kila dalili cement iliibiwa kwa wingi kwa jinsi inavyoonekana.
 
Wadau mada inajieleza; nimeshitushwa sana nimepita Morogoro eneo la Mkundi ambako mwaka jana tu miezi ya mwishoni ulifanyika ujenzi wa mitaro ya maji ya mvua kandokando ya Highway ya Morogoro - Dodoma. Mvua iliyonyesha siku chache zilizopita imesomba mawe yote yaliyojengwa kwa cement na mchanga na kuiacha mitaro wazi kabisa. Kiukweli ile ni hujuma na ubadhirifu wa wazi kabisa uliofanywa na Mamlaka zilizopewa dhamana ya kusimamia fedha za kodi zetu.

Kumradhi nimeshindwa kupiga picha kwakuwa nilikuwa kwenye usafiri wa public, naamini wapo wana-Morogoro humu walioona ubadhirifu huo wanaweza kutusaidia kupost picha humu kama kielelezo.

Angalizo:
Habari hii haijalenga kumchafua mtu, nimeileta hapa ili wahusika wajitathimini kama kweli wanaitendea haki fedha ya kodi tunayolipa. Waandishi wa habari mnaweza kusaidia kuifikishia taarifa serikali kuu, kwakweli inasikitisha, inahuzunisha na kuumiza sana.

Nawasilisha

F9866DAB-EA83-4949-876A-00F63C888107.jpeg
 
Ubadhirifu upi maana umeeleza maji yamesomba sasa ubadhirifu umefanywaje na maji yenyewe au watu na kivipi?
Hujamwelewa. Anachosema hapa ni kwamba mawe na cement vilikuwa vimejengwa kwa kuegeshwa tu na hivyo mitaro ilionekana imejengwa kumbe hapana. Mvua ilipokuja ikasomba kirahisi tu kila kitu kilichokwepo.
Unajua nini? Mpaka inabidi ifikie mahali tuwe tunafanya kitu kama kinavyotakiwa kufanyika na mamlaka zilizoagiza kitu hicho kufanyika. Vinginevyo hata ashuke malaika kutoka mbinguni kuja kuongoza nchi, hatuwezi kutoka hapa tulipo
 
Hujamwelewa. Anachosema hapa ni kwamba mawe na cement vilikuwa vimejengwa kwa kuegeshwa tu na hivyo mitaro ilionekana imejengwa kumbe hapana. Mvua ilipokuja ikasomba kirahisi tu kila kitu kilichokwepo.
Unajua nini? Mpaka inabidi ifikie mahali tuwe tunafanya kitu kama kinavyotakiwa kufanyika na mamlaka zilizoagiza kitu hicho kufanyika. Vinginevyo hata ashuke malaika kutoka mbinguni kuja kuongoza nchi, hatuwezi kutoka hapa tulipo
nchi hii
 
waziri husika sijui anafahamu hili suala
 
Back
Top Bottom