Precious Diamond
JF-Expert Member
- Jun 9, 2023
- 593
- 1,376
Wakuu, nasikia tren ya SGR Dar-Dodoma imezima katika kituo cha kidete.
Pia soma:
Uzi mkuu unaoonesha yaliyojiri kwenye mradi wa SGR tangu kuanza kwake mpaka mradi ulipofikia hivi sasa
Serikali yasema treni ya SGR haitokuwa na tatizo la umeme
Milango imefunguliwa ili wapate hewa wakisubiri umeme urejee.
Mwenye taarifa zaidi atujuze.
==
UPDATE
Umeme ulirudi karibia saa saba za usiku na safari ikaendealea, hitilafu hiyo yasemwa kusababishwa na high voltage ya umeme wa TANESCO.
Pia soma: TRC yatolea ufanunuzi kuzimika kwa treni ya SGR Julai 30, 2024 katikati ya Stesheni ya Kilosa na Kidete
UPDATE
HITILAFU YA UMEME KATI YA KILOSA NA KIDETE
Dar es Salaam, Tarehe 31 Julai 2024
Shirika la Reli Tanzania (TRC) linaomba radhi kufuatia hitilafu ya umeme iliyojitokeza kati ya Stesheni ya Kilosa na Kidete na kusababisha treni ya reli ya kiwango cha kimataifa (SGR) iliyokuwa inasafiri kutoka Dar es Salaam kuelekea Dodoma kusimama kwa muda wa saa mbili (2) siku ya tarehe 30 Julai 2024.
Taarifa za awali zinaonesha kuwa hitilafu za aina hiyo husababishwa na wanyama (ngedere) au ndege (bundi) wanapogusa nyaya za umeme zilizotandazwa juu ya reli (overhead catenary system). Hitilafu ilisababisha umeme kukatika kituo cha kupoozea umeme namba 7 (Godegode) ambayo kitaalamu hujulikana kama (Instanteneous Overcurrent Protection Trip) majira ya saa 4:20 usiku.
Mafundi wa TRC walifanikiwa kutatua changamoto na kurejesha umeme saa 6:30 usiku na treni kuendelea na safari kuelekea Dodoma, na kuwasili Dodoma majira ya saa 7:57 usiku.
Shirika la Reli Tanzania linaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
Jamila Mbarouk
MKUU WA KITENGO CHA UHUSIANO
Pia soma:
Uzi mkuu unaoonesha yaliyojiri kwenye mradi wa SGR tangu kuanza kwake mpaka mradi ulipofikia hivi sasa
Serikali yasema treni ya SGR haitokuwa na tatizo la umeme
Milango imefunguliwa ili wapate hewa wakisubiri umeme urejee.
Mwenye taarifa zaidi atujuze.
==
UPDATE
Umeme ulirudi karibia saa saba za usiku na safari ikaendealea, hitilafu hiyo yasemwa kusababishwa na high voltage ya umeme wa TANESCO.
Pia soma: TRC yatolea ufanunuzi kuzimika kwa treni ya SGR Julai 30, 2024 katikati ya Stesheni ya Kilosa na Kidete
UPDATE
HITILAFU YA UMEME KATI YA KILOSA NA KIDETE
Dar es Salaam, Tarehe 31 Julai 2024
Shirika la Reli Tanzania (TRC) linaomba radhi kufuatia hitilafu ya umeme iliyojitokeza kati ya Stesheni ya Kilosa na Kidete na kusababisha treni ya reli ya kiwango cha kimataifa (SGR) iliyokuwa inasafiri kutoka Dar es Salaam kuelekea Dodoma kusimama kwa muda wa saa mbili (2) siku ya tarehe 30 Julai 2024.
Taarifa za awali zinaonesha kuwa hitilafu za aina hiyo husababishwa na wanyama (ngedere) au ndege (bundi) wanapogusa nyaya za umeme zilizotandazwa juu ya reli (overhead catenary system). Hitilafu ilisababisha umeme kukatika kituo cha kupoozea umeme namba 7 (Godegode) ambayo kitaalamu hujulikana kama (Instanteneous Overcurrent Protection Trip) majira ya saa 4:20 usiku.
Mafundi wa TRC walifanikiwa kutatua changamoto na kurejesha umeme saa 6:30 usiku na treni kuendelea na safari kuelekea Dodoma, na kuwasili Dodoma majira ya saa 7:57 usiku.
Shirika la Reli Tanzania linaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
Jamila Mbarouk
MKUU WA KITENGO CHA UHUSIANO