Moses Machali, naona ukuu wa Wilaya Bukoba unaelekea ukingoni, vijiwe vya kahawa soko kuu vinakung'oa

Moses Machali, naona ukuu wa Wilaya Bukoba unaelekea ukingoni, vijiwe vya kahawa soko kuu vinakung'oa

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Ile ajenda ya Kodi za zamani aliyoisema Mh. Rais na Mbunge wa Bukoba Mjini ni taa ya kukaa sawa dhidi ya Moses Machali, mkuu wa wilaya ya Bukoba, kwamba "walangila wameshamkalia vikao, na hawamtaki".

Bukoba ni wilaya ambayo Siasa imetamalaki, na Kuna wafanyabiashara wameshamuunguzia Uzi, na wanasiasa wanamuona anaharibu upepo wa kisiasa.

Kwa kifupi, anaweza kuhamishwa au kutupiwa virago.

Zile Kodi za leseni za biashara ulizoanza kuwapigia, kodi za miaka kadhaa nyuma, ukamdaka Afisa Biashara .....na mengineyo, na "kuwanyanganya" maduka wale wazee pale soko kuu, na kuwapangisha wapangaji, ni jambo jema, lakini hao jamaa " wanachoma utambi" balaa kwa kukunanga na "kukusimanga" kisiasa, na ushindi wao ni wewe kuondolewa Kagera.

Hiyo ndio Kagera, wenyewe Wana msemo wao " ukija Kagera ukaondoka hujaharibikiwa, mshukuru Mungu".

Kwa hisani ya wanywa kahawa soko kuu Bukoba
 
Machali ni fisadi mkubwa tu ambaye alitembelea nyota ya magufuli. Alikotoka nanyumbu aliacha maumivu ya kufa mtu. Yaan mkuu wa wilaya mzima unagombania nesi mpaka kuwaweka ndani watu.
Kuna kashule kalipaswa kuwa kameisha ila jamaa alisimamisha Kila mtu Ili iwe rahisi kupiga pesa. Machali ni jambazi
 
Machali ni fisadi mkubwa tu ambaye alitembelea nyota ya magufuli. Alikotoka nanyumbu aliacha maumivu ya kufa mtu. Yaan mkuu wa wilaya mzima unagombania nesi mpaka kuwaweka ndani watu.
Kuna kashule kalipaswa kuwa kameisha ila jamaa alisimamisha Kila mtu Ili iwe rahisi kupiga pesa. Machali ni jambazi

Kajamaa kalikuchukulia mzigo naona una hasira nako balaa
 
Machali ni fisadi mkubwa tu ambaye alitembelea nyota ya magufuli. Alikotoka nanyumbu aliacha maumivu ya kufa mtu. Yaan mkuu wa wilaya mzima unagombania nesi mpaka kuwaweka ndani watu.
Kuna kashule kalipaswa kuwa kameisha ila jamaa alisimamisha Kila mtu Ili iwe rahisi kupiga pesa. Machali ni jambazi
Pole sana kwa kuchukuliwa hicho kinesi chako na huyo Machali! Wakati mwingine akiingia kwenye 18 zako, usikubali tena kuwa mnyonge! Uwa wote, na wewe jitie kitanzi! Safi kabisa.
 
Kagera siku zote ni moto wake huanza kueashwa hapo Bukoba kwa Waendangabo. N8 watu wa kwendea kwa tatahadhari.Tunaambiwa enzi hizo alikuwepo DC Muleba hapo akiitwa Nditi akajifanya anajua kuingilia bei ya kahawa na kutaka kuwalimisha watu kilimo cha mihogo kwa lazima. Aliondoka bila kuaga baada ya wazee kumkemea hadharani mkutanoni.

Alikuwepo huyu Albert Mnari alikuwa DC Bukoba hapo,huyu kila mmoja anajua kilichompata baada ya kujipa mamlaka ya kusimamia walimu badala yavelimu.

Huyu Massawe sijui yuko wapi sasa hivi anguko lake lilianzia huko. Kuna chizi alicheza ngoma hapo uwanja wa Mayunga wakati wa kampeni za 2015 wazee wa Kiendangabo wakafanya yao mana alitia najisi ardhi yao yaliyofuata ni historia.

Ukipata fursa ya kuwa mtumishi Kagera nenda kwa staha wale watu hawataki dharau after all wanajua hakuna "mnyamahanga" anajua kuliko wao. Sasa huyo Machali ajiangalie.
 
Mkuu inaonekana bifu lako na machali lilikuwa sio la nchi hii au ww ndo yule muhasibu uliekuwa unatingisha mnara network isisome. Ila huko mkalama wanapelekewa Moto kwanzia mkurugenzi mpk mwenyekiti wa kitongoji
 
Wahaya mlikuwa tishio zamani, Sasa hivi hamna jipya. Hayo ni mambo ya kwenye kahawa na yatabakia kwenye kahawa tu.

By the way, bado huko Bukoba mnakunywa kahawa? Kinywaji cha enzi za mitume!! Mko nyuma sana aisee.

Miji mingine huku kwenye vijiwe tunavuta shisha, tunakunywa alikasusu, n.k
 
Back
Top Bottom