Mackanackyyy
JF-Expert Member
- Mar 26, 2019
- 2,338
- 5,271
Kwani umeambiwa hao marehemu 20 ni Wachaga? Unaamini kila aliye Dar es Salaam ni Mzaramo, na kila aliyeko Chato au Kolomije au Serikalini ni Msukuma?Hata uchagani wapo kumbe wajinga? Mbona huwa mnasema humu kuwa wachaga wamesoma sana? Au hawakuelimika? Pole zao!
Kusiwe na Double Standard,Kitendo alichokifanya Mwamposa si cha kiungwana hata kidogo,waamini wake 20 wamekufa yeye amepanda ndege na kurudi Dar kwenda kawe kuhubiri,Huyo jamaa anastahili kifungo,kwanza inabidi awekwe ndani kwa usalama wake maana sie tunaamini ametoa kafara ndio maana haijamgusa kabisa,kwa usalama wake tunaomba polisi mumuuhifadhi ndani kwa mda mpaka uchungu wa kuondokewa na ndugu zetu 20 upungue.
Siyo dini ya Kikristo tu. Hata dini nyingine, wajinga wa dini wapo kila sehemu. Hao wajinga wa dini wanakuwa wepesi kuwa-brainwashed na kufanywa religious extremists kisha wanaanza kupelekeshwa kama mbwa wa mwindaji. Hata magaidi wengi ni religious idiots wanaokuwa brainwashed na wanadanganywa na baadae kuamrishwa kufanya ujinga kwa kisingizio cha kuitetea imani/dini yao. Kwa maneno mengine hata hao wanaodanganywa na kuamini eti wakikanyaga mafuta wataondokana na shida walizonazo hadi kufikia hatua ya kuuana kwa kukanyagana hawana tofauti na gaidi anayeaminishwa kwamba akijilipua na kuua wengine atakwenda mbinguni! Wote ni wajinga wa dini.Yaani kiongozi wa dini upande wa kikristo anaweza kufanya chochote kwa waumini na wakatii...Poleni sana
jamaaa limetoa bonge la kafara aise hapo lazima mafanikio yaonekane ...Waumini 18 wa Dini ya Kikristo wamefariki dunia usiku huu mjini Moshi, wakati wakikanyagana kugombea kukanyaga mafuta ya upako katika kongamano la kidini la Mtume Boniface Mwamposa, DC wa Moshi Kippi Warioba amethibitisha
Updates: 00:45
Idadi ya watu waliopoteza maisha kwa kukanyagana imefikia 20 na uenda idadi hiyo ikaongezeka Mkuu wilaya amethibitisha.
UPDATES:
Watu 20 wamefariki dunia leo jioni Jumamosi Februari 1,2020 katika ibada ya mahuburi wakati wa harakati za kukanyaga mafuta ya upako kwenye kongamano la Mtume Boniface Mwamposa 'Buldoza' katika Viwanja vya Majengo Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro.
Inadaiwa kuwa waumini hao walikumbwa na maafa hayo wakati wakikanyagana kwa ajili ya kugombania kukanyaga mafuta yaliyomwagwa na mhubiri huyo yakidaiwa kuwa na upako.
Inaelezwa kuwa watu zaidi ya 40 walikanyagana katika harakati za kugombania mafuta ya upako na kukimbizwa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro ya Mawenzi.
Idadi ya waliokufa huenda ikaongezeka kwa kuwa hakuna taarifa ya ujumla ya majeruhi waliopelekwa katika vituo vya afya vya jirani pamoja na Hospitali ya Rufaa ya KCMC.
Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kippi Warioba amelithibitisha leo saa 5:00 usiku kuwa taarifa za awali waumini 20 wamekufa lakini akasisitiza hizo ni taarifa za awali.
βTaarifa za awali tulizonazo ni kuwa ni waumini 20 wamepoteza maisha lakini tunaendelea kufuatilia maeneo mengine ya zahanati, vituo vya afya na hospitali kama kuna watu walipelekwa huko,β amesema Kippi.
Apostle Boniface Mwamposa a.k.a Bulldozer
=====
MWAMPOSA ATAKIWA POLISI KWA MAHOJIANO
Jeshi la Polisi limemtaka Boniface Mwamposa kujisalimisha polisi kwa mahojiano ya vifo vya watu 20 vilivyotokea mjini Moshi Mkoa wa Kilimanjaro usiku Februari Mosi, 2020
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro, Salum Hamduni amesema mchungaji wa Kanisa la Calvary Assemblies of God, Elia Mwambapa ndiye aliyeomba kibali cha kongamano hilo la siku tatu lililomalizika jana Jumamosi
Amesema baada ya hilo tukio wamemtafuta sana huyo Boniface Mwamposa maarufu kama Bulldozer bila mafanikio. Na kumtaka ajisalimishe kwa mahojiano
Kamanda Hamduni alifafanua kuwa idadi ya waliokufa ni 20 hadi sasa, ambapo kati yao watoto wadogo ni wanne, watu wazima 16
Hata uchagani wapo kumbe wajinga? Mbona huwa mnasema humu kuwa wachaga wamesoma sana? Au hawakuelimika? Pole zao!
[/QUOTE
Mbona maka watu 5000 walikufa kwa kukanyagana nao je??hiyo ni ajali tu acheni kulopoka
Usizunguke. Hii mwamposa tayari katoa kafara maisha ya watu wasio na hatia, tena mwanzoni kabisa mwa mwaka. Kwani ndiyo mara yake ya kwanza kuwakanyagisha watu hayo matunguli yake?Here we go again, unaleta tena ramli chonganishi eti " Mwamposa akamatwe na kufunguliwa mashitaka" unataka ashitakiwe kwa kosa lipi hasa?
Vifo vimesababishwa watu kukanyagana, kila mtu alitaka kuwahi kukanyaga mafuta hawakutaka kufuata utaratibu walio wekewa na wahudumu - hapo ungetegemea nini kama sio maafa?
Haya mambo ya kumlahumu Mwamposa kwamba aliondoka bila ya kutoa msaada wowote - tuhuma hizo hazina ukweli wowote kwani wahudumu wake ndio wahusika wakuu wa kuongoza wahumini kukanyaga mafuta.
Kwa taarifa yako Mwamposa alazimiki kuwepo masaa yote wakati wahumini wanakanyaga mafuta, binafsi nina uhakika kwamba wakati wa stampede Mwamposa alikuwa amekwisha ondoka uwanjani.
Hapa naona mnaleta mwendelezo wenu wa kampeini za kumpiga vita Mwamposa, kinacho endelea hapa nyinyi mnakuwa driven by wivu mkishirikiana na washindani wake ambao waliwahi kupendekeza kwa JPM eti "akina Mwamposa na WRM awafunge na kupiga marufuku dini zao!"
Kwani dini ndiyo zinafanya watu kuwa manyani? Au huu unyani wetu unataka kutupia lawama kwenye dini?Dini.
Endeleeni kuamini huyo jamaa yenu toka juu atashuka tu kudadeki. Tukiitwa nyani tunapiga kelele ila the majority wana-act ka monkeys.
Jamani, kwanini aliweka mafuta machache mpaka watu wakanyagane hivo, hakukua na utaratibu wowote ile kukanyaga kwa zamu labda duh, hii inaonesha jinsi watu tuko desperate, matatizo, kiasi ukiambiwa chochote unafata tu so sad.
Sent using Jamii Forums mobile app
Pamoja na Mungu kuendelea kuwaumbua hawa manabii wa uongo lakin mijitu imeendelea kuzba macho na maskio yao. Alianza kumuumbua Mzee wa upako,akaja Gwajima na sasa Mwamposa. Chaajabu wiki ijayo ukienda kanisani utakuta mijitu bado imejaa ikisubiri kununua mafuta ya upako.
Sjui Mungu atumie mbinu gani kutuonyesha kuwa hawa ni manabii wa uongo?
Sent using Jamii Forums mobile app
Usizunguke. Hii mwamposa tayari katoa kafara maisha ya watu wasio na hatia, tena mwanzoni kabisa mwa mwaka. Kwani ndiyo mara yake ya kwanza kuwakanyagisha watu hayo matunguli yake?
Hata uchagani wapo kumbe wajinga? Mbona huwa mnasema humu kuwa wachaga wamesoma sana? Au hawakuelimika? Pole zao!