Moshi: Watu 20 wapoteza maisha kwa kukanyagana kwenye Ibada ya Mwamposa; Polisi wathibitisha kumshikilia

Moshi: Watu 20 wapoteza maisha kwa kukanyagana kwenye Ibada ya Mwamposa; Polisi wathibitisha kumshikilia

Watu wengi wanatafuta upako badala ya kumtafuta Mungu mwenye upako.

Watu wengi wanatafuta utajiri badala ya kumtafuta Mungu mwenye utajiri

Yeye(MUNGU) anasema utafuteni kwanza ufalme Wake na enzi yake na hayo mengine yote mtazidishiwa.
Watu wanatafuta kuzidishiwa kabla hawajautafuta ufalme wa Mungu.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu hafanyi jambo bila kuwasiliana na nabii


Mungu kamuumbua kuwa ni tapeli , Maana Mungu angemuonesha kuna maafa yanatokea

Nilishasema humu hawa manabii wa Uongo watawamalizeni ,wamewafilisi sasa wanawatoa kama kafara ,mtakufa sana tu maana mmeacha Neno La Mungu na kuwafata matapeli .
 
Huyo mchungaji hata hakamatwi? Kama hayupo kizuizini mpaka sasa basi serikali imeoza, ikafukiwe tu tuendelee na maisha yetu.
Akamatwe kwa kosa gani wakati alikuwa na vibali vyote vya kusanyiko hilo.
 
Intelejensia ya Jeshi la Polisi inaishia kwenye kuzuia mikutano ya kisiasa ya wapinzani, lakini kwenye mikutano hii ya hatari ya waganga wa kienyeji haifanyi kazi.. Kuuziwa maji yanayodaiwa yana upako ni utapeli..

Wapumzike kwa amani wote waliokutwa na umauti..
 
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Umaskini ni mbaya sana. Huyo mchungaji akamatwe haraka sana.
Kwanini akamatwe? Hakuwa na vibali? Ameshatoa maelezo take polisi na kwasasa yupo uraiani.
 
Hata uchagani wapo kumbe wajinga? Mbona huwa mnasema humu kuwa wachaga wamesoma sana? Au hawakuelimika? Pole zao!
Wewe ni ujinga kweli kama makonda. Kwani wanaoishi Moshi ni wachaga pekee? Ukiambiwa waumini waliokufa ni makabila nje ya Kilimanjaro utashangaa?
Bwege sana wewe!
 
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Umaskini ni mbaya sana. Huyo mchungaji akamatwe haraka sana.
Akamatwe ili awatoe huko darini alikowaweka kama misukule au?? Tujiulize, huu ujinga ujinga wa kuuziwa hirizi na pete za kuvuta mali kwenye makanisa, utaendelea hivi mpaka lini?? Ni nini kinawasumbua wa tz hadi kuutafuta msaada wa vitu vya hovyo kama hivi??
Mara kikombe cha babu, kijiko cha maji ya mtoto wa bikira maria na makorokoro mengineyo. Je watz tumekuwa wakiroho saana au?? Tutafuteni vyanzo vya uhitaji huu mkuu sio kuwakamata hao wajanja.
Huenda ni hali ngumu ya maisha mtu anajitafutia miujiza. Vyuma vimekaza mno huku mtaani na haswa huko kwa Kippi jicho liko huko kuwathibit mno
 
Back
Top Bottom