Moshi: Watu 20 wapoteza maisha kwa kukanyagana kwenye Ibada ya Mwamposa; Polisi wathibitisha kumshikilia

Moshi: Watu 20 wapoteza maisha kwa kukanyagana kwenye Ibada ya Mwamposa; Polisi wathibitisha kumshikilia

Wameangamia kwa kukosa maarifa. Mafuta ya upako yana tofauti gani na irizi za waganga wa kienyeji?
Ifike mahali serikali ilinde raia wake dhidi ya utapeli wa kidini.

Serikali ya CCM Mpya inapenda aina hii ya ujinga.
 
Ujinga mwingi tu, you can't believe!
Huyu mchungaji Mwamposya alikuwa hapa Moshi few months ago. Alitengeneza 'mpunga' wa kutosha, kisha amerudi kuchukua mpunga tena. Nonsense!
Anacheza na minds za Wachagga kuhusu uhaba wa ardhi na ukosefu wa ajira.
Unanunua mafuta ya alizeti kisha unamwaga ili upate baraka. Ujinga.





Sent using Jamii Forums mobile app
Hawakuelewi sasa wenzio

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ama kweli maisha yamekuwa magumu , wachaga nao wameingiwa na roho za kutaka utajiri pasipo Fanya kazi?
 
Maji ya upako, mafuta ya upako, maji ya baraka na mambo kama haya ni utapeli kama utapeli mwingine.

Huyo jamaa afunguliwe mashitaka ya uzembe na kusababisha vifo.

Mahubiri mwisho ni sa 12, yeye usiku alipata wapi kibari cha kuhubiri na kumwaga mafuta?

Watu 20 ni wengi sana, ashughulikiwe haraka sana.

Hivi mtu una akili zako timamu unauziwaje maji au mafuta unaambiwa ni ya baraka, mara maji ya mto jordan, mara sijui ujinga gani.

Mambo mengine bwana.
 
Pamoja na Mungu kuendelea kuwaumbua hawa manabii wa uongo lakin mijitu imeendelea kuzba macho na maskio yao. Alianza kumuumbua Mzee wa upako,akaja Gwajima na sasa Mwamposa. Chaajabu wiki ijayo ukienda kanisani utakuta mijitu bado imejaa ikisubiri kununua mafuta ya upako.

Sjui Mungu atumie mbinu gani kutuonyesha kuwa hawa ni manabii wa uongo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nitabezwa sana na wenye ufahamu mdogo lakini hilo lilifanyika kama kafara.. Na mwenye hiyo siri ni mhusika mkuu
Waumini 18 wa Dini ya Kikristo wamefariki dunia usiku huu mjini Moshi, wakati wakikanyagana kugombea kukanyaga mafuta ya upako katika kongamano la kidini la Mtume Boniface Mwamposa, DC wa Moshi Kippi Warioba amethibitisha

Updates: 00:45
Idadi ya watu waliopoteza maisha kwa kukanyagana imefikia 20 na uenda idadi hiyo ikaongezeka Mkuu wilaya amethibitisha.

UPDATES:

Taarifa zinaeleza kuwa baada ya tukio hilo kutokea Mhubiri huyo alielekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) akitaka kuondoka, lakini ndege aliyokuwa amepangwa kuondoka nayo ilichelewa (delayed) na ndipo Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro lilipomtia mbaroni uwanjani hapo



Chanzo: Mwananchi

Jr[emoji769]
 
Dhambi isiyo samehewa ni ya kumkashifu roho mtakatifu (Marko 3:22-30)
Ndugu zangu kwenye hili tuwe makini hasa kipindi hiki ambacho tumewapoteza wenzetu huko Moshi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nime Sadiki Maneno Ya Dk. William M.Tanzania Wa USA America
Waumini 18 wa Dini ya Kikristo wamefariki dunia usiku huu mjini Moshi, wakati wakikanyagana kugombea kukanyaga mafuta ya upako katika kongamano la kidini la Mtume Boniface Mwamposa, DC wa Moshi Kippi Warioba amethibitisha

Updates: 00:45
Idadi ya watu waliopoteza maisha kwa kukanyagana imefikia 20 na uenda idadi hiyo ikaongezeka Mkuu wilaya amethibitisha.

UPDATES:

Taarifa zinaeleza kuwa baada ya tukio hilo kutokea Mhubiri huyo alielekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) akitaka kuondoka, lakini ndege aliyokuwa amepangwa kuondoka nayo ilichelewa (delayed) na ndipo Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro lilipomtia mbaroni uwanjani hapo



Chanzo: Mwananchi

Jr[emoji769]
 
.
Sijakuelewa mkuu! Yaani wamekanyagana wakigombea kukanyaga mafuta au wakigombea kuchukua hayo mafuta?

Mungu tuhurumie Africa

Sent using Jamii Forums mobile app
tapatalk_1580597589477.jpeg


Jr[emoji769]
 
Watu 18 wamekufa leo Jumamosi Februari Mosi, 2020 baada ya kukanyagana katika harakati za kukanyaga mafuta ya upako kwenye

kongamano la Mtume Boniface Mwamposa mjini Moshi, DC wa Moshi Kippi Warioba amethibitishaView attachment 1343848

Chanzo:Mwananchi


Watu 18 Niwengi Sana Sana Jamani Tanzania Tunaangamia Kwakukosa Maarifa

Am Speechless [emoji26][emoji26]
Sent using Jamii Forums mobile app

Unyonge na Umaskini ndiyo malipo yake hayo.
 

Attachments

  • 2292603_IMG_20200201_135350.jpeg
    2292603_IMG_20200201_135350.jpeg
    36.7 KB · Views: 1
  • 2292739_tapatalk_1580554635924.jpeg
    2292739_tapatalk_1580554635924.jpeg
    87 KB · Views: 1
Wanajua mafuta ndio tegemeo lao au inakuaje?


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Waumini 18 wa Dini ya Kikristo wamefariki dunia usiku huu mjini Moshi, wakati wakikanyagana kugombea kukanyaga mafuta ya upako katika kongamano la kidini la Mtume Boniface Mwamposa, DC wa Moshi Kippi Warioba amethibitisha

Updates: 00:45
Idadi ya watu waliopoteza maisha kwa kukanyagana imefikia 20 na uenda idadi hiyo ikaongezeka Mkuu wilaya amethibitisha.

UPDATES:

Taarifa zinaeleza kuwa baada ya tukio hilo kutokea Mhubiri huyo alielekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) akitaka kuondoka, lakini ndege aliyokuwa amepangwa kuondoka nayo ilichelewa (delayed) na ndipo Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro lilipomtia mbaroni uwanjani hapo



Chanzo: Mwananchi
Maisha magumu watu wanaona pengine wataponea kwa manabii japo wengi ni manabii wa uongo.

Nawaza walikuwa wanamtumikia Mungu gani ambaye hawezi hata kuzuia vifo vya watu kukanyagana?? I guess it was a satanic mass.
 
Back
Top Bottom