Mossad yatajwa kutibua shambulio dhidi ya Waisraeli katika nchi za Tanzania, Ghana na Senegal

Mossad yatajwa kutibua shambulio dhidi ya Waisraeli katika nchi za Tanzania, Ghana na Senegal

Sam Gidori

Senior Member
Joined
Sep 7, 2020
Posts
165
Reaction score
417
Watu watano wanaripotiwa kutiwa mbaroni katika nchi za Tanzania, Ghana na Senegal wakihusishwa na jaribio lililotibuliwa la shambulio dhidi ya Watalii wa Israel, Kituo cha Televisheni cha Channel 12 cha Israel kimeripoti.

Kituo hicho kimenukuu taarifa za kiintelijensia zikionesha kuwa watu hao waliokamatwa walipata mafunzo ya Wapiganaji wa Quds wenye mafungamano na Jeshi la Iran (Islamic Revolutionary Guards Corps), ikiongeza kuwa kukamatwa kwao kumetokana na taarifa za Majasusi wa “Magharibi.”

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Watano hao walipewa mafunzo na vifaa, ambayo havikubainishwa, kutoka Lebanon na kutumwa katika mataifa hayo ya Afrika chini ya mwamvuli wa kuwa Wanafunzi wa Kidini, wakiwa na ‘misheni’ ya kuwatafuta watalii wa Kiyahudi na kuwashambulia.


Ripoti hiyo imetaja Shirika la Upelelezi la Israel (Mossad) kuhusika na kutibua mpango huo, bila kubainisha hasa kuhusika kwake ni kwa namna gani. Hakuna uthibitisho uliotolewa kutoka mataifa yote yaliyohusika (Israel, Iran na nchi za Afrika). Iran imekana kuhusika, ikisema madai hayo hayana msingi wowote.

Watu wote hao wamekamatwa kabla hawajafanikiwa kutekeleza azma yao, kwa mujibu wa ripoti, bila kubainisha hasa mahali walipokamatwa, huku ikitaja kuwa washambuliaji hao wanaendelea kufanyiwa mahojiano.


Chanzo: Times of Israel

AP18103515670855-640x400.jpg
 
Israel wanataka kuanzisha kampuni Tanzania.
Itarahisisha kufanya upelelezi kwenye issues kama hizi na kuchukua hatua wenyewe kushughulikia uharifu

Wakimwachia Kamanda Siro watakuja kujuta wapo busy na kesi za ugaidi

Hii miongoni mwa sababu za Israel kufungua kampuni
 
Israel wanataka kuanzisha kampuni Tanzania.
Itarahisisha kufanya upelelezi kwenye issues kama hizi na kuchukua hatua wenyewe kushughulikia uharifu

Wakimwachia Kamanda Siro watakuja kujuta wapo busy na kesi za ugaidi

Hii miongoni mwa sababu za Israel kufungua kampuni
Tunawakaribisha kwa sauti moja, wafungue na matawi mikoani
 
08 November 2021
Tel Aviv, Israel

Iranian plot to attack Israelis, Jews said foiled in Africa​

Five arrested in Ghana, Senegal and Tanzania on suspicion of planning attacks against tourist or business people, after being trained in Lebanon, channel 12 news reports



The terrorists, from the Iranian Quds Force, have reportedly been trying for months to target Israeli businessmen in Senegal and Ghana, as well as in Tanzania, where Israelis are used to going on safari.

Iran is trying to avenge the November 2020 assassination of scientist Mohsen Fakhrizadeh, which Tehran blames on Israel.
Source : i24News is an independent English-language media company based in Tel Aviv that provides daily news and entertainment to its viewers.
 
Watu watano wanaripotiwa kutiwa mbaroni katika nchi za Tanzania, Ghana na Senegal wakihusishwa na jaribio lililotibuliwa la shambulio dhidi ya Watalii wa Israel, Kituo cha Televisheni cha Channel 12 cha Israel kimeripoti.

Kituo hicho kimenukuu taarifa za kiintelijensia zikionesha kuwa watu hao waliokamatwa walipata mafunzo ya Wapiganaji wa Quds wenye mafungamano na Jeshi la Iran (Islamic Revolutionary Guards Corps), ikiongeza kuwa kukamatwa kwao kumetokana na taarifa za Majasusi wa “Magharibi.”

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Watano hao walipewa mafunzo na vifaa, ambayo havikubainishwa, kutoka Lebanon na kutumwa katika mataifa hayo ya Afrika chini ya mwamvuli wa kuwa Wanafunzi wa Kidini, wakiwa na ‘misheni’ ya kuwatafuta watalii wa Kiyahudi na kuwashambulia.


Ripoti hiyo imetaja Shirika la Upelelezi la Israel (Mossad) kuhusika na kutibua mpango huo, bila kubainisha hasa kuhusika kwake ni kwa namna gani. Hakuna uthibitisho uliotolewa kutoka mataifa yote yaliyohusika (Israel, Iran na nchi za Afrika). Iran imekana kuhusika, ikisema madai hayo hayana msingi wowote.

Watu wote hao wamekamatwa kabla hawajafanikiwa kutekeleza azma yao, kwa mujibu wa ripoti, bila kubainisha hasa mahali walipokamatwa, huku ikitaja kuwa washambuliaji hao wanaendelea kufanyiwa mahojiano.


Chanzo: Times of Israel

AP18103515670855-640x400.jpg

Misura yao inatisha na miwasiwasi mingi kwelikweli, laana co ki2 kizuri.
 
Israel wanataka kuanzisha kampuni Tanzania.
Itarahisisha kufanya upelelezi kwenye issues kama hizi na kuchukua hatua wenyewe kushughulikia uharifu

Wakimwachia Kamanda Siro watakuja kujuta wapo busy na kesi za ugaidi

Hii miongoni mwa sababu za Israel kufungua kampuni

Mama samia hatathubutu kuwapa nafasi mashoga/magaidi kwenye ishu kama hizi.
 
Back
Top Bottom