‘Motivational Speakers’ wanaweza kuharibu maisha ya waajiriwa

‘Motivational Speakers’ wanaweza kuharibu maisha ya waajiriwa

OLS

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2019
Posts
426
Reaction score
685
Ni kwa muda mrefu wafanyakazi wamekuwa wakiambiwa wanafanya kazi za kitumwa. Mawazo kama haya yako tangu zamani sana.

Wakati wa vita baridi kati ya Usoshalisti na Ubepari, nchi nyingi za Afrika zilisema hazina upande lakini baadae wakaelemea kwenye Usoshalisti, taifa kama Tanzania likaweka kitu chake kilichoitwa ‘ujamaa’

Ili kufanya wafanyakazi wawachukie mabosi wao, Ujamaa ukasema kuwa matajiri ni wanyonyaji wa wafanyakazi, wafanya biashara ni wanyonyaji wa wakulima. Kwa sera zilizoshindwa kuangalia mazingira halisi.

Watu wakaiamini serikali na kwenda serikalini, na wengine kuacha kuwauzia wafanyabiashara wakubwa. Matokeo yake wakaanza kulalama maslahi madogo, yaani wakaona walipokuwa wanaambiwa wananyonywa kulikuwa na maslahi kuliko huku ambapo waliambiwa kuko vizuri.

Kwa sababu hiyo kukawa na migomo ya kimya kimya, ambayo ilitekelezeka kwa uvivu makazini hali iliyopelekea shughuli za serikali kuzorota. Kwenye biashara, raia wakaanza kupeleka biashara zao nje, ili kupata maslahi maana serikali ilikuwa inanunua kwa bei ya chini sisiyo ridhisha. Hapo biashara za magendo zikapanda chati.

Kwa sasa wameibuka vijana waliojiajiri kuongea, motivational speakers, ambao kiuhalisia wanapita mulemule ambapo Sera za Ujamaa zilipita na kusababisha majanga. Wafanyakazi wanaaminishwa kuwa wananyonywa na wengine wanaoamini huacha kazi na kujikuta katika hali mbaya zaidi mitaani.

Mifano wanayotumia kuwaonyesha watu waliofanikiwa haizingatii sheria za kitakwimu bali huamua kuwataja wachache waliofanikiwa ambao pia huwa hawaangalii sababu nyingine za kufanikiwa kwao.

Sikatai kwamba ni vizuri mtu kuwa na biashara zake lakini, kutumia 100% ya hela uliyojisevia ya mashahara kwenye biashara ni kujiua kwa kuwa biashara ina vitu vingi hujitokeza katikati.

Kwa kuwa biashara inataka kuongezewa hela mara kwa mara, kunakuwa na haja ya kuwa na chanzo cha mapato ili kuifinance biashara yako ambayo inaweza kuwa mikopo au mshahara unaoupata kwenye kazi yako.

Wapo wengi wanabiashara kubwa lakini pia bado wameajiriwa na wanapata mapato zaidi ya sehemu moja.

Kwa wafanyakazi wote, ni vyema kusoma zaidi masuala ya kibiashara na sio kufuata ushauri wa motivational speaker ambaye hajui kitu kuhusu biashara yasije kutokea kama yanayowakuta wengine.

Signed



OEDIPUS
 
86453ADF-2E84-408D-A86D-630007838A96.png
 
Ni kweli mkuu, hawa watu wamegeuza maskini, wanawake na wasiojielewa kuwa ni fursa
 
Akili za kuambiwa changanya na zako mkuu,kwenye maisha ni vyema kutumia akili yako vizuri..
 
Aaah jamaa wajinga sana, wanapotosha [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]eti jiajiri pumbaf
 
Motivational speakers wengi hawana hata biashara
Motivational speaking ndio “biashara” yao. Wanawakusanya kwa kiingilio say cha 15,000/- na mkiwa mia tu, keshapiga hela ndefu.

Mtu unaweza kuwa “motivated” but without moving your ass and actually do something, hakuna kufanikiwa. Mimi hata siwasikilizi hao watu wanaopiga porojo tu wala kusoma vitabu vyao. Ni bora nikamsikilize mtu anayefanya business kwa vitendo maana anaweza kunipa real-life & practical experience
 
Kwa mtu makini anayefahamu management, marketing, logistics na economics akisikia hao jamaa atacheka sana..
Nadhani wanafanya kazi kwa kuwalenga watu wasiosoma vitabu vya maswala tajwa hapo juu.

Mfano:
Jiulize tu kwa nini unataka kufanya biashara?
Je biashara ni utajiri?

Unataka kipato cha aina ipi na kwa kutoa bidhaa au huduma ipi?
Muda unao wa kufanya kazi ya ziada?(kama umeajiriwa)

Ukipewa hamasa mipango ndio inatimia ukiifanya au kuna vitu vitahitajika,je unavyo? Itakugharimu muda gani angalau kupata faida ya juu zaidi (supernormal profit)

Note:
Mafanikio ya biashara ni tofauti na maneno ya kuhamasishwa..lazima uweze kufanya mipango sahihi na kwa wakati husika na kuweza kukadiria vyema.
 
mleta thread ni motivation speker yupi ambae unamzungumzia hapa,maana nnavyojua ili uwe motivation spiker ni lazma unachokimotivate uwe umekifaulu na uwe kwenye hatua kubwa
Kwa Tanzania ni karibia wote, huwa wanasoma tu vitabu na kutengeneza madini kwa kiswahili then wanaweka viingilio. Ila ukiangalia katika positive side wanasaidia kiasi kuamsha watu tuliolala
 
Kitu chakuzingatia ni uwe na vyanzo vingi vya mapato chochote kinachokuingizia pesa kiheshim sana na kitunze sana
 
Motivational speaking ndio “biashara” yao. Wanawakusanya kwa kiingilio say cha 15,000/- na mkiwa mia tu, keshapiga hela ndefu.

Mtu unaweza kuwa “motivated” but without moving your ass and actually do something, hakuna kufanikiwa. Mimi hata siwasikilizi hao watu wanaopiga porojo tu wala kusoma vitabu vyao. Ni bora nikamsikilize mtu anayefanya business kwa vitendo maana anaweza kunipa real-life & practical experience
Kuna jamaa yangu kila mwaka kama wa 4 ana attend hizo semina na kujipa moyo kwamba ipo siku atafungua biashara yake lakini hakuna anachofanya
 
Back
Top Bottom