‘Motivational Speakers’ wanaweza kuharibu maisha ya waajiriwa

‘Motivational Speakers’ wanaweza kuharibu maisha ya waajiriwa

Motivational speakers wanawaambia watu kitu ambacho watu wanapenda kusikia. Wanafahamu kuwa watu wengi wanapenda kujiajiri, hivyo na wao wanaingia na gia hiyo hiyo.

Ukweli ni kwamba, sio kila mtu anaweza kujiajiri. Kujiajiri sio jambo la uamuzi tu, bali ni jambo ambalo linategemea uwezo wako pia. Kwa watu wengine kuajiriwa ni uamuzi mzuri zaidi. Wapo watu walioajiriwa na wamefanikiwa katika maisha. Ingawa ni wachache, lakini hiyo inaonyesha kufanikiwa katika ajira ni kitu kinachowezekana, na wewe unaweza kuwa mmoja kati ya hao wachache.

Ushauri wa motivational speakers ni ushauri wa "jumla". Ushauri mzuri ni ushauri ambao ni "personal". Badala ya kuwafuata motivational speakers, ni bora kuwa na "personal coach/adviser" mtu ambae atakupa ushauri kwa kuzingatia mazingira yako, uwezo wako, vipaji vyako etc.
 
NILIANZA BIASHARA YANGU YA KUKU NA MANYOYA MAWILI

Hivi wanatuonaje lakini?

Mtu unakengeuka unaacha kazi ya maana kisa maneneo ya kuambiwa?

Mara uza simu ufuge kuku, mara lima matikiti...yeye muulize sasa utakavyoshangaa
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16] kuna jamaa alining'ang'ania kuingia forever ehheehhehe, adi kutaka kunikopesha hela. Yaan ww bwana Gerald, sijui saiv utajiri wako ni kiasi gani..utakua unakaa meza moja na tajiri Mwamedi.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Haukumuuliza mbona yeye hajafika hiyo level na kakutangulia?
 
Jamaa mmoja rafiki yangu motivational speaker alitunga kitabu jinsi ya kupata mafanikio maishani uwe na kipato kizuri.
Wakati anakizindua akaniomba hela akizindue.
Nikamuambia kasome kitabu chako utapata mafanikio.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom