Movie: Kanumba na Arnold Schwarzenegger

Movie: Kanumba na Arnold Schwarzenegger

Kuzitazama filamu za kitanzania inataka uwe umejitoa akili kwa kiwango fulani...huku ukiwa umeshatupia viroba kadhaa kichwani...maana ukitumia akili ya kawaida wanaweza wakakusababishia ukaipasua tv yako kwa hasira ya madudu yanayofanyika humo.....kwa kifupi filamu zetu zinatia kinyaa kwani hakuna tunachokiona humo zaidi ya chupi na mapaja ya wadada..wanaoitwa wasaniii..

hahahaaaa mkuu nilifikir ni mimi peke! niliwahi enda nyumba ya mtu nikakututa wanaangalia nilichoka nilipokutana na kipande kwenye subtitle BABU anaitwa OLDMAN
 
Kuzitazama filamu za kitanzania inataka uwe umejitoa akili kwa kiwango fulani...huku ukiwa umeshatupia viroba kadhaa kichwani...maana ukitumia akili ya kawaida wanaweza wakakusababishia ukaipasua tv yako kwa hasira ya madudu yanayofanyika humo.....kwa kifupi filamu zetu zinatia kinyaa kwani hakuna tunachokiona humo zaidi ya chupi na mapaja ya wadada..wanaoitwa wasaniii..

Ume-Hack kichwa changu wewe, kwakua maelezo kama haya nilikua nimeyawka kwenye folder la ujinga na sanaa za kijinga.. Sema ume edit kidogo!
Big like
 
Inawezekana alikuwa muigizaji mzuri...

Ila kufikia level za schwarzenegger??? Labda schwarzenegger wa kichina...

Kweli nakubaliana na ww kua Schwarzenegger ni untouchable levels kibongo bongo, sema kwa juhudi za yule jamaa kanumba inawezekena angeshafikia kiwango hicho.. Si unakumbuka alishawah kumleta yule bishoo wa nollywood na akaigiza nae (ramsey noah) sijui ndo jilake hilo!... Na huyo jamaa kule Nigeria ni nguli hatari..

Pia sikusema kuigiza au kua na kipaji kama cha Schwarzenegger bali kuigiza nae...
 
Bongo mavii ni shida tupuu....siwezi kuangalia muvi za kbongo nikiwa na wazaz wangu nitaaibikaa bure.
 
Kudhania kuwa Kanumba angeleta mabadiliko kwenye tasnia ya filamu ni hisia zaidi kuliko uhalisia....na sina ugomvi na wanaodhani hivyo.

Ila mimi nataka nitazame kwa angle nyingine...inawezekana kuwa tulivutiwa na harakati za Kanumba katika kujitangaza nje ya nchi lakini lazima tutofautishe SANAA na HARAKATI....Tanzania tuna tatizo la sanaa (tasnia) na sio harakati za kujitangaza.

Inawezekana kuwa Marehemu Kanumba kama bado angekuwepo angekuwa ameshafika mbali kwenye kujitangaza nje ya Tanzania, nchi kama Nigeria,Ghana, Congo, Rwanda n.k....lakini hebu tujiulize hizo muvi zote ambazo Marehemu aliwashirikisha wasanii wa nje zina lipi jipya ? mpaka leo hii nikiiangalia muvi ya DEVIL KINGDOM aliyomshirikisha Ramsey sioni cha maana zaidi tu ya kujifurahisha na uwepo wa huyo Ramsey.

To cut a long story short ni kuwa tuna tatizo la KISANAA na mfumo duni wa kuendesha tasnia ya filamu, na hata Marehemu angekuwepo kamwe asingeweza kurekebisha chochote, zaidi yeye angeendeleza juhudi zake zilizokuwa zinamjenga zaidi yeye binafsi, ingawa pia hii sio dhambi coz wakati mwingine kila mtu na bahati yake...unaweza kuwa na wakati mzuri maishani hata kama unachofanya hakina thamani hiyo...na hili hutokea kwa mmoja kati ya milioni...ni uwepo wa misingi mizuri ya sanaa ndio utaibadilisha tasnia na sio Msanii mmojammoja.
 
Mpeni sifa zote hapa bongo lakini kumuweka level moja na Arnold Schwarzenegger ni sawa na kufananisha kifo na usingiIzi in short they are not comparable...
 
FYATU nimekusoma sana ktk maelezo yako na hakika nimekuelewa, ni kweli jamaa asingeweza kuleta mabadiliko directly but ange yaleta ki indirect maana yangu ni kama ifuatavyo:-

Kumbuka kanumba alisoma mpaka f6 pale jiteute huku akiwa ktk maigizo kaole lakini baadae akaona anahitaji kuongeza elimu ya sanaa ya kuigiza baadae akaenda pale bwagamoyo kupiga kozi ya maigizo...
KWA MAANA HII, labda huko mbeleni angeongeza ujuz wa kujifunza zaidi na hata kuinvest more kwenye knowledge na skills za sanaa ya maigizo na lastly ange hit angles za Hollywood.. Who knows?

Pia kumbuka kumove to nigeria na ghana, ilikua ni first move ever to be made by tanzanians kwenye tasnia ya kuigiza and thus paved a way to other artists kuanza kufikiri beyond the imaginary lines.. Kumbuka akina monalisa, pasta miyamba, masanja n.k...
MAANA YANGU ktk hili ni kua baada ya move hii alio kua amepiga na tunaskia alienda mpaka mtoni kwa obama kisanaa, ilianza kuleta chachu kwa wasanii wengine na hata kupelekea kuanza kufikiri otherwise kuhusu soko la kazi zao.

Matumizi ya lugha ya kigeni, kanumba alikua ni msanii wa kwanza kuforce kutumia ngeli ktk kazi zake na ikapelekea bonge la scandal baada kuhudhuria pale BBA, ila baadae tuliona muamko ktk kuanza kufikiri namna gan lugha nyingine zinaweza zikaanza kuotanua soko la kazi zao, kwa mantiki hii watu wwngine wangelifanyia ubunifu zaidi na wakaona namna gani wajipenyeze kimataifa.

But mkuu FYATU Inabidi tuamini kua pengine labda sanaa hii asinge ibadilisha yeye moja kwa moja lakini kupitia influence ange badili huu mchezo ki ujumla.. Refer mziki wa bongo flavor, utagundua vijana wanao onekana kuubadili muzik sio wao sio wale walio anziaha harakati hizo, bali ni wengine na hawa wa sasa wametake over..

And that's what would have been happened if this great guy was still alive!
 
Last edited by a moderator:
Moja ya tatizo kubwa linaloikabili tasnia yetu ni uwepo wa watu wasio sahihi kwenye tasnia...kuanzia Waigizaji mpaka Wasmbazaji mpaka wenye dhamana na Wizara ya sanaa.

Miaka ya tisini Watanzania walifanya mapokezi mazuri kwa sanaa yetu ya uigizaji, haswa baada ya ITV kuonyesha kuwa Watanzania wanalo la kufanya pia, ila kwa bahati mbaya mapokezi hayo yakaangukia kwenye mikono isiyo sahihi.

Na kama ilivyo udhaifu wa Mtanzania tamaa ya pesa huwekwa mbele kwenye kila jambo, kama wanafanya wengi wa viongozi wetu na watendaji wa Serikali, tuli/tunashuhudia jinsi ambavyo Wasanii wenyewe kuingia tamaa na kutamani kuhodhi kila kitu kinachohusu uandaaji wa muvi bila kujali weledi, na aliyekuja kushindilia jeneza kwenye hilo ni Msambazaji/Wasambazaji.

Wasambazaji walishikana mikono na Wasanii,na hii ni kwa kuwa tu usambazaji ulihitaji mtaji mkubwa ambao wasanii hawakuwa nao otherwise wasanii wangekaba kote, athari hizi ndizo zilizoendelea mpaka leo hii, na Wasanii waliotangulia ndio wa kulaumiwa pakubwa kwa jinsi walivyoshindwa kutumia vizuri MAPOKEZI ya Watanzania kwao na kutanguliza tamaa.

Tofauti na Msambazaji, Wasanii walipaswa kukaa chini na kutumia akili badala ya kuichukulia filamu kama jambo rahisi tu, leo hii tasnia ikipotea Msambazaji atabadili biashara na kumuacha Msanii anag'aa macho. Wasanii na Wasambazaji "walichangamkia tenda" hawakujali Filamu inahitaji nini kuwa Filamu, vigezo pekee walivyoshinikiza Wasambazaji ni UMAARUFU na sio sanaa, unatengeneza nini halikuwa la maana kwao, Msanii anapatana na Msambazaji, hivyo anaburundaburunda ilimradi Filamu ikamilike, then inakimbizwa sokoni bila kujali Washabiki wao.

Filamu ni team work, hivi kweli umpe JB au RAY milioni thelathini aandae muvi utegemee aumize kichwa kuandaa team ? atakachofanya ni kukusanya jamaa/rafiki zake na kuburundaburunda tu, na mfumo huu ulipelekea baada ya muda kila Msanii kutamani kuwa PRODUCER.

Nchi zote zenye akili timamu wamewekeza kwenye PRODUCERS na sio Wasanii haohao kujigeuza PRODUCERS (hapa nazungumziaa Producers kwa weledi sio Financiers), ni Producer aliyekaa darasani pekee ndiye anaweza kujua umuhimu wa SCREENWRITERS, CINEMATOGRAPHER, DIRECTOR, EDITOR n.k., ni Producer pekee ndiye ana/angeweza kumshauri Msambazaji kuwa haiwezekani kuandaa filamu ndani ya mwezi mmoja, au kukataa mambo ya pati one na two, au kutafuta Screen plays zenye ubora badala ya Msanii kujiandikia tu chochote na kuita Screenplay n.k.

Kwa hiyo kina JB, Ray, Richi, Cloudi ni wa kubebesha lawama kwa ujinga wao, na inahitaji nguvu kubwa sasa ili kufufua tena imani ya Watanzania, na kama bado kuna wanaodhani kuwa Tasnia ya Filamu haijayumba watakuwa wanazidanganya nafsi zao, Washabiki wengi wamehamia kwenye kazi za Kiharamia za kina Rufufu na wenzake, sina utafiti rasmi lakini nimeshuhudia hivyo pakubwa.
 
Moja ya tatizo kubwa linaloikabili tasnia yetu ni uwepo wa watu wasio sahihi kwenye tasnia...kuanzia Waigizaji mpaka Wasmbazaji mpaka wenye dhamana na Wizara ya sanaa.

Miaka ya tisini Watanzania walifanya mapokezi mazuri kwa sanaa yetu ya uigizaji, haswa baada ya ITV kuonyesha kuwa Watanzania wanalo la kufanya pia, ila kwa bahati mbaya mapokezi hayo yakaangukia kwenye mikono isiyo sahihi.

Na kama ilivyo udhaifu wa Mtanzania tamaa ya pesa huwekwa mbele kwenye kila jambo, kama wanafanya wengi wa viongozi wetu na watendaji wa Serikali, tuli/tunashuhudia jinsi ambavyo Wasanii wenyewe kuingia tamaa na kutamani kuhodhi kila kitu kinachohusu uandaaji wa muvi bila kujali weledi, na aliyekuja kushindilia jeneza kwenye hilo ni Msambazaji/Wasambazaji.

Wasambazaji walishikana mikono na Wasanii,na hii ni kwa kuwa tu usambazaji ulihitaji mtaji mkubwa ambao wasanii hawakuwa nao otherwise wasanii wangekaba kote, athari hizi ndizo zilizoendelea mpaka leo hii, na Wasanii waliotangulia ndio wa kulaumiwa pakubwa kwa jinsi walivyoshindwa kutumia vizuri MAPOKEZI ya Watanzania kwao na kutanguliza tamaa.

Tofauti na Msambazaji, Wasanii walipaswa kukaa chini na kutumia akili badala ya kuichukulia filamu kama jambo rahisi tu, leo hii tasnia ikipotea Msambazaji atabadili biashara na kumuacha Msanii anag'aa macho. Wasanii na Wasambazaji "walichangamkia tenda" hawakujali Filamu inahitaji nini kuwa Filamu, vigezo pekee walivyoshinikiza Wasambazaji ni UMAARUFU na sio sanaa, unatengeneza nini halikuwa la maana kwao, Msanii anapatana na Msambazaji, hivyo anaburundaburunda ilimradi Filamu ikamilike, then inakimbizwa sokoni bila kujali Washabiki wao.

Filamu ni team work, hivi kweli umpe JB au RAY milioni thelathini aandae muvi utegemee aumize kichwa kuandaa team ? atakachofanya ni kukusanya jamaa/rafiki zake na kuburundaburunda tu, na mfumo huu ulipelekea baada ya muda kila Msanii kutamani kuwa PRODUCER.

Nchi zote zenye akili timamu wamewekeza kwenye PRODUCERS na sio Wasanii haohao kujigeuza PRODUCERS (hapa nazungumziaa Producers kwa weledi sio Financiers), ni Producer aliyekaa darasani pekee ndiye anaweza kujua umuhimu wa SCREENWRITERS, CINEMATOGRAPHER, DIRECTOR, EDITOR n.k., ni Producer pekee ndiye ana/angeweza kumshauri Msambazaji kuwa haiwezekani kuandaa filamu ndani ya mwezi mmoja, au kukataa mambo ya pati one na two, au kutafuta Screen plays zenye ubora badala ya Msanii kujiandikia tu chochote na kuita Screenplay n.k.

Kwa hiyo kina JB, Ray, Richi, Cloudi ni wa kubebesha lawama kwa ujinga wao, na inahitaji nguvu kubwa sasa ili kufufua tena imani ya Watanzania, na kama bado kuna wanaodhani kuwa Tasnia ya Filamu haijayumba watakuwa wanazidanganya nafsi zao, Washabiki wengi wamehamia kwenye kazi za Kiharamia za kina Rufufu na wenzake, sina utafiti rasmi lakini nimeshuhudia hivyo pakubwa.

Technically your correct!
 
Mpeni sifa zote hapa bongo lakini kumuweka level moja na Arnold Schwarzenegger ni sawa na kufananisha kifo na usingiIzi in short they are not comparable...

Mkuu nilitaka kusema umekurupuka ila naona sio neno zuri kwako, kwahyo nalifuta bali nitasema umeenda kwa kasi..

Sisi, hasa mimi hatu/sifananishi uwezo, weledi na kila kitu cha Anorld bali naongelea KUMSHIRIKISHA katika kazi zake kutokana na juhudi za marehem alizokua nazo,

Pia kauli hii ya kanumba na Schwarzenegger inaweza isieleweke vyema ukikimbilia kuwafananisha lakini ukaielewa vizuri wakati wa kutafsiri juhudi za kanumba..

Kwa mfano mtu akisema, "mwanangu anavyo jituma darasani mimi naamini kuna siku atakuja kua raisi wa nchi yetu".. Je wewe ktk maneno ya mzazi huyu umeelewa nini?
 
And that's what would have been happened if this great guy was still alive!

Impact kwa tasnia nzima isingekuwa kubwa kihivyo kwani naye alikuwa anakumbatia mfumo huuhuu unaoiangamiza tasnia leo hii.
 
Pengo lake halifutiki wala kuzibika.Enzi zile nilikua naweza hata kuangalia movie za hapa nyumbani japo mara moja moja ila tokea atangulie mbele za haki sijui hata jina la filamu yoyote ya kibongo.

Cjawahi kuwa na filam ya kibongo baada ya kufa kanumba
 
Impact kwa tasnia nzima isingekuwa kubwa kihivyo kwani naye alikuwa anakumbatia mfumo huuhuu unaoiangamiza tasnia leo hii.

Lakini matokeo yake yasingekua kama tunavyoona tasnia ilivyo sasa, ingekua somewhere huko!
 
Ni miaka mi3 sasa toka huyu jamaa atutoke duniani, lakini pengo lake linajidhihirisha kila kukicha..

Jamaa alishapiga hatua nyingi za kuonesha kua alikua anaelekea kwenye mafanikio zaidi ya kimaigizo kwa tanzania, na nathubutu kusema kua huyu jamaa angeshafikia kiwango cha kuigiza na magwiji wa Hollywood kama akina Schwarzenegger na wengine wengi..

Ushahidi wa hayo upo na wala haupingiki, na baaadhi ya juhudi tulikua tumeshaziona!

Pia hawa wasanii waliobaki naona kama wanazidi kukera kila kukicha hakuna wanachofanya, yaani ni ushenzi mtupu...

Kuna huyu jamaa RAY alikua anajifanya ndio mbadala wa kanumba lakini siku hizi simsikii, yaani kwa kifupi kafulia...

Dah kweli pengo lako halitofutika mkuu.. R.i.p


wabongo hamjui Movie, hamjui namna movie zinavotengenezwa, na pia hamjui hata muige movie gani ili muweze kuwa juu.

kanumba hakuwai kuwa bora kati ya waigizaji bora Afrika.
viwango vya kumfananisha Kanumba na waigizaji bora Africa havipo.
 
wabongo hamjui Movie, hamjui namna movie zinavotengenezwa, na pia hamjui hata muige movie gani ili muweze kuwa juu.

kanumba hakuwai kuwa bora kati ya waigizaji bora Afrika.
viwango vya kumfananisha Kanumba na waigizaji bora Africa havipo.

Mhhh, we mwenzetu ni mnini? Maana inaonekana si mmbongo
 
Daa! Acha tu kwa kanumba watasubiri sana, hakunaga kama yeye ray ni mzigo tu hakuna analofanya
 
Back
Top Bottom