Johnny Sins
JF-Expert Member
- Nov 4, 2019
- 2,537
- 3,873
Aliletwa kutoka sayari ya mbali akiwa kwenye mwili wa binadamu kwa nje,ila kwa ndani ni cyborg muuaji..katengenezwa na vyuma maalumu vinavyomuwezesha kufanya anachojisikia hapa duniani..
Lengo ni kumuua sarah connor,kwa sababu hao waliomleta arnord kutoka mwaka 2029 mpaka mwaka 1984 kwa kazi hiyo tu. Ni kitengo maalumu katika sayari ya mbali kinachojiita skynet..skynet walijua kuwa sarah atapata mimba na atajifungua mtoto ataekuja kuwa ni serious machine kuliko uwezo wao..arnord akatumwa kazi ikamshinda.
Ndio ilimshinda,sababu katika hali isiyo ya kawaida anashuka kiumbe mwingine mwenye asili kama ya arnold kwa ajili ya kumlinda sarah..ikawa ni vita ya kisayansi..yenye ufundi mkubwa wa matumizi ya technology.
TERMINATOR ONE IKAISHA
Sarah akajifungua na baada ya miaka saba,yeye akiwa hajui kuwa mwanae ni ufunguo wa vizazi vijavyo vya kutengeneza robot zenye nguvu kubwa kuliko viumbe vyote vya kisayansi.
Anatumwa tena Terminator kutoka miaka ya mbele kuja mwaka 1991 kumuua john connor..anaitwa T-1000..wahuni tulimuita uji uji, Judgement Day, jamaa hafi kwa risasi wala bomu, ni machine kweli.
Ni Arnold Shwarzenegger tena. Akitumia jina la T-800 safari hii analetwa kuhakikisha john na mama yake wanakuwa salama..john akiwa kama ndo mwenye umiliki wa kila anachofanya arnorld kama machine.
Inapigwa vita ya kisayansi isiyo na mfano.ni mwendo wa vyuma na ubabe tu..arnold anashinda na kupotea pamoja na T-1000 kwenye saruji ya moto,akimuacha john na mama yake wakiwa salama.
TERMINATOR TWO IKAISHA..
Maisha yakaanza vizuri,yakaisha vibaya..skynet walim trace john wakaaamua kufanya azma nyingine,akaletwa tena kutoka miaka ya mbele kuja miaka ya nyuma mwanamke,rise of the machine nyingine..T-X..sababu skynet ni mafundi juu ya viumbe hao..
John afanyeje na kifo kinamuandama..alichokuwa hajui john ni kuwa skynet walimjua yeye tangu yupo tumboni,na yeye hajui kuwa anachokijua yeye akiamua kukitumia basi skynet hawamuwezi,ndo maana wamemuandama tangu mtoto..
Hakuaachwa hivi hivi ni rafiki yake wa tangu utotoni, ni Arnorld tena..anakuja kuhakikisha John anajjijua ye ni nani hapa duniani, kutoka sayari ya mbali kabisa tena ya miaka ijayo,battle inaanza upya na kila vita ni yenye ufundi mpya pia.
Mwanaume anashinda tena na kumuacha John salama huku akimwachia kila alijualo kuhusu technology na kwamba pamoja na kuwa Arnold anaonekana kufa. John asisite kutumia alichoachiwa kama njia ya kumleta tena Arnorld mpya duniani akiwa kama machine.
TERMINATOR TATU IKAISHA
Terminator Genisys. Skynet hawakuridhika, na walichelewa sababu sasa hivi john ni mkubwa na yeye ana uwezo hata wa kumfanya anachotaka robot yoyote duniani..anaongoza kitengo cha binadamu kwa ajili ya kuipinga skynet.
Kuhakikisha mama yake anakuwa salama,anamleta machine kutoka mwaka 1984 mpaka 2015 kumlinda mama yake kutokana na ma terminator.
Katika hali isiyo ya kawaida John anakuja kugundua kuwa mama yake ni skilled fighter, mtu mwenye ufundi mkubwa wa kupambana,hasa na vitu kama machine, na anachogundua mara ya pili ni kuwa pembeni ya mama yake kuna the guardian, machine for killing.
Yess ni Arnorld karudi tena, akiwa kwenye ubora wa mwaka 2015, ni complete machine kuliko zote zilizopita. Hapa ndo ilipigwa vita ya kiume ya miaka yetu sababu skynet nao walituma watu wenye uwezo mkubwa pengine kuliko wote waliopita, battle battle tu
Team John wakashinda tena.
TERMINATOR GENYSIS NNE IKAISHA
Now we are back again..ni tarehe 23 mwezi wa kumi. Sarah Connor na timu yake, na Arnold ndani kwenye mission nyingine nzito. Cant wait. Mwezi uende haraka aisee.
TERMINATOR THE DARK FATE..ON LOADING!
Picha ni mwaka 1991. John alipokuwa mdogo na T-800 yake nyuma.
250 × 369