Moyo wangu unavuja damu

Moyo wangu unavuja damu

Kanashimi I assure you, HIV is No longer an issue to worry to that extent.
Nimehudumia wateja wa HIV for about 8 yrs now.

Ninachokijua akilini mwako umejawa simanzi zito ukiwaza kwamba unaenda kumpoteza mama hivi karibuni. Lakini nakuhakikishia haotokuwa hivyo unavyowaza endapo mama ataanza Clinic haraka na kutumia dawa kwa ufuasi mzuri kabla hajaendelea kuadvance kwenye AIDS.

Kuna ndugu zetu hapo juu wamejitolea kukusaidia katika hili, jaribu kuwapa nafasi na ikitokea unahitaji msaada zaidi nitaku Link na Nurse mmoja ambaye ni Mmama wa 53 yrs ameishi na HIV for over 15 yrs na yuko Healthy kuzidi hata wasio na HIV atamsaidia kwa mambo kadhaa freely na vile ni Mmama mwenzie itafit zaidi.
 
Habari zenu wana Jamii Forum… Natumaini sote tumesherehekea Eid vizuri wale Eid iliyokuwa mbaya kama mimi nawapa pole tupo pamoja Mimi ni member wa muda mrefu ila imebidi nije na ID mpya kutokana na haya yanayonisibu….. \

Ndugu zangu wana jamii forum naombeni mchango wa mawazo hili jambo ni zito nashindwa kulibeba na nimeona nikiandika huku huwenda nitakuwa nimetua mzigo natanguliza shukran.



Pole Sana.

Magonjwa Kama UKIMWI ni ugonjwa ambao unaweza kuishi nao na maisha yakaenda vizuri tu.

unapokuwa unamuuguza mgonjwa haijalishi yupo hatua gani Ila hakikisha unakuwa optimistic -yaani make sure mgonjwa asi-notice sura ya uzuni kwako wewe unayeuguza ,then hakikisha unongea maneno ya USHINDI 24/7 mbele ya mgonjwa.


Mama yako mpatie matibabu ktk haya maeneo.

@ psychological (therapy)
@ Huduma bora za Afya ya mwili
@ spiritual - mfanye awe connected with divine power.

tatizo lolote linaweza kuwa kubwa au Dogo kutokana na vile umelitafsiri.

so hilo sio tatizo .

Jitahidi -ufanye gratitude -penda kumshukuru MUNGU kwa kila jambo linalotokea ktk maisha yako.

Nakuombea na naimani mama atakuwa bora Sana.🙏🏽⭐🌙
 
Dada chukuliwa easy tu.. mtu akiwa positive sio mwisho wa maisha yake mi nimezaa watoto wawili na mwanamke ambaye yuko positive japo tumetengana ila watoto wote wapo negative na mimi pia nipo negai na afya ya huyo bi shosti ipo njema na fresh kabisa... Kuzingatia dawa na vyakula tu atakaa na afya njema na ataishi hadi wajukuu wafike vyuo au waolewe na kuoa
 
Ukiusoma kwa makini uzi wako ni kama mama yako anaijua hali yake, isipokuwa ni ama ameamua kuishi hivyo hivyo bila kutumia ARV...

Ongea na daktari aliyekupa habari za hali ya mama yako, afanye kama anamuita kutaka kujua maendeleo yake, then akiwa huko amchane hali yake ya afya...
 
Ukiusoma kwa makini uzi wako ni kama mama yako anaijua hali yake, isipokuwa ni ama ameamua kuishi hivyo hivyo bila kutumia ARV...

Ongea na daktari aliyekupa habari za hali ya mama yako, afanye kama anamuita kutaka kujua maendeleo yake, then akiwa huko amchane hali yake ya afya...
Unachokisema kinaweza kuwa sahihi niliwaza hivyo pia naona anahisi tutaumia sana esp mimi pengine aliamuua akae zake kimya.
 
Karne ya 21 unaanzaje kuuona ukimwi ni ugonjwa wa ajabu hadi unakaa unalialia.hayo ni mawazo ya miaka ya 90.In short hilo sio tatizo bali wewe ndo unalifanya tatizo kwa kuendekeza hisia uchwara badala ya akili na huko shule ni dhahiri hukwenda kupata elimu bali ulikwenda kusomea kazi. Mgonjwa ukimpeleka hospitali na akafata utaratibu wa kidakitari anaendelea na maisha kama kawaida na mwili wake unarudi.
 
Habari zenu wana Jamii Forum… Natumaini sote tumesherehekea Eid vizuri wale Eid iliyokuwa mbaya kama mimi nawapa pole tupo pamoja Mimi ni member wa muda mrefu ila imebidi nije na ID mpya kutokana na haya yanayonisibu….. Nitajaribu kuelezea kwa ufupi sana kadri nitakavyojaaliwa…

Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 31 ni mtoto wa kwanza kwenye familia ya watoto wa3 wote tukiwa ni wa kike kwa bahati mbaya wazazi wangu walitengana miaka mingi sana iliyopita sisi tukiwa wadogo… Kwa miaka yote hiyo tumekuwa tukilelewa na mama ambaye yeye ndiyo sababu ya mimi kuandika uzi huu

Mama yangu amekuwa akitulea kwa mapenzi makubwa mno na alipambana kuhakikisha sote tumesoma vizuri na kupata mahitaji ya msingi Alhamdulilah.

Baada ya kumaliza degree yangu ya kwanza Mungu alinisaidia nikapata kazi nzuri na nashukuru nimeweza kuisupport familia yangu kwa kipindi chote hiki

Miaka kadhaa nyuma nilianza kuona mabadiliko kwa mamangu na kwa kuwa ni mtu ambaye nampenda sana hata kitu kidogo tu kikiwa hakipo sawa nakuwa wakwanza kugundua tofauti na ndugu zangu.

Mama yangu ni mwanamke mrembo sana ambaye ni mchanganyiko wa Mtanzania na Mgiriki hivyo ni mtu aliyekuwa na muonekano wa kuvutia sana nakumbuka katika miaka yangu yote ya kusoma akiwa anakuja shule marafiki na walimu walikuwa wanabisha kuwa ni mama yangu na wengi walidhani ni dada yangu wa kwanza kutokana na muonekano na namna anavyojipenda.

Tuendelee mama alianza kubadilika na taratibu urembo wake ukaanza kupotea akawa hana raha, afya ikaanza kuyumba na kuna muda inakaa sawa nikawa naongea nae kumuuliza ana shida gani tofauti na Pressure inayomsumbua lakini akawa anadai yupo sawa basi siku zinazidi kwenda… 2021 akawa anashambuliwa na maradhi mara kwa mara anaenda hospital anakuwa poa kusema kweli nilianza kuwa na hofu kubwa juu yake… lakini siku zikawa zinakimbia

Moyoni mwangu kuna sauti ilikuwa inaniambia kuna kitu kikubwa hakipo sawa nilichokuwa nafanya kila nikisali nilikuwa namuomba Mungu amrejeshee furaha mama yangu

To cut a story short mwaka huu mwanzoni mwa mwezi wa tatu nilisafiri kwa majukumu ya kikazi na nikiwa huko wadogo zangu walinipigia wakanambia mama amepata typhoid kali sana na yupo kwenye dawa ila nisiwe na hofu… ila niliporudi Mungu wangu mama yangu alikuwa ameisha nyie nilipomuona sikuweza kuzuia machozi yangu nikawauliza wadogo zangu imekuwaje hii hali wakanambia amekuwa mvivu wa kula.

Ikabidi siku iliyofuata nimpeleke hospital mimi na last born wetu nilivyofika nikaingia kwa doctor na dozi alizopewa za Typhod nikaomba amfanyie mama vipimo vyote ili nijue shida nini… majibu yakatoka doctor akanambia nani anaishi nae nikamwambia ni mimi na ndugu zangu akanihoji maswali kadhaa na mwishowe akaniambia MAMA YAKO NI HIV POSITIVE kwa mujibu wa vipimo. Naomba nikiri sijawahi kusikia maumivu kama niliyosikia ile siku niliona kama dunia imenielemea nyie mama yangu kipenzi changu

Nilisali pale Mungu anipe uvumilivu nisionyeshe mabadiliko yoyote kwa mama na ndugu yangu maana walikuwa nje na Doctor alinishauri nisimwambie yeyote hata ndugu zangu ila nimkazanie ale kisha nitafute hospital ya wilaya aanze CLINIC…. nilipotoka wote wakaniuliza umeambiwaje kwa ujasiri nikajibu ni Typhod inabidi umalize dozi

Nikiri hakuna siku nililia kama ile maana tuliporudi home niliwaaga wadogo zangu nikatoka mara moja nikatafuta mahali nikalia sana ndugu zangu naomba niwaambie nimekata tamaa nawaza nitaanzaje kumwambia mama hali yake moyo wangu umejaa maumivu makali sana.

Niliwashawishi wadogo zangu wasafiri for eid ili mimi nibaki na mgonjwa niongee nae wameondoka tangu jana lakini mpaka ninavyoandika hapa sijaweza kumwambia chochote…. kila nikikaa ni machozi tu yanatoka na ameanza kunotice ananiuliza mbona huna raha.

Ndugu zangu wana jamii forum naombeni mchango wa mawazo hili jambo ni zito nashindwa kulibeba na nimeona nikiandika huku huwenda nitakuwa nimetua mzigo natanguliza shukran.
Pole sana ndugu na pia hongera kwa kupata ujasiri wa kushare,

Kwa hali aliyonayo mama yako haitakiwi kukutoa kwenye mstari ukizingatia sasa hivi kuna dawa akitumia kwa ufasaha (good adeherence) atakuwa vizuri tu ndani ya muda mfupi na hakuna gharama zozote katika clinic zote (CTC) za HIV, na kuna privacy ni yeye tu kumuweka wazi ili ajue hali aanze dawa.

Jitahidi umuambie mapema na ikiwezekana nenda nae kwa counselor kama wewe unawasiwasi ili aweze kumhandle vzuri for pre and post counseling.
 
Pole sana dada.
Allah atawapa nguvu na ujasiri wa kulikabili hili.

Mimi kwa umri ni kaka yako, kwa miaka 5 zaidi. Najitolea, kuwa mfariji wako na unitambulishe kwa mama kama rafiki yako wa muda tu nilikua mkoani nikiishi huko.
Tuongee na mama pole pole na kwa kipawa nilichojaaliwa na Allah tutafanikisha kumueleza mama hali yake. Nna imani ataipokea. Ntakuja na daktari, tutashauri kitu na hali ataipokea mwenyewe. We jifanye hujui kitu.
After all, maisha lazima yaendelee, no matter what. Ni jaribu tu hili. Litapita.
Karibu.
Mmmmmh aiseee...
Takbir....
 
Kanashimi

Sijui ni kwa Nini Daktari alikueleza wewe hizo habari badala ya mama.

Ninavyojua utaratibu mgonjwa ndio anatakiwa kuwa mtu wa kwanza kujua afya yake isipokuwa kama ana hali mbaya sana.
Yeye ndio ataamua kuwajulisha wengine.

Kwa kuwa imeshatokea mimi Nakushauri, usimwambie.
Mchukue mpeleke hospitali, Mueleze Mtoa huduma, amupime then ikithibitika anao yeye ndio amueleze.

DR Mambo Jambo unasemaje.
 
Nika zani cancer kumbe ukimwi..ondoa shaka na mzingatie ushauri wa madaktari ataishi mda mrefu pasipo gharama.
 
mdada nazani hiyo kazi ya kushauri siyo yako ila wewe ni muhudumiaji kulingana na maelekezo ya dokta sasa chakufanya nenda hospitali ongea na mtoa ushauri nasaa/psychologist ambae atakaeweza kumshauria atumie dawa na pili akukutanishe wewe na mama yako ili ajaribu kuweka jambo hilo huwenda mama yako anahofu juu yenu kuwa mkijua hana pa kuweka uso wake ila kama dokta akifanya inshu ya kuwaonganisha wewe na mama yko kwamba mama yako ajue kwamba kuna mwanawe mkubwa anajua siri yake ila anaitunza atakuwa hana hofu na atakuwa katika hali normal.

usimwambie chochote na jikaze.
 
Back
Top Bottom