Mchochezi
JF-Expert Member
- Feb 29, 2012
- 10,962
- 7,830
Kwa miaka 15 iliyopita katika ligi yetu ya VPL nadiriki kusema mpaka sasa sijaona beki wa kati wa kariba ya Victor Costa Nampoka "Nyumba".
Victor Costa alibarikiwa kila kitu ambacho beki wa kisasa anatakiwa kuwa navyo, kuanzia uwezo wa kumsoma adui, ukabaji, utulivu na bila kusahau matumizi makubwa ya akili. Beki pekee ambaye angeweza kuonyesha utulivu wa hali ya juu katika box lake bila kutetereka.
Kitu ambacho sijaona kwa mabeki wetu wa kizazi hiki, ambao wengi wao huwa na papara kubwa wawapo ndani ya 18 yao na huishia kubutua ili kuondoa lawama. Atleast, Pasco Wawa alikaribia kufikia walau robo ya uwezo wa Costa.
Nadiriki kusema kwa miaka 15 iliyopita sijawahi kuona beki wa kati mwenye uwezo mkubwa kama Costa, na laiti kama angepata washauri wazuri walau enzi zake angelikuwa anatamba ulaya maana naamini Victor Costa ni mahiri kuliko Chris Smalling, Per Matesaka, Samuel Umtiti au Kurt Zouma. Bahati mbaya alichezea soka lake lote hapahapa Bongo kutokana na washauri wabovu waliomzunguka.
Tunakukumbuka Victor Costa Nampoka Nyumba!!
Victor Costa alibarikiwa kila kitu ambacho beki wa kisasa anatakiwa kuwa navyo, kuanzia uwezo wa kumsoma adui, ukabaji, utulivu na bila kusahau matumizi makubwa ya akili. Beki pekee ambaye angeweza kuonyesha utulivu wa hali ya juu katika box lake bila kutetereka.
Kitu ambacho sijaona kwa mabeki wetu wa kizazi hiki, ambao wengi wao huwa na papara kubwa wawapo ndani ya 18 yao na huishia kubutua ili kuondoa lawama. Atleast, Pasco Wawa alikaribia kufikia walau robo ya uwezo wa Costa.
Nadiriki kusema kwa miaka 15 iliyopita sijawahi kuona beki wa kati mwenye uwezo mkubwa kama Costa, na laiti kama angepata washauri wazuri walau enzi zake angelikuwa anatamba ulaya maana naamini Victor Costa ni mahiri kuliko Chris Smalling, Per Matesaka, Samuel Umtiti au Kurt Zouma. Bahati mbaya alichezea soka lake lote hapahapa Bongo kutokana na washauri wabovu waliomzunguka.
Tunakukumbuka Victor Costa Nampoka Nyumba!!