Mpaka lini tutavumilia juu ya Vituko vya Marefa wanaochezesha Ligi Mbalimbali Tanzania?

Mpaka lini tutavumilia juu ya Vituko vya Marefa wanaochezesha Ligi Mbalimbali Tanzania?

Sawa,mfano tukio la Morrison kumpiga ngumi Nyoso mechi ya jkt na simba,na penyewe hadi VAR??
Kwa mfano penati waliyopewa Yanga dhidi ya Simba ambapo kosa lilifanyika nje ya box,au penati waliyopewa Yanga dhidi ya KMC wachezaji wamegongana lakini Yanga wakazawadiwa penati. Kwa ujumla wake marefa wetu wako chini kabisa ya kiwango ndiyo maana malalamiko hayaishi.
 
Ukiwalaumu waamuzi peke unakosea.Kifupi sisi watanzania "tumeoza"wengi.
Kuna maeneo mengi mambo hayako sawa.TRA ,Polisi,Bunge,Ikulu,Halmashauri,Mashuleni,Vyuoni,n.k.ni ubatili tupu.Iweje waamuzi wawe tofauti?

Hiyo ni taswira ya jamii tunayoishi na kuitengeneza. Nitajie taasisi hata 1 tu iliyo "smart".
100%
 
Kwa mfano penati waliyopewa Yanga dhidi ya Simba ambapo kosa lilifanyika nje ya box,au penati waliyopewa Yanga dhidi ya KMC wachezaji wamegongana lakini Yanga wakazawadiwa penati. Kwa ujumla wake marefa wetu wako chini kabisa ya kiwango ndiyo maana malalamiko hayaishi.
wanatuharibia mpira hawa. Kwann hatua kali zisichukukuliwe??
 
Sote tumekuwa Mashuhuda wa matukio mbalimbali katika soka yanayofanywa na marefaree wetu hapa Bongo. Imefika mahala mechi zinaharibika kutokana na utashi mdogo wa watu hawa katika kuchezesha soka. Watu hawa muhimu kabisa katika soka ndo wamekuwa vinara wa kutuharibia soka letu.

Ukianza kuchambua ni matukio mengi sana ya ajabu yanayofanywa na waamuzi wa soka kote nchini. Swali ni je,hawana uelewa na sheria za mchezo huu? Je ni wageni katika mchezo huu?

Kwa uchunguzi wa haraka haraka ,nimekuja kugundua kuwa wengi wao wanamahaba na timu flani flani hapa Bongo,ndio maana wakipewa dhamana ya kuendesha michezo inayoambatana na timu zao wanaambulia kuharibu mechi, kwa mbeleko za mbao.

Je, hiyo ni sababu tosha kwako mpenda soka? Je, Unahisi nini chanzo cha uhaini huu katika soka letu?

Nini mchango wako (Tuchukue hatua gani kwa vilaza hawa).

#jr
Jana Mikia wamepewa penalty ya bure. Over.
 
Ukiwalaumu waamuzi peke unakosea.Kifupi sisi watanzania "tumeoza"wengi.
Kuna maeneo mengi mambo hayako sawa.TRA ,Polisi,Bunge,Ikulu,Halmashauri,Mashuleni,Vyuoni,n.k.ni ubatili tupu.Iweje waamuzi wawe tofauti?

Hiyo ni taswira ya jamii tunayoishi na kuitengeneza. Nitajie taasisi hata 1 tu iliyo "smart".
uko sahihi wote tunakosea lakini sasa nani atamvisha paka kengere,kwamfano kwa game kama ya jana simba wangesema hapana ile sio penalty na mpijaji wa penalty kagere angetoa njee tayari ingejenga aina Fulani kichwani kuwa tusioneane kwa maamuzi mabovu ya marefa
 
uko sahihi wote tunakosea lakini sasa nani atamvisha paka kengere,kwamfano kwa game kama ya jana simba wangesema hapana ile sio penalty na mpijaji wa penalty kagere angetoa njee tayari ingejenga aina Fulani kichwani kuwa tusioneane kwa maamuzi mabovu ya marefa
Ulishaona wapi hiyo? Timu inatafuta ushindi,fursa imejitokeza ,hata wewe utaiachia?
NB.Hata kwa wenzetu tunaodhani wako mbele yapo.VAR inawafanya "kitu" mbaya wengi lakini hatusikii malalamiko kama haya bali wanajitahidi kuboresha na si kutaka kukazia waamuzi. Ili tusonge mbele nadhani tuanzishe matumizi ya VAR au kuwe na jopo la kupitia matukio yenye utata na uamuzi utolewe hapo hapo!
 
Back
Top Bottom