Mpaka sasa sijaona wa kumfananisha na Mzee Dossa Aziz Ally Tanzania hii

S Sema kweli
 
Baba yake alimpeleka madrsa kusoma Quran halafu kuna Mijitu inataka Mwl Nyerere a mpatie ukuu wa mkoa
Na yeye kusoma Quraan wewe imekukera sana au sio?
Ungesikia kasoma Ufunuo na galatia ungeskia raaaha.
Makafiri mna laana ya Mungu. Mnaugua maradhi mabaya kwa roho zenu mbaya.
Haya Corona hio . Nyie si mmesoma? Tuleteeni Tiiba basi sisi watu wa madrasa tunasubiri.
Laanatullahi wahedi.

.
 

Laana ipo kwa wasiolijua neno
 
Nguruvi3,
Hata wale ambao wananichukia kwa ajili ya hasad hawajapata kusema kuwa Mohamed Said anaandika ''ngano'' mfano labda wa Irving Wallace au James Clavell.

Naweza nikakuwekea hapa vitabu nilivyoandika pamoja na papers kisha nikakupa changamoto uoneshe ''ngano,'' nina hakika hutaweza la kama unabisha sema ''su,'' nikuwekee.

Naamini unataarifa kuwa kitabu cha Wasifu wa Julius Nyerere kimetoka siku chache zilizopita.
Soma hapo chini ujumbe nilioandikiwa na waaandishi wake:

''Ndugu Mohamed,
Salaam kutoka Dar es Salaam. Tunatumai uko mzima. Tuna furaha kukujulisha kuwa kile kitabu cha wasifu wa Mwalimu Nyerere tulokuwa tunakiandika sasa kimeshachapishwa. Ndugu Mohamed, ulitoa mchango muhimu kwenye mchakato wa utafiti, na hivyo tuna furaha kubwa kukutunukia nakala ya kitabu. Ikiwa utapenda kukifuata kitabu kupitia kijana wako hapo TPH mtaa wa Samora, unaweza kufanya hivyo. La sivyo, tunaomba anuani ya kukutumia nakala yako. Tunatoa shukrani zetu tena na kukutakia kila la kheri.
Prof Issa Shivji
Prof Saida Yahya-Othman
Dr Ng’wanza Kamata''

Bwana Nguruvi3,
Bado unaamini naandika ''ngano?"?

Kuhusu historia ya TANU sina sababu ya kubishana na mtu yeyote kwani mimi nimeandika historia ya wazee wangu jinsi walivyounda chama cha TANU wewe kinakukasirisha nini?

Vipi utataka kuniingiza katika ubishi usio na tija wa Nyerere aliishi kwa Abdul au aliishi nyumbani kwa Ally?
Hivi kweli Abdul Sykes kadi yake ya TANU no. 3?

Kweli Denis Phombeah Mnyasa wa Nyasaland kadi yake ya TANU no. 5 na Dome Budohi Mluya kutoka Kenya kadi yake ya TANU ni no. 6?
Sasa ilikuwaje hawa wakawa wanachama wa TANU na wengine kuwa viongozi?

Kweli Chief Kidaha Abdul ndiye alimtaka awe Rais wa TAA kisha waunde TANU.

Hivi kweli African Association iliasisiwa na baba yake Abdul Sykes?
Hivi ni kweli Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa anauza kadi za TANU misikitini wakati anadarsisha?

Waliotaka kujua historia ya wazee wangu wamesoma kitabu na wakaja nyumbani kwangu kwa heshima na ustaarabu wote kuja kunihoji kuhusu uhusiano wa Julius Nyerere na wazee wangu.

Kama wewe una historia nyingine andika tusome.

Hawa waliaondika wasifu wa Nyerere waliona athari ya kuiacha historia yangu ibaki peke yake haina jibu nami nimemtaja sana Mwalimu katika kitabu cha Abdul Sykes.

Angalia picha ya mimi kwa heshima ya hawa walimu wangu walionisomesha mimi nimekaa chini ya miguu yao.
Waliponiuliza kwa nini nakaa chini nikawaambia hii ndiyo adabu ya ilm.

Ndugu yangu unakuja hapa na kejeli na lugha za maudhi...
Mimi si mtu wa hayo tafuta mfano wako mshambuliane kifu yenu.
 

Attachments

  • PROF. SHIVJI, PROF. SAIDA NA DR. KAMATHA.JPG
    12.6 KB · Views: 8
  • PROF. ISSA SHVJI NA PROF. SAIDA YAHYA-OTHMAN.jpeg
    34.5 KB · Views: 8
  • WASIFU WA JULIUS NYERERE.jpg
    6.4 KB · Views: 8
Mohamed Said
Heee! sheikh imekuwaje tena na swaumu hii, mbona umetufikia kwa taharuki, hamaki na jazba?
Katika uzi huu sijataja neno 'ngano'' iweje unilishe maneno yako!

Hata hivyo huhitaji vitabu na paper, kuamini Nyerere alikuja Dar mwaka 1952 kwa mara ya kwanza si ngano?

Kuamini mwenyekiti wa TAA Bw Abdul hakumjua katibu wa tawi la Tabora Mh Nyerere si ngano hiyo?

MS, mbona tupo jamvini muongo mmoja tukionyesha mchele, chuya na Mashudu seuse ngano!

MS au ulitaka mahala pa kueleza umeletewa nakala ya kitabu cha Mwl Nyerere, eleza tu usinitumbukize huko

Badala ya kunishambulia mjibu mleta mada, kwamba, mikutano ilifanyika barazani kwa Dossa na si kwa mwana wa Bi Mluguru, Bw Abdulwahidi Kleist Sykes Mbuwane(mamluki).

Maslaam

Mag3
 
Nguruvi3,
Unapenda shari na naona unajisikia raha kutafuta kushambuliana.

Kwanza mimi si sheikh kama wewe ulivyokuwa si mchungaji.

Mimi ni sawasawa na mtu yeyote yule.

Wala hakuna taharuki wala hamaki.

Mimi natafakhari kuwa wazee wangu wana historia na katika historia hii yao ya TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika ndipo wanapokutana na Nyerere.

Vinginevyo labda ungesoma kitabu changu na ungekisahau kama kitabu kingine chochote kwani sijakusoma ukiishambulia historia ya Chuo Cha CCM Kivukoni.

Haikukukera kwa kuwa ndani yake hukumkuta Abdul Sykes na historia yake ya kuwa ndiye aliyempokea Mwalimu Dar es Salaam.

Haikukera kwa kuwa hukumsoma Sheikh Suleiman Takadir wala Iddi Faiz Mafungo wala Bi. Tatu bint Mzee.

Wewe na wengine wengi mfano wako wazalendo hawa hamkuwajua na kamwe msingewajua majina yao wala nafasi zao katika maisha ya Nyerere kama nisingenyanyua kalamu kuandika.

Umeghadhibika kwa nini Waswahili hawa wameunganishwa na Nyerere?

Labda umefunzwa kudharau watu na ulipotambua kuwa umedanganywa ndipo ulipojenga chuki.

Lakini nimewaeleza hawa wazee wangu kama inavyostahili kuelezwa na heshima yao leo imerejea.

Ulitaka historia hii ipotee ibaki historia ya Nyerere peke yake?

Ndiyo maana katika kuandika historia ya Julius Nyerere nikawekwa katika orodha ya watu wanaomjua Nyerere lau kama mimi na yeye hatukupata kukutana hata siku moja.

Mimi nijifarague kwa kitabu cha Nyerere?

Nimemtafiti Nyerere na kuandika historia yake na kitabu chake kuchapwa Uingereza zaidi ya miaka 20 iliyopita na sababu ya kitabu kuchapwa nje ni kuwa publishers wote nchini pamoja na Oxford University Press Nairobi walikiogopa kitabu changu.

Kipi kiliwatia hofu?

Hiki kinachokughadhibisha wewe ndicho kilichowatisha.

Lakini baada ya kitabu kutoka Oxford Nairobi (2007)na Oxford New York (2011)na wachapaji wengine wamechapa kazi zangu na cha kustaajabisha zote Nyerere nimetaja kwa sifa zake anazostahili.

Kama kujifaragua ningejifaragua na hawa si kwa kupewa kitabu kitabu cha Nyerere.

Ningejifaragua kwa kumzungumza Abdul Sykes Northwestern University, Evanston, Illinois, Ukumbi wa Eduardo Mondlane.

Nahitimisha kwa kukufahamisha kuwa nimeombwa nifanye "book review," ya kitabu cha Mwalimu.







Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kafanya yote Mazuri kwa ajiliya Nchi lkn Leo kasahaulika kabsaa anakumbukwa Piere au Kingwendu..
Mungu amrehem Mzee Dossa Aziz..
Mungu awalipe ubaya wale wote walozulumu haki yake huyu Mzee

Sent using Jamii Forums mobile app
Wakati mwingine watu kawa hawa wanasahaulika kwa sababu ya kutokuwepo na kumbukumbu zozote zinazo wahusu. wengi tunaujua mtaa wa Dosa pale Magomeni lakini hatukua tunajua mwenye jina alikuwa ni nani. Tujifunze kuweka kumbukumbu za mambo/watu mbalimbali kwa ajili ya vizazi vijavyo
 
Kitumaki,
Huu ni Mtaa wa Dosi siyo Dossa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"Mohamed Said, post: 35310156, member: 12431"]
Nguruvi3,Unapenda shari na naona unajisikia raha kutafuta kushambuliana.
Mzee Said, Hakikha katika kaumu ya waungwana sikosi kiti. Chembelecho punguza jazba mwezi 15 tunashuka
Kwanza mimi si sheikh kama wewe ulivyokuwa si mchungaji.
Kuna mtu alinigutia sheikh si msalishaji, ni neno la kiarabu la 'mzee''. Kama unaukana uzee hair inshallah, wakati ukifika ni majaaliwa tu
Mimi ni sawasawa na mtu yeyote yule.
Wewe ni sawa na mimi na sijui uchungaji unanipa kutoka wapi Yarabi.
Vinginevyo labda ungesoma kitabu changu na ungekisahau kama kitabu kingine chochote kwani sijakusoma ukiishambulia historia ya Chuo Cha CCM Kivukoni.
Kuna sababu sishambulii kitabu cha Kivukoni.
Nilishakisoma mara moja na sitakirudia tena, sasa upige Bomu mochuari halafu utambe umeua
Haikukera kwa kuwa hukumsoma Sheikh Suleiman Takadir wala Iddi Faiz Mafungo wala Bi. Tatu bint Mzee.
Bi Mluguru pia. Inikere nini wewe kutaja wazee wako!
Umeghadhibika kwa nini Waswahili hawa wameunganishwa na Nyerere?
Lahaula! mimi mwenyewe Mswahili, leo uswahili unikere! Hakika akutukane hakuchagulii tusi.
Nanynyua nyuso kukuombea kwa maulana akujaze palipopungua, na palipojaa ajazie pomoni! akusamehe unapoghafilika, kaupe subra penye hamaki na upendo kwa Nyerere
Labda umefunzwa kudharau watu na ulipotambua kuwa umedanganywa ndipo ulipojenga chuki.
Hii wanaita inferiority complex, yaani mtu anahisi kuchukiwa bila kuwepo chuki.
Lakini nimewaeleza hawa wazee wangu kama inavyostahili kuelezwa na heshima yao leo imerejea.
Waliowavunjia heshima ni Wazee wako wa Dar es salaam,

Yusuph Makamba ana alama Dar lakini ya Idd Faiz Mafungo hatuioni, ya Bi mluguru hatuioni, Bi Selengia, au Mnonji, na hata basi mamluki Mbuwane aliyetuletea ''uzao maalumu'' kama unavyoamini hatuoni.

Hawa wazee wako walikuwa madiwani na mameya miaka mingi tu baada ya uhuru ndio walianza kukosa adabu sisi wengine tunafuata tu.Sikumoja natamani nikusikie ukiwasota madole ya macho, ukimaliza ndipo urejee kwetu!
Mimi nijifarague kwa kitabu cha Nyerere?
Huyu bwana humpendi weweee!

Yaani ukimsikia Nyerere roho inapaa.Hata hivyo ukweli unabaki pale pale ndiye aliyepokea uhuru si Abdul Sykes! Ni ukweli si mimi wala adabu zangu.
Hiki kinachokughadhibisha wewe ndicho kilichowatisha.
Yaani nilisoma vitabu vyote, kiingereza na kiswahili , matoleo yote magazetini, sijawahi kughadhabika.

Kinachotia ghadhabu si kitabu ni maudhui, unaponyunyuzia hamira, ukaumua tukabaki na shudu na ngano.
Hili linatia ghadhabu sana. Halafu hutaki kubadilika hata ukiambiwa 1 na 1 ni 2.

Nyerere hakufika Dar mwaka 1952 wala hakuingizwa siasa na Abdul na kwamba Abdul alimjua akiwa Tabora na walikutana mkutano mkuu Dar es salaa.Sasa tunasikia katika uzi huu kuwa vikao viilikuwa kwa Dossa si kwa mwana wa Bi Mluguru , karani wa soko Abdul.
Lakini baada ya kitabu kutoka Oxford Nairobi (2007)na Oxford New York (2011)na wachapaji wengine wamechapa kazi zangu na cha kustaajabisha zote Nyerere nimetaja kwa sifa zake anazostahili.
Tafadhali bwana, wewe umuheshimu Nyerere mvaa Kaptula!

MS umeheshimu Nyerere! real? Unavyomchukia mzee wa watu!
Yaani wewe unayekaa kimya watu wakisema Nyerere laanatullah leo unampenda !
Mzee Said, una swaumu kumbuka. Lahaula kapate Iftar kama si daku kisha funda la maji!
 
Nguruvi3,
Launcelot Gobbo...
Soliloquy!

Umenichekesha kidogo.
Ahsante sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…