Mpangaji aliyeishi Chumba cha giza kwa miaka Nane ili kufanikisha malengo yake

Mpangaji aliyeishi Chumba cha giza kwa miaka Nane ili kufanikisha malengo yake

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Screenshot_20250113_143836_Google.jpg


Hii ni true story ya mpangaji wa bibi yangu pale ilala kota,naandika uzi huu kama hamasa kwa wapambanaji wote kwamba ukiweka malengo na kuishi nayo hakika utafika pale unapotaka kufika

Mpangaji huyu na mume wake walikuwa ni miongoni mwa wapangaji kadhaa pale kwa bibi yangu,pamoja na kwamba nyumba ya bibi ilikuwa na umeme,lakini baadhi ya vyumba vilivyo ongezwa havikuwa na umeme

Hivyo ilikuwa ni jukumu la mpangaji mpya kujionganishia yeye umeme kutoka katika vyumba vingine,lakini miongoni wa wapangaji wengi ambao wote wana umeme,ni mama huyu na mume wake pekee hawakutaka kuonganisha umeme,lakini nyuma ya pazia waliwakuwa na malengo yao

Ni kawaida sana kuamka saa kumi usiku kumkuta bibi huyu akichoma maandazi,na hiyo ilikuwa ni daily au kila siku,lakini nyuma ya mapambano haya wanafamilia hawa walikuwa na malengo mazito sana ya kuwa na mji wao

Screenshot_20250113_155138_Google.jpg


Hatimaye baada ya miaka nane ya upangaji walihamia katika nyumba yao wenyewe,hapa ndio ikajulikana ile siri ya kujinyima kujionganishia umeme,kwao wao hela hiyo ilikuwa na thamani kubwa sana,kikubwa ilikuwa kufikia malengo yao

Sikwambii wewe ukae chumba cha giza laa,nakwambia kwa kila malengo unayotaka kufikia basi lazima ujitoe sadaka kwa baadhi ya mambo fulani katika maisha ili ufikie pale unapopataka,huna budi kujinyima baadhi ya mambo ili ufikie katika lengo husika

Kuna mtu mmoja alikuwa anapenda kula ovyo ovyo,nadhani tunawajua watu ambao akikuta sambusa lete,keki lete,karanga lete na kadhalika,basi kuna bwana mmoja baada ya kutambua udhaifu wake wa kula kula akaona hivi hawezi akabadilisha hii tabia na kuzalisha kitu kikubwa zaidi

Badala ya kula kula ovyo alihifadhi hela zake na kujenga msikiti mkubwa unaitwa NIMESHAKULA,kwa maana kila alipopata hamu ya kununua hiki ama kile alijiambia nimeshakula

Mwisho wa siku alifikia malengo,hata sisi tunaweza kufikia malengo yetu kwa kujikagua na baadhi ya mambo ambayo hayana umuhimu na mwisho wake tukayaepuka na kutumia hizo fedha kufikia malengo fulani maishani

Anza sasa na sio baadae

Ni hayo tu!
 
View attachment 3200775

Hii ni true story ya mpangaji wa bibi yangu pale ilala kota,naandika uzi huu kama hamasa kwa wapambanaji wote kwamba ukiweka malengo na kuishi nayo hakika utafika pale unapotaka kufika

Mpangaji huyu na mume wake walikuwa ni miongoni mwa wapangaji kadhaa pale kwa bibi yangu,pamoja na kwamba nyumba ya bibi ilikuwa na umeme,lakini baadhi ya vyumba vilivyo ongezwa havikuwa na umeme

Hivyo ilikuwa ni jukumu la mpangaji mpya kujionganishia yeye umeme kutoka katika vyumba vingine,lakini miongoni wa wapangaji wengi ambao wote wana umeme,ni mama huyu na mume wake pekee hawakutaka kuonganisha umeme,lakini nyuma ya pazia waliwakuwa na malengo yao

Ni kawaida sana kuamka saa kumi usiku kumkuta bibi huyu akichoma maandazi,na hiyo ilikuwa ni daily au kila siku,lakini nyuma ya mapambano haya wanafamilia hawa walikuwa na malengo mazito sana ya kuwa na mji wao

Hatimaye baada ya miaka nane ya upangaji walihamia katika nyumba yao wenyewe,hapa ndio ikajulikana ile siri ya kujinyima kujionganishia umeme,kwao wao hela hiyo ilikuwa na thamani kubwa sana,kikubwa ilikuwa kufikia malengo yao

Sikwambii wewe ukae chumba cha giza laa,nakwambia kwa kila malengo unayotaka kufikia basi lazima ujitoe sadaka kwa baadhi ya mambo fulani katika maisha ili ufikie pale unapopataka,huna budi kujinyima baadhi ya mambo ili ufikie katika lengo husika

Kuna mtu mmoja alikuwa anapenda kula ovyo ovyo,nadhani tunawajua watu ambao akikuta sambusa lete,keki lete,karanga lete na kadhalika,basi kuna bwana mmoja baada ya kutambua udhaifu wake wa kula kula akaona hivi hawezi akabadilisha hii tabia na kuzalisha kitu kikubwa zaidi

Badala ya kula kula ovyo alihifadhi hela zake na kujenga msikiti mkubwa unaitwa NIMESHAKULA,kwa maana kila alipopata hamu ya kununua hiki ama kile alijiambia nimeshakula

Mwisho wa siku alifikia malengo,hata sisi tunaweza kufikia malengo yetu kwa kujikagua na baadhi ya mambo ambayo hayana umuhimu na mwisho wake tukayaepuka na kutumia hizo fedha kufikia malengo fulani maishani

Anza sasa na sio baadae

Ni hayo tu!
Huyo wa msikiti nimemuonea huruma sana!alijitesa bure kabisa!

Wanaswali Kwa ajili ya kesho akhera na akhera ni kuzimu !hasara kubwa sana!
 
Kuna kipato mtu anapata hawezi weka malengo yoyote kinaisha chote huyu mnamsaidiaje?
Ni sahihi kabisa unavyosema,mtu kama hana budi kuongeza njia nyingine ya kuongeza kipato ili walau mambo yaende sawa

Lakini doktori Janabi anasema hivi hakuna anayeamka asubuhi na njaa,hivyo tunakunywa chai kwa mazoea tu,acha breakfast kwa kipindi flani uweke akiba,kama unatumia breakfast 2000 asubuhi,ukiacha chai ambayo sio ya lazima mwisho wa mwezi una 60,000 je miezi mitatu hujapata kamtaji ka kufanya chochot?

Naamini kabisa kwa kila kitu kuna njia
 
Huyo wa msikiti nimemuonea huruma sana!alijitesa bure kabisa!

Wanaswali Kwa ajili ya kesho akhera na akhera ni kuzimu !hasara kubwa sana!
Hakujikutesa hakuacha kula kabisa ila aliacha kula kula hovyo
Nadhan kama ni kuzimu au laa itajulikana siku ya mwisho
 
Kuna kipato mtu anapata hawezi weka malengo yoyote kinaisha chote huyu mnamsaidiaje?
Umeongea ukweli kabisa , vyovyote vile maisha lazima yaendelee uhai ujiwepo, na uhai unapatikana kwa kula .
Sasa mtu unajaliwa uwezo wa kula leo tu kesho majaliwa ya Mungu, bado mahitaji muhimu kabisa katika maisha huwezi kuyakwepa.

Utahisi ni kusema ili iwe kawaida inahitajika 2,000
Lakini kupata kwako ni 1,000 au 800 , hapo unaona kila siku inapo kucha una deni la jana!

Vipi utaweka akiba, vipi utajinyima nk nk ili kufikia malengo?
 
View attachment 3200775

Hii ni true story ya mpangaji wa bibi yangu pale ilala kota,naandika uzi huu kama hamasa kwa wapambanaji wote kwamba ukiweka malengo na kuishi nayo hakika utafika pale unapotaka kufika

Mpangaji huyu na mume wake walikuwa ni miongoni mwa wapangaji kadhaa pale kwa bibi yangu,pamoja na kwamba nyumba ya bibi ilikuwa na umeme,lakini baadhi ya vyumba vilivyo ongezwa havikuwa na umeme

Hivyo ilikuwa ni jukumu la mpangaji mpya kujionganishia yeye umeme kutoka katika vyumba vingine,lakini miongoni wa wapangaji wengi ambao wote wana umeme,ni mama huyu na mume wake pekee hawakutaka kuonganisha umeme,lakini nyuma ya pazia waliwakuwa na malengo yao

Ni kawaida sana kuamka saa kumi usiku kumkuta bibi huyu akichoma maandazi,na hiyo ilikuwa ni daily au kila siku,lakini nyuma ya mapambano haya wanafamilia hawa walikuwa na malengo mazito sana ya kuwa na mji wao

Hatimaye baada ya miaka nane ya upangaji walihamia katika nyumba yao wenyewe,hapa ndio ikajulikana ile siri ya kujinyima kujionganishia umeme,kwao wao hela hiyo ilikuwa na thamani kubwa sana,kikubwa ilikuwa kufikia malengo yao

Sikwambii wewe ukae chumba cha giza laa,nakwambia kwa kila malengo unayotaka kufikia basi lazima ujitoe sadaka kwa baadhi ya mambo fulani katika maisha ili ufikie pale unapopataka,huna budi kujinyima baadhi ya mambo ili ufikie katika lengo husika

Kuna mtu mmoja alikuwa anapenda kula ovyo ovyo,nadhani tunawajua watu ambao akikuta sambusa lete,keki lete,karanga lete na kadhalika,basi kuna bwana mmoja baada ya kutambua udhaifu wake wa kula kula akaona hivi hawezi akabadilisha hii tabia na kuzalisha kitu kikubwa zaidi

Badala ya kula kula ovyo alihifadhi hela zake na kujenga msikiti mkubwa unaitwa NIMESHAKULA,kwa maana kila alipopata hamu ya kununua hiki ama kile alijiambia nimeshakula

Mwisho wa siku alifikia malengo,hata sisi tunaweza kufikia malengo yetu kwa kujikagua na baadhi ya mambo ambayo hayana umuhimu na mwisho wake tukayaepuka na kutumia hizo fedha kufikia malengo fulani maishani

Anza sasa na sio baadae

Ni hayo tu!
Malengo mengine yanachukua muda mrefu. Miaka nane na mbu plus joto la Dar bila nishati ya umeme kisa kusave hela ya ujenzi, hapana. Maisha ni pamoja na hiyo miaka nane. Heri wangekaa miaka miwili zaidi (jumla kumi) ambayo ingetumika kama gharama za umeme, kuliko kukaa miaka nane bila umeme. Wamejinyima raha, na walijitengenezea karaha
 
Safi sana mpangaji najua hata watoto wake wote aliwatoa EMs akawarudisha Kayumba saafi sana
 
Back
Top Bottom