Mpangaji aliyeishi Chumba cha giza kwa miaka Nane ili kufanikisha malengo yake

Mpangaji aliyeishi Chumba cha giza kwa miaka Nane ili kufanikisha malengo yake

Daah mimi kuishi Giza ili nihamie kwangu hapana...kuna kufa halafu uliwoacha wanauza tu...let me enjoy the moment..
Hii kauli inafanya watu wengi wasipambane eti unakufa unaviacha.

hao wanaopambana daily hawatakufa?

Wanafanya maendeleo yao kila siku hawatakufa??
 
Lakini alitumia Mwanga unaoliolipiwa na wenzake kupika maandazi yake usiku na kwenda chooni. Unyonyaji si lazima umchome mtu sindano na kuvuta damu, tabia na matendo yako yanaweza akisi Kwa kuwa kinzani na wenzako lakini unaendelea kuji enjoy Kwa manufaa ya jasho la wenzako Hata kama ni kidogo.

Huyu unaweza Kuta anakuja kwako anamshika remote kuangalia mchezo.
 
Ni sahihi kabisa unavyosema,mtu kama hana budi kuongeza njia nyingine ya kuongeza kipato ili walau mambo yaende sawa

Lakini doktori Janabi anasema hivi hakuna anayeamka asubuhi na njaa,hivyo tunakunywa chai kwa mazoea tu,acha breakfast kwa kipindi flani uweke akiba,kama unatumia breakfast 2000 asubuhi,ukiacha chai ambayo sio ya lazima mwisho wa mwezi una 60,000 je miezi mitatu hujapata kamtaji ka kufanya chochot?

Naamini kabisa kwa kila kitu kuna njia
Hii ni slowlane way ambayo hadi ufike unapopataka utachukua muda sana... Suluhisho hapo ni kutafuta njia ya kumuongezea kipato tu.
 
View attachment 3200775

Hii ni true story ya mpangaji wa bibi yangu pale ilala kota,naandika uzi huu kama hamasa kwa wapambanaji wote kwamba ukiweka malengo na kuishi nayo hakika utafika pale unapotaka kufika

Mpangaji huyu na mume wake walikuwa ni miongoni mwa wapangaji kadhaa pale kwa bibi yangu,pamoja na kwamba nyumba ya bibi ilikuwa na umeme,lakini baadhi ya vyumba vilivyo ongezwa havikuwa na umeme

Hivyo ilikuwa ni jukumu la mpangaji mpya kujionganishia yeye umeme kutoka katika vyumba vingine,lakini miongoni wa wapangaji wengi ambao wote wana umeme,ni mama huyu na mume wake pekee hawakutaka kuonganisha umeme,lakini nyuma ya pazia waliwakuwa na malengo yao

Ni kawaida sana kuamka saa kumi usiku kumkuta bibi huyu akichoma maandazi,na hiyo ilikuwa ni daily au kila siku,lakini nyuma ya mapambano haya wanafamilia hawa walikuwa na malengo mazito sana ya kuwa na mji wao

View attachment 3200848

Hatimaye baada ya miaka nane ya upangaji walihamia katika nyumba yao wenyewe,hapa ndio ikajulikana ile siri ya kujinyima kujionganishia umeme,kwao wao hela hiyo ilikuwa na thamani kubwa sana,kikubwa ilikuwa kufikia malengo yao

Sikwambii wewe ukae chumba cha giza laa,nakwambia kwa kila malengo unayotaka kufikia basi lazima ujitoe sadaka kwa baadhi ya mambo fulani katika maisha ili ufikie pale unapopataka,huna budi kujinyima baadhi ya mambo ili ufikie katika lengo husika

Kuna mtu mmoja alikuwa anapenda kula ovyo ovyo,nadhani tunawajua watu ambao akikuta sambusa lete,keki lete,karanga lete na kadhalika,basi kuna bwana mmoja baada ya kutambua udhaifu wake wa kula kula akaona hivi hawezi akabadilisha hii tabia na kuzalisha kitu kikubwa zaidi

Badala ya kula kula ovyo alihifadhi hela zake na kujenga msikiti mkubwa unaitwa NIMESHAKULA,kwa maana kila alipopata hamu ya kununua hiki ama kile alijiambia nimeshakula

Mwisho wa siku alifikia malengo,hata sisi tunaweza kufikia malengo yetu kwa kujikagua na baadhi ya mambo ambayo hayana umuhimu na mwisho wake tukayaepuka na kutumia hizo fedha kufikia malengo fulani maishani

Anza sasa na sio baadae

Ni hayo tu!
Kuishi bila umeme ni gharama zaidi kuliko mwenye umeme.

miaka 8 unanunua mishumaa ama unakuwa na kibatari au tochi? biga gharama na za kuchaji simu mbili

piga gharama ya bulb 2 chumbani na sebereni basi luku ya buku kwa mwezi ama buku mbili inatosha kabisa kwa matumizi yao ukiunganisha na wiring hapo haizidi 100k kwenye chumba chake kama alikuwa na single room ni bulb moja tu buku ni mwezi na ushee.
 
Kuishi bila umeme ni gharama zaidi kuliko mwenye umeme.

miaka 8 unanunua mishumaa ama unakuwa na kibatari au tochi? biga gharama na za kuchaji simu mbili

piga gharama ya bulb 2 chumbani na sebereni basi luku ya buku kwa mwezi ama buku mbili inatosha kabisa kwa matumizi yao ukiunganisha na wiring hapo haizidi 100k kwenye chumba chake kama alikuwa na single room ni bulb moja tu buku ni mwezi na ushee.
Unachosema kuhusu wiring ni sahihi lkn nadhan walikwepa ile donation ambayo huwaumiza baadhi ya watu katika nyumba za kupanga

Wewe unawasha taa tu ukirudi geto lakini wenzio wana pasi,sijui brenda,friji na mambo kama hayo

Lau wangekuwa na luku yao walau ingekuwa poa,na wakati ule kulikuwa hakuna vile vimita kama ambavyo tunavyo siku hizi ambapo kila mtu analipa kutokana na matumizi yake
 
Kuna kipato mtu anapata hawezi weka malengo yoyote kinaisha chote huyu mnamsaidiaje?
Huyu mtu hakuwa na malengo kabla ya kupata hela...

Aweke malengo yanayomvutia/anachopenda kabla, hela ikifika ni utekelezaji.

Aache tabia ya kuwa na hela mkononi ndo anatafuta malengo, ITAISHA KAMA UPEPO
 
Hii ni slowlane way ambayo hadi ufike unapopataka utachukua muda sana... Suluhisho hapo ni kutafuta njia ya kumuongezea kipato tu.
Ni sahihi ishu inakuja utapataje kipato cha ziada,ndio hapo pa kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili upate mtaji

Njia nyingine unaweza kwenda na lunch box yako kibaruani kwako,watu kama hawa wapo ila huwa tunawaona ni wabahili sana,hivi karibuni nilibahatika kukaa na wabena fulani hivi,wakaniambia hawa jamaa kabila la Vunja bei ni kawaida kwao kwenda na lunch box katika shughuli zao (wakinga) na wana hela chafu

Kuna wakinga fukani nilishawahi kuishi nao utotoni ni family friend,hawa ugali unakaa hata siku tatu katika friji na unalika
 
Unachosema kuhusu wiring ni sahihi lkn nadhan walikwepa ile donation ambayo huwaumiza baadhi ya watu katika nyumba za kupanga

Wewe unawasha taa tu ukirudi geto lakini wenzio wana pasi,sijui brenda,friji na mambo kama hayo

Lau wangekuwa na luku yao walau ingekuwa poa,na wakati ule kulikuwa hakuna vile vimita kama ambavyo tunavyo siku hizi ambapo kila mtu analipa kutokana na matumizi yake
Yawezekana hata mimi niliwahi wagomea bulb moja tu wanadai 5000 kwa mwezi nikawaambia wanaumwa
 
Inategemeana una mke wa dizaini gani
Wewe ni mtu wa pili unasema hili expert,je hatuwezi kuwaingiza katika mfumo wetu kwa kipindi fulani ili mambo yaende sawa

Kuna baba wa familia moja wakati anataka kumaliza nyumba yake,aliwaambia familia yake pamoja na watoto kwamba,sasa hivi tutajibana kidogo hatuta kula vizur kwa wakati fulani ili tumalize nyumba yetu,na ikawa hivyo
 
Wewe ni mtu wa pili unasema hili expert,je hatuwezi kuwaingiza katika mfumo wetu kwa kipindi fulani ili mambo yaende sawa

Kuna baba wa familia moja wakati anataka kumaliza nyumba yake,aliwaambia familia yake pamoja na watoto kwamba,sasa hivi tutajibana kidogo hatuta kula vizur kwa wakati fulani ili tumalize nyumba yetu,na ikawa hivyo
Wanawake wengine hata kama una pesa we mdanganye umezikopwa na mtu ili apunguze matumizi ya rough
 
Back
Top Bottom