Tetesi: Mpango mchafu wa Mange Kimambi na Freeman Mbowe wavuja

Tetesi: Mpango mchafu wa Mange Kimambi na Freeman Mbowe wavuja

FISIEM zimeiba 1.5 trillion
IMG_20180420_181134_107.jpg
 
Huyo aliendika hyo topic hajui Historia ya China.

Ila kwa kifupi aliyeleta maendeleo China na kui'transform kuwa hii China tunayoiona leo sio Mao Zedong bali ni Deng Xiaoping.

Deng Xiaoping anajulikana kama the Father of Modern China ambaye ali'introduce principles of free markets and democracy na kuiwezesha China kufunguka na kukubalika katika mfumo wa kimataifa wa masoko na uchumi.

Mao Zedong alileta vifo, mateso, njaa kwa watu wake katika kipindi alichokiita Cultural Revolution. Sema hii topic ni taboo kuongelewa China. Unaweza kufungwa ama kuuawa kwa kumuongelea vibaya Mao Zedong.

Ila ukweli wachina wengi wanaujua kwamba aliyeleta maendeleo ni Deng Xiaoping na sio Mao Zedong. Ona hii makala ya New York Times

Deng Xiaoping: A Political Wizard Who Put China on the Capitalist Road

It doesn't matter whether a cat is black or white, as long as it catches mice. Deng aliamua kuweka ujamaa pembeni.

Sisi tunataka kurudi kwenye Ujima wa Mao.
 
Yaani umemuona mbowe akiwa na mange kimambi tu, bila hata kusikia wanaongea nini, ukaja kuandika gazeti lote hili

Sasa ungesikia mazungumzo yao si ungeandika vitabu
 
*MPANGO MCHAFU WA MANGE KIMAMBI NA FREEMAN MBOWE WAVUJA!!!!!!!!*

• Wakutana Marekani kujadili mipango ya kuivuruga Tanzania
• Watanzania waishio Marekani watahadharisha.

Na Julius Bernard, Maryland USA.

Imethibitika, Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe ametua nchini Marekani na kufanya kikao cha siri na Mange Kimambi, Mwanadada anayetumia mitandao ya kijamii kuhamsisha maandamano haramu na kuishambulia Serikali ya Tanzania.

Mbowe ametua Marekani kutoka Tanzania, pasi kutolewa taarifa yoyote kwenye vyombo vya habari wala mitandao ya kijamii kama ambavyo viongozi wanasiasa wamekuwa wakifanya hasa ndani ya chama chake cha CHADEMA.

Nimemuona Mbowe akiwa na baadhi ya Watanzania wa hapa Marekani wakijadiliana mambo na baadaye akiwa na Mange Kimambi ambaye amekuwa akiunga mkono harakati za kisiasa za CHADEMA zenye mlengo wa kuichafua Serikali, viongozi wa Tanzania hasa Rais John Magufuli na nchi ya Tanzania.

Kwa sasa Mange anahamasisha maandamano haramu anayoyatangaza kuwa yatafanyika tarehe 26 Aprili, 2018 siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Ninachokiona dhahiri ni njama halifu za kuichafua Tanzania, Mbowe anafanya mbinu zote hizi kuhakikisha nchi haikaliki na hili ni jambo ambalo Watanzania lazima walielewe.

Mange Kimambi anahamisisha maandamano tarehe 26 Aprili, zimebaki siku tatu kufikia tarehe hii na tayari Mbowe amekimbia Tanzania na kuja huku Marekani ili Watanzania watakaothubutu kuandamana wakutane na mkono wa dola wakati yeye akiwa salama salimini.

Hii ina maana kuwa Freeman Mbowe na Mange Kimambi wamechora mpango huu wa kutaka watu waandamane kiharamu, wakumbane na vyombo vya dola, waumizwe ama wapoteze maisha kama alivyosema yeye mwenyewe wafe kama 100 au 200 ilihali yeye na mhamasishaji wa maandamano Mange Kimambi wapo Marekani wanakula bata.

Watanzania waliopo Marekani ambao wamemshuhudia Mbowe akiwa hapa pamoja na Mange Kimambi katika mipango yao ya kuhamasisha maandamano wanaonya juu ya upuuzi huu, na wanasema watasema kila wanachokifanya hapa Marekani.

Na hii ndio imekuwa janja ya wanasiasa wengi kuhamasisha maandamano na kukimbilia mafichoni pale wanapoona mkono wa dola hautawaacha. Wengi wamekuwa wakijificha majumbani kwao au kusikojulikana ndani ya nchi, lakini safari hii Mbowe kaona akimbilie nchi nyingine.

Tulioko Marekani na tunaofuatilia hali ya nyumbani Tanzania tunajua hakuna cha maandamano wala mikusanyiko itakayofanyika kwa kuhamasishwa na Mange Kimambi, na itakuwa ajabu sana kama vyombo vya dola vitavumilia hata kwa dakika moja jaribio lolote la kuwaacha watu waandamane ama kukusanyika visivyo halali.

Nimalizie kwa kuwatakia heri Watanzania wenzangu wote huko Tanzania mnapoelekea katika maadhimisho ya siku ya Muungano Aprili 26, tuendeleeni kujenga nchi, tushikamane na serikali na Rais Magufuli ambaye ameonesha dhamira ya kweli ya kuitoa nchi katika mkwamo wa uchumi na kujenga uchumi imara, wa kujitegemea, wenye heshima na endelevu kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Nchi zote zilizoendelea zilipita katika kipindi hicho na watu kama akina Freeman Mbowe na washirika wake wanaotumiwa na wanyonyaji na mabepari walidhibitiwa kwa nguvu zote na bila kuona haya.

Kasomeni wakati Baba wa Taifa la China Mao Zedong (Mao tse-Tung) aliyeishi kati ya mwaka 1893 na mwaka 1976 alipoamua kuchukua hatua ya kuijenga china, alipata upinzani mkubwa kutoka kwa baadhi ya wanasiasa lakini alikomaa nao na China ikapiga hatua kubwa zilizojenga msingi imara uliopelekea China ya leo.

Kwa heri.
Wakuu hivi masharti ya dhamana ya Mbowe hayakuhusisha uwasilishaji wa pasipoti polisi kama dhamana?
 
Tatizo sio Mboe wala Mange Kimambi tatizo ni serikali ya chama cha mapinduzi na mipango mibovu isio tekelezeka kama serikali imesema itapeleka mikataba ya madini Bungeni alafu haikupeleka tatizo ni Mboe na Mange kimambi? Kama serikali haina majibu kwa walipa kodi tilion 1.5 zipo wap? Kama serikali haiweki wazi bajeti ya manunuzi ya ndege tatizo ni Mboe? Kama Rais ana vunja katiba kukataza mikutano ya kisiasa Tatizo ni Mange? Duh hoja zako zakijinga kabisa
 
Sawa andamana basi kisha utajua kama ulikua inachuuzwa ama unatahadharishwa
Wewe ni mtu au robot?

Tatizo langu sio kuandamana, tatizo ni hizo tuhuma hewa mnazotaka kumpakazia mtu asiye na hatia kisa ni chuki zenu kwake.

Kama mna ushahidi kwanini msimfungulie kesi mahakamani na sio kuandika tuhuwa zisizo na mashiko kama mahohehahe
 
Alieturoga wa tz bado hajapatikana ila ulozi wake ni mkali sana kiasi kwamba waliobahatika kujitambua nibwachache sana,,hivi kwa hali ilivyo tz sasahv bado kuna mtu anahitaji kupimwa mkojo au ubongo ndo aelewe kuwa tunapokwenda sipo??
Wapo mkuu wanaotakiwa kupimwa hadi vinasaba kubaini kama ni binadamu au ni mazombi
 
Wewe ni mtu au robot?

Tatizo langu sio kuandamana, tatizo ni hizo tuhuma hewa mnazotaka kumpakazia mtu asiye na hatia kisa ni chuki zenu kwake.

Kama mna ushahidi kwanini msimfungulie kesi mahakamani na sio kuandika tuhuwa zisizo na mashiko kama mahohehahe

Mna tuhuma hewa ngapi kwa JPM.
 
Nimemuona Mbowe akiwa na baadhi ya Watanzania wa hapa Marekani wakijadiliana mambo na baadaye akiwa na Mange Kimambi ambaye amekuwa akiunga mkono harakati za kisiasa za CHADEMA zenye mlengo wa kuichafua Serikali, viongozi wa Tanzania hasa Rais John Magufuli na nchi ya Tanzania.
Watanzania waliopo Marekani ambao wamemshuhudia Mbowe akiwa hapa pamoja na Mange Kimambi katika mipango yao ya kuhamasisha maandamano wanaonya juu ya upuuzi huu, na wanasema watasema kila wanachokifanya hapa Marekani.
Kweli wewe ni punguani wa akili, Mara nimemuona Mbowe akiwa na baadhi ya watanzania wa hapa Marekani wakijadiliana Mambo na baadaye akiwa na Mange Kimambi,mara watanzania waliopo Marekani wamemshuhudia Mbowe akiwa hapa pamoja na Mange Kimambi halafu unajiita uko Marekani.

Ni Marekani ileile ya Trump aliyemjambisha Bwana kiduku mpaka kalazimika kufanya mazungumzo na Marekani sambamba na kuachana na silaha za nyukria? au ni Marekani ya milembe?.
 
*MPANGO MCHAFU WA MANGE KIMAMBI NA FREEMAN MBOWE WAVUJA!!!!!!!!*

• Wakutana Marekani kujadili mipango ya kuivuruga Tanzania
• Watanzania waishio Marekani watahadharisha.

Na Julius Bernard, Maryland USA.

Imethibitika, Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe ametua nchini Marekani na kufanya kikao cha siri na Mange Kimambi, Mwanadada anayetumia mitandao ya kijamii kuhamsisha maandamano haramu na kuishambulia Serikali ya Tanzania.

Mbowe ametua Marekani kutoka Tanzania, pasi kutolewa taarifa yoyote kwenye vyombo vya habari wala mitandao ya kijamii kama ambavyo viongozi wanasiasa wamekuwa wakifanya hasa ndani ya chama chake cha CHADEMA.

Nimemuona Mbowe akiwa na baadhi ya Watanzania wa hapa Marekani wakijadiliana mambo na baadaye akiwa na Mange Kimambi ambaye amekuwa akiunga mkono harakati za kisiasa za CHADEMA zenye mlengo wa kuichafua Serikali, viongozi wa Tanzania hasa Rais John Magufuli na nchi ya Tanzania.

Kwa sasa Mange anahamasisha maandamano haramu anayoyatangaza kuwa yatafanyika tarehe 26 Aprili, 2018 siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Ninachokiona dhahiri ni njama halifu za kuichafua Tanzania, Mbowe anafanya mbinu zote hizi kuhakikisha nchi haikaliki na hili ni jambo ambalo Watanzania lazima walielewe.

Mange Kimambi anahamisisha maandamano tarehe 26 Aprili, zimebaki siku tatu kufikia tarehe hii na tayari Mbowe amekimbia Tanzania na kuja huku Marekani ili Watanzania watakaothubutu kuandamana wakutane na mkono wa dola wakati yeye akiwa salama salimini.

Hii ina maana kuwa Freeman Mbowe na Mange Kimambi wamechora mpango huu wa kutaka watu waandamane kiharamu, wakumbane na vyombo vya dola, waumizwe ama wapoteze maisha kama alivyosema yeye mwenyewe wafe kama 100 au 200 ilihali yeye na mhamasishaji wa maandamano Mange Kimambi wapo Marekani wanakula bata.

Watanzania waliopo Marekani ambao wamemshuhudia Mbowe akiwa hapa pamoja na Mange Kimambi katika mipango yao ya kuhamasisha maandamano wanaonya juu ya upuuzi huu, na wanasema watasema kila wanachokifanya hapa Marekani.

Na hii ndio imekuwa janja ya wanasiasa wengi kuhamasisha maandamano na kukimbilia mafichoni pale wanapoona mkono wa dola hautawaacha. Wengi wamekuwa wakijificha majumbani kwao au kusikojulikana ndani ya nchi, lakini safari hii Mbowe kaona akimbilie nchi nyingine.

Tulioko Marekani na tunaofuatilia hali ya nyumbani Tanzania tunajua hakuna cha maandamano wala mikusanyiko itakayofanyika kwa kuhamasishwa na Mange Kimambi, na itakuwa ajabu sana kama vyombo vya dola vitavumilia hata kwa dakika moja jaribio lolote la kuwaacha watu waandamane ama kukusanyika visivyo halali.

Nimalizie kwa kuwatakia heri Watanzania wenzangu wote huko Tanzania mnapoelekea katika maadhimisho ya siku ya Muungano Aprili 26, tuendeleeni kujenga nchi, tushikamane na serikali na Rais Magufuli ambaye ameonesha dhamira ya kweli ya kuitoa nchi katika mkwamo wa uchumi na kujenga uchumi imara, wa kujitegemea, wenye heshima na endelevu kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Nchi zote zilizoendelea zilipita katika kipindi hicho na watu kama akina Freeman Mbowe na washirika wake wanaotumiwa na wanyonyaji na mabepari walidhibitiwa kwa nguvu zote na bila kuona haya.

Kasomeni wakati Baba wa Taifa la China Mao Zedong (Mao tse-Tung) aliyeishi kati ya mwaka 1893 na mwaka 1976 alipoamua kuchukua hatua ya kuijenga china, alipata upinzani mkubwa kutoka kwa baadhi ya wanasiasa lakini alikomaa nao na China ikapiga hatua kubwa zilizojenga msingi imara uliopelekea China ya leo.

Kwa heri.
we need the bloody 1.5tr back. and fast!
 
Alieturoga wa tz bado hajapatikana ila ulozi wake ni mkali sana kiasi kwamba waliobahatika kujitambua nibwachache sana,,hivi kwa hali ilivyo tz sasahv bado kuna mtu anahitaji kupimwa mkojo au ubongo ndo aelewe kuwa tunapokwenda sipo??
Na wewe acha mawazo ya kiushirikina. Unawaza kurogwa? Tena watanzania? Sio wote wanarogeka ! Simama na damu ya Yesu uone.
 
Na wewe si ndo walewale. Akili yako nyembamba kama ya mange kama uzi wa kushonea nguo. Ile hela kwa mwenye akili hawezi, ni kulink matukio na shughuli za serikali utagundua kitu. Serikali haiwezi kukwambia kila kitu inachokifanya. Vingine ni siri yake. Timu ukawa acheni ubwege na kulishwa maneno.
Yani wewe kweli akili yako ndio kabisa sio hata nyembamba bali ni hewa kabisa.

Eti serikali sio lazima iseme kila kitu vingine ni siri?????

Upumbavu kama huu ndio unatakiwa ukemewe, yani kodi nalipa mimi alafu matumizi ya hiyo kodi unataka yawe siri?

Kweli hii nchi bado tupo nyuma sana, siamini kama kuna watu bado wana akili za ki-zombie kama wewe.

Au kuna under age humu jamani?
 
Nyie watanzania mnaoishi Marekani ni watu wa hovyo sana. Kwanza unasema amefanya mazungumzo ya siri alafu hapo hapo unasema umemwona akiwa na Mange, kuna mantiki hapo?

Alafu unadai kuwa kila kiongozi akisafiri nje ya nchi lazima chama kitanganze au lazima apost kwenye mitandao? Kweli? Nilifikiri mtu kufika kuishi tu Marekani basi hata fikra zako zinakuwa zimebadilika.

Alafu pia nilidhani kwakuwa mnaishi katika nchi inayoongoza kwa democracy duniani basi mngeishauri serikali iruhusu maandamano ya amani ila mnayapinga kama wapumbavu.

Kwanza siamini kama hii kitu imeandikwa na mtu anaeishi Marekani, wapuuzi wa Lumumba mnatuchuuza hapa.
Nawe umemuamini km Mbowe yupo Marekani,labda Marekani ya Chato.
 
Back
Top Bottom