Mtazamo wangu ni kuwa muandishi ameandika makala kwa kutumia hisia zaidi ya uthibitisho. Kama anavyowakosoa CCM kwa kujenga hoja ya madi huu bila ya kutupa uthibitisho wa vyanzo vya pesa n.k, ndivyo yeye alivyoshindwa kutupa uthibitisho wa kwa nini mradi huu haufai.
Ndugu zangu, lengo kubwa lisilosemwa la kujenga hilo jiji jipya la Kigamboni ni kukubali kuwa watawala wetu wa leo wameshindwa kuboresha na kujenga jiji la Dar la sasa. Ni kukubali kuwa kufanya jiji la Dar la sasa kuwa la kisasa kumewashinda sasa wanataka kujaribu eneo jipya wakiamini kuwa wataweza.
Nna mashaka mengi na hili hitimisho alilolifikia mwandishi kuwa lengo kubwa lisilosemwa ni kuwa watawala wameshindwa kuboresha jiji la Dar kwa hiyo wameamua kujaribu kwengine. Mwandishi amefikia hitimisho hilo kama nani? Mtaalamu wa mipango miji? Mwandishi aliyetumia vielelezo au ni maoni binafsi yasiyofungamana na nukuu za kitaalamu?