KWELI Mpapai dume ukifungwa gunzi la mhindi au kitu chochote huzaa

KWELI Mpapai dume ukifungwa gunzi la mhindi au kitu chochote huzaa

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2
Hivi kuna mpapai dume ambao watu wanasema ni ule ambao hauzai ila unatoa maua tu!?!

(b) Kufunga gunzi la mhindi lina maana gani kwa mmea kama mpapai usio zaa ili uzae??

1723685145808.jpeg
 
Tunachokijua
Mpapai ni mti wa familia Caricaceae ambao unazaa mapapai. Mti huo unatoka Meksiko lakini siku hizi hukuzwa kila mahali katika ukanda wa tropiki kwa sababu matunda yake hupendwa sana.

Mpapai dume ni mti wa mpapai ambao ukikomaa hutoa maua pekee na kuishia hapo, hauendelei kufikia hatua ya kutoa matunda, wakati mpapai jike wenyewe ukikomaa hutoa maua na kuendeleza hatua ya kutoa matunda.
1723682127152-jpeg.3070340

Kufunga gunzi la mhindi lina maana gani kwa mmea kama mpapai usio zaa ili uzae?
Katika mimea inayoweza kubadili jinsia yake ‘sex labile plant’ mojawapo ni mipapai na inabadilika pale mazingira yatakapokua magumu kwa yenyewe kuishi, ili kuendeleze kizazi chake ni lazima ubadilike kutoka dume kuwa jike ile uweze kuacha kizazi chake.

Katika baadhi ya jamii ni suala la kawaida kufunga gunzi kwenye mpapai dume. Mipapai hiyo baada ya kufungwa gunzi hubadilika kuwa jike na kuanza kuzaa. Mingine ukiiondolea gunzi hurudi kuwa dume na kutoa maua badala ya kuzaa kama mwanzo.

Kufunga bunzi/gunzi ni watu wameaminishwa, ila unaweza kufunga chochote kile hata ukipigilia misumari ilimradi mmea upate shuruba ‘stress’ hapo mmea utahisi kuwa upo kwenye mazingira magumu na unaweza kufa muda wowote. Hapo mmea utachukua hatua ya kubadili jinsia na kuzaa matunda haraka sana kabla haujafa ili uache kizazi chake.

Kwa baadhi ya mimea kama miembe na miparachichi ukiipa shuruba, kwa kugongelea msumari au vinginevyo, miti hiyo ili kuacha kizazi huzaa matunda mengi sana.

Hivyo basi, hakuna mahusiano yoyote kati ya mpapai na gunzi au bunzi la mhindi bali kinachofanyika ni mpapai kupewa shurba(stress) na lile gunzi lililofungwa ndio hufanya mpapai uweze kuzaa kwa kuhisi utakufa, hivyo unaweza kufunga kitu chochote na si gunzi pekee.

800px-Starr_061105-1375_Carica_papaya.jpg
Yaani jamii yetu inaamini sana hili. Ngoja tusubiri majibu. Wngine husema ukiupigilia msumari kwenye mpapai dume, pia hugauka na kuanza kuzaa
 
Africa raha sana!
Utasikia hata wanawake ambao hawashiki mimba ndio wale ambao hawakuwahi beba chochote migongoni mwao mithiri ya mtoto mgongoni.

Mpapai dume ni dume tu hata ukiubebesha guzi ila kuna namna nyingine tofauti kabisa na gunzi ndio iufanyao mpapai dume uzae nimeona kwa macho. Ya gunzi nimeshajaribu kwa mipapai mitano tofauti bila mafanikio.
Hiyo namna nyingine nitafuatilia zaidi.
 
Hizi Imani hizi acheni tu ona Sasa na huko nkurumah tower kumejaa wasomi😅
Yes kumejaa wasomi, lakini usisahau, kule Nkuruma street hata wa Kiparang'anda wanafanya biashara zao za nyama za mishikaki au maji ya kunywa. Sasa kijiweni kwake ndo kunakuwa na mambo hayo
 
Hii hata bi mkubwa home nilikuta amefunga gunzi la mhindi kwenye mpapai nilipomuuliza kwanini kafanya hivo akasema ule mpapai ni dume! Sasa nikamuuliza tena inahusianaje kati ya kubebesha gunzi ili shina la mpapai dume utoe matunda? Ex wangu akanipigia nikaondoka kabla bi mkubwa hajanijibu, nikienda kumtembelea disemba nitaangalia kama mpapai dume ule umetoa matunda!...
 
Binafsi nina amini katika hili kwasababu nilishawahi kuufunga gunzi mpapai uliokuwa unasemekana ni dume nyumbani na ukaanza kuzaa. Sijui kuna mechanism gani ila that's what happened on my experience
 
Yaani jamii yetu inaamini sana hili. Ngoja tusubiri majibu. Wngine husema ukiupigilia msumari kwenye mpapai dume, pia hugauka na kuanza kuzaa
Ni kweli kuna eneo nilipanda mipapai yoooote ikawa DUME. Nikaikata yooote nikaa ,anamoja ilipofika kipindi cha kuzaa yote ikawa DUME TENA. Bila maelekezo ya mtaalamu nitafutamagunzi ya kuyafungia . Hakika mipapai yote inazaa tena papai zake ni tamu kama embe dodo.
 
Back
Top Bottom