Mpesa Safaricom- Vodacom,

hehehe wachekesha, nimejifunza kwa njia ngumu. nitakuwa naandika nasoma narudia namwomba mtu aisome tena alafu ndio natuma.
 
Huo utapeli wa kulipa na Mpesa kisha wanareverse ndio ulifanya Safaricom waje na ile till number. Hiyo hamna cha kureverse wala nini. Kama ni kweli umekosea unaenda kuongea na mwenye biashara.
 
kweli kabisa, wanafaa pia hela ikitumwa angalau ichukue ata dakika 30 kabla kumfikia anayepokea. kuwa makini sana ukituma hela, nimejifunza sasa. nimepoteza laki kadhaa za Tz.
laki ni pesa ndogo sana hapa Tanzania @ be calm bro
 
Kwani Safaricom (Ke) siyo Vodacom (Tz)? Kwanini wasi-exchange informations as long as wote ni ndugu?...

Kwa sababu kisheria, haya ni makampuni mawili tofauti.

Pili kwa kuwa zipo nchi mbili tofauti, zinaongozwa na sheria tofauti, chini ya mamlaka tofauti TCRA kwa TZ na CA kue Kenya.

Tatu, kwa kuwa hii ni international transfer (sio kama voda-voda) exchange of subscriber information nafikiri itabidi itungiwe sheria maalum kama vile sheria za benki au international money transfer.
 
Aki pole sana shiku,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…