sili SG
Member
- Oct 12, 2018
- 22
- 26
MJINGA
Mjinga akimaliza la saba anaanza biashara ya mkaa halafu atachoma mahindi halafu atauza miwa, atalima viazi.
Baada ya miaka miwili atafungua duka la nguo atasafiri kwenda Dar kufunga mzigo....
Kila hela atakayopata ataitunza kwa nidhamu kuu.
Matokeo yake meneja wa benki atavutiwa na nidhamu hii atamuita na atamuuliza kama atapenda mkopo na malengo yake.
Mjinga atajieleza wazi kua akikopeshwa atapanua duka lake, atainunua nyumba aliyopanga duka na atanunua fuso la kusomba mzigo wake badala ya kukopa kwani hela anayotumia kulipa kodi na kukodi mafuso ni mara nne ya hela ya kulipa mkopo.
Baada ya miaka miwili mjinga kamaliza deni na kachukua mkopo mwingine kanunua mabasi manne ya kwenda Dar Mbeya Songea na watu watasema ni mchawi kaua wazazi wake wakati walikufa wakiwa na umri wa miaka kati ya 85 - 99
MJANJA WA MJINI
Huyu atapiga mesheni town na kufanikiwa kuchukua mkopo mkubwa huku akiweka hati ya nyumba ya urithi kama dhamana....
Akiishapata mkopo atanunua BMW X6 ya kupigia misele, mchepuko vogue range na ataitisha bonge la pati kujipongeza kupata mkopo....
Atatesa sana mjini kila kona .
Hela itakapokaribia kuisha atainvest kwenye biashara ya madini atauziwa vichupa akiambiwa almasi.....
Baada ya miaka miwili atafilisiwa na nyumba itapigwa mnada na atasema karogwa
MSOMI
Huyu atafanya kazi weee lakini hakuna savings kwani kila anachoingiza kina matumizi yake kisomi.....
Atakapochoka kuteswa mjini atachukua mkopo......
Atanunua gari ya familia....
Ataezeka nyumba yake
Atabaki na deni la kulipa mpaka amalize huku akiandamwa na barua za default..
Huyu hana wa kumlaumu ila ujuaji wake...
Wakuu
Tumheshimu mjinga
Ana nidhamu ya hela na kipaji cha biashara.
Kupata hela sio kazi bali kuitunza na kuiheshimu.
Mjinga akimaliza la saba anaanza biashara ya mkaa halafu atachoma mahindi halafu atauza miwa, atalima viazi.
Baada ya miaka miwili atafungua duka la nguo atasafiri kwenda Dar kufunga mzigo....
Kila hela atakayopata ataitunza kwa nidhamu kuu.
Matokeo yake meneja wa benki atavutiwa na nidhamu hii atamuita na atamuuliza kama atapenda mkopo na malengo yake.
Mjinga atajieleza wazi kua akikopeshwa atapanua duka lake, atainunua nyumba aliyopanga duka na atanunua fuso la kusomba mzigo wake badala ya kukopa kwani hela anayotumia kulipa kodi na kukodi mafuso ni mara nne ya hela ya kulipa mkopo.
Baada ya miaka miwili mjinga kamaliza deni na kachukua mkopo mwingine kanunua mabasi manne ya kwenda Dar Mbeya Songea na watu watasema ni mchawi kaua wazazi wake wakati walikufa wakiwa na umri wa miaka kati ya 85 - 99
MJANJA WA MJINI
Huyu atapiga mesheni town na kufanikiwa kuchukua mkopo mkubwa huku akiweka hati ya nyumba ya urithi kama dhamana....
Akiishapata mkopo atanunua BMW X6 ya kupigia misele, mchepuko vogue range na ataitisha bonge la pati kujipongeza kupata mkopo....
Atatesa sana mjini kila kona .
Hela itakapokaribia kuisha atainvest kwenye biashara ya madini atauziwa vichupa akiambiwa almasi.....
Baada ya miaka miwili atafilisiwa na nyumba itapigwa mnada na atasema karogwa
MSOMI
Huyu atafanya kazi weee lakini hakuna savings kwani kila anachoingiza kina matumizi yake kisomi.....
Atakapochoka kuteswa mjini atachukua mkopo......
Atanunua gari ya familia....
Ataezeka nyumba yake
Atabaki na deni la kulipa mpaka amalize huku akiandamwa na barua za default..
Huyu hana wa kumlaumu ila ujuaji wake...
Wakuu
Tumheshimu mjinga
Ana nidhamu ya hela na kipaji cha biashara.