Mpina yuko sahihi, Wizara walitaja Idadi ya mikataba bila kutaja jina la mkataba na thamani ya kila mkataba

Mpina yuko sahihi, Wizara walitaja Idadi ya mikataba bila kutaja jina la mkataba na thamani ya kila mkataba

Mkuu, bado hujajibu swali la msingi. Kwahiyo aliyekosea hapaswi kurekebika?
Alikua mbunge wa kawaida alikua Mpiga kelele sana enzi mwenyekiti wa kamati ya biashara na viwanda. Alipopewa unaibu-waziri 2015 akasaliti yote aliyosimamia.
Hoja iwe hivi; Mpina sio sehemu ya serikali kwa sasa! Kiapo chake ni kwaajili ya wananchi na nchi kwa ujumla wake, SIO JUKUMU LAKE KUTUNZA SIRI ZA BARAZA LA MAWAZIRI.
Sio kweli, kwa katiba yetu waziri lazima awe mbunge so Kila mbunge ni potential waziri tofauti na Kenya kwamba ukiamua kuwa mbunge huwezi kuwa waziri. Ndio maana wapiga kelele wote kuanzia Nape, Bashe, na Mpina walipopewa uwaziri wakakaa kimya kulamba asali. Ila kabla ya hapo walikua moto kweli utadhani wazalendo.
Ndani ya Baraza, Boss ni mmoja, na ndio mfumo ulivyo, huwezi kumu-outclass boss, iwe siasani au ajirani sio?
Sasa kama anajua Hilo anategemea huyo waziri afanyeje kama yeye alishindwa kumpinga rais? Si ndio unafiki naousemea huu. Kitu alichoshindwa yeye mwingine atawezaje?
Usipokubaliana na maamuzi ya kikao, ama ujiuzulu au ukae kimya, SIO UKAYAONGEE NJE ya KIKAO cha BARAZA! Dhima nzima ya kusema, mtu anapewa nafasi fulani kufungwa mdomo, sio ili naye awe sehemu ya UPIGAJI, ila awe chini ya MFUMO utakaomzuia kufanya atakavyo.
Yeye anataka uwazi si ndio, issue sio kuongelea nje ya baraza la mawaziri. Issue ni yeye Mpina akiwa waziri wa uvuvi obviously Kuna miradi mingi tu ya blue economy Ali sign je Kuna ambao ameuleta bungeni? Kama hakuuleta kwanini anajifanya ndio ana uchungu na mikataba kuwa wazi Leo?
Lisu, Mbowe, wamepewa walivyovikosa, leo wanaongea nini?
Hawa hawajapewa kitu vyote walivyopewa iwe ruzuku, stahiki ya matibabu au mikutano zipo kisheria hakuna favor so sio mfano sahihi. Kingine hao kina Zitto au Mbowe hajawapewa uwaziri au Urais so hawana mamlaka ya kufanya maamuzi. So mfano ni irrelevant
 
Ninawashangaa sana wanaombeza Mhe. Mpina. Mhe. Mpina was 100% right. Tujiulize tu kuleta ripoti ya mikataba mbele Bunge bila viambatisho kwa mfano mkataba Na. 1 kiambatisho ni hiki ndiyo sheria inavyotaka. Kumtuhumu kuwa analilia cheo cha Uwaziri haina mashiko. Hoja hapa ni sheria kuleta orodha ya mikataba bila viambatisho?. Tuache mambo ya ushabiki. Mimi ninatupa lawama kwenye kiti cha Spika kunyamazia mambo ya msingi. Sijui Bunge letu lina matatizo gani.
Yeye alipokua waziri aliwahi fanya hivyo??. Sheria ya TEITI inataka mikataba ya extractive industry iwekwe hadharani yaani page zote kama ni 1000 zisomwe na kamati za bunge. Cha kushangaza yeye hakuwahi peleka hata mkataba mmoja. Eti Leo Hana uwaziri ndio anajifanya ana uchungu na usiri wa mikataba? Huu unafiki ndio tunaupinga.

Usidanganyike ndugu hakuna mwana CCM ana uchungu na mikataba kuwa Siri. Kinachomuuma ni kwamba mikataba ya Siri wanaofaidika nayo ni waliopo Serikalini yeye hapati mgao. Ila akipewa uwaziri unadhani ataileta hiyo mikataba?? Kama alishindwa akiwa waziri ataweza sahivi?
 
Wewe ndio mpumbavu, kwani hizo sheria hazikuwepo tokea enzi za JPM? Huyo Mpina akiwa waziri ni mkataba upi wa wizara yake aliwahi peleka bungeni? Kakosa uwaziri anaanza kelele alafu unataka wote tuwe mazuzu. No my friend awadanganye wajinga wengine sio Mimi. We Kaa hapo ulidhani anapigania haki zako wakati mwenzio anataka kurudishiwa uwaziri.

Tutarudi hapa akishaupata uwaziri nifukue nyuzi zenu hizi baada ya kukana yote anayopigia kelele wakati huu.
Ukweli NDIYO huo kuwa huyo mnafiki na mzandiki Mpina anausaka uwaziri and nothing else. Alipokuwa waziri wa uvuvi alitesa Sana wananchi hadi tukawa tunakosa samaki na dagaa tokana na yeye kuwachomea wavuvi vitendea kazi na alizuia raia kusafirisha dagaa hata wa kula.
 
Kwanza mtu ukishakuwaga waziri halafu baada ya kuukosa unakuja kubwabwaja uraiani ni kukosa hekima. Mengine pengine ameyajua ndani ya baraza la mawaziri ambayo uliapa kulinda km siri za baraza la mawaziri leo unataka uonekane unajua mambo ni ushamba tu. Mpina hafai tena kuwa kiongozi mkubwa nchi hii.

Akajifunze hekima kutoka kwa George Simbachawene. Ni wananchi wachache watakuamini tena kuwa unatetea wananchi zaidi ya tumbo lako. Ukishakuwa mserikali unatakiwa uendelee kuzungukia mlemle. Mbona Dr. Medard Kalemani ametulia? Huyu hajafunzwa vizuri au ana upungufu wa malezi. Ni mtoto wa single mother au ushamba tu wa kinyantuzu?
Lakini anachokijadili ni siri za baraza au vitu vilivyowekwa wazi na CAG?

Hakuna sheria ya kulinda confidentiality ya taarifa uzipatazo ukiwa nafasi fulani kisha ukatoka?

Ukizungumza maadili una maanisha nini?
  • Tume ya maadili ina maadili?
  • TAKUKURU ipo namba ngapi kati ya taasisi zinazoongoza kwa rushwa na ubadhirifu?
  • Polisi haikutajwa kwenye rushwa na uvunjifu wa haki?
  • Mahakama si ndo mama lao kwa kila kitu?

Ni kina nani waliitwa STUPID, WAPUMBAVU?

Leo unajua kuwa Mwigulu kakopa 1.28trillion kiholela tu bila idhini ya Bunge, 1.7 trillion kalala nazo mbele kwa mujibu wa Mpina, kutokana na taarifa ya CAG.

Sasa, nani bora, yule anayekwapua na kusubiri nafasi nyingine kukwapua, au aliyekwapua, hana nafasi, anawajuza na kuanika ukwapuaji hadharani?

  • Waziri walioiba na kusema ni VIJISENTI au HELA YA MBOGA? Au anayetaka BUNGE lijadili waganga wa kienyeji?
  • Raisi aliyekopa Tzs trilioni 7 na hazikuingia serikalini kwa mujibu wa BBC, CAG hana habari!

Ukumbuke hiyo pia ni hulka ya Watanzania wezi wengi, Lowasa hakutoka tu hivi hivi, waligombana ndani huko, wenyewe kwa wenyewe, sis tukaijua Richmond mpaka akina Ruge.
 
Mhe. Mpina nianze kukupongeza kwa michango yako kila Bunge linapokaa. Leo ulipokuwa unachangia kwenye bajeti ya Wizara ya Sheria na Katiba ulitoa hoja ambayo kila Mtanzania atakuunga mkono.

Wizara katika taarifa yake walitaja Idadi ya mikataba bila kutaja jina la mkataba na thamani ya kila mkataba. Unapotayarisha taarifa yako lazima iwe detailed. Wizara inataja tu mikataba bila kuambatisha annexes. Je hiyo ni sahihi?.

Hapa Mhe. Mpina alikuwa sahihi kabisa. Leo nimeishangaa kiti cha Mwenyekiti kupuuzia hoja ya Mhe. Mpina. Mimi sielewi Bunge hili linafanyaje kazi kupuuzia mambo ya msingi kama hoja ya Mhe. Mpina. Pili, lingine alilouliza ni Azimio lililoletwa mbele ya Bunge ikidaiwa kuwa tayari ilikwishajadiliwa na Bunge kumbe bado. Hapa pia kiti cha Mwenyekiti linanyamazie jambo zito kama hilo.

Mhe. Mpina utachukiwa sana kwa kusema ukweli na sisi tuliopo huku uraiani tunakuombea kwa Mungu. Hoja zako ni za ukweli lakini kiti cha Spika kinakuangusha.

Nihitimishe kwa kusema kuwa nimemshangaa sana Mwenyekiti kwa kupuuzia hoja ya Mhe. Mpina. Hivi Bunge letu lina matatizo gan?. Time will tell.
Sasa nimeanza kuona na kukubali kuwa kifo cha JPM ni hasara ya Karne moja wa watanganyika.
 
Mhe. Mpina nianze kukupongeza kwa michango yako kila Bunge linapokaa. Leo ulipokuwa unachangia kwenye bajeti ya Wizara ya Sheria na Katiba ulitoa hoja ambayo kila Mtanzania atakuunga mkono.

Wizara katika taarifa yake walitaja Idadi ya mikataba bila kutaja jina la mkataba na thamani ya kila mkataba. Unapotayarisha taarifa yako lazima iwe detailed. Wizara inataja tu mikataba bila kuambatisha annexes. Je hiyo ni sahihi?.

Hapa Mhe. Mpina alikuwa sahihi kabisa. Leo nimeishangaa kiti cha Mwenyekiti kupuuzia hoja ya Mhe. Mpina. Mimi sielewi Bunge hili linafanyaje kazi kupuuzia mambo ya msingi kama hoja ya Mhe. Mpina. Pili, lingine alilouliza ni Azimio lililoletwa mbele ya Bunge ikidaiwa kuwa tayari ilikwishajadiliwa na Bunge kumbe bado. Hapa pia kiti cha Mwenyekiti linanyamazie jambo zito kama hilo.

Mhe. Mpina utachukiwa sana kwa kusema ukweli na sisi tuliopo huku uraiani tunakuombea kwa Mungu. Hoja zako ni za ukweli lakini kiti cha Spika kinakuangusha.

Nihitimishe kwa kusema kuwa nimemshangaa sana Mwenyekiti kwa kupuuzia hoja ya Mhe. Mpina. Hivi Bunge letu lina matatizo gan?. Time will tell.
Atateuliwa kuwa Balozi iki akae mbali na mama.

Mama anapaswa kula kwa utulivu.

Time will tell
 
Back
Top Bottom