Mpira (ndondo) ulifanya nikapotea Morogoro

Mpira (ndondo) ulifanya nikapotea Morogoro

Mohammed wa 5

JF-Expert Member
Joined
Jun 20, 2022
Posts
1,215
Reaction score
3,035
Habari za zenu Wana Jf
Throw back Tuesday

Ilikuwa mwezi wa 12 miaka mingi kidogo nyuma baada ya kwenda likizo Morogoro tulifikia kwa baba mdogo ambaye alikuwa anaishi maeneo ya tazara

Siku moja majira Kama ya saa 8 au 9 baada ya kula msosi nikawa nimekaa kwenye kibaraza Cha mbele ya nyumba Niko alone Sina rafiki ukicheki ni mgeni pale mtaani na nyumba aliokuwa anaishi baba mdogo inaangalia barabara kubwa ya mtaa wakati nimekaa pale nje ya nyumba ghafla naona watu wanapita wapo kimakundi waongelea habari za mpira kila kundi linalopita habari ni mechi ya leo.

Ikabidi niwafuate kwa nyuma na Mimi nikajichanganya kwenye kundi moja kila wakipiga hatua me Niko nyuma baada ya kitambo kiasi Cha kutembea tukaja kutokezea kwenye uwanja wa shule na baada ya kufika pale nikawa nashangaa jinsi watu walivyojaa wakisubiri mechi kumbe siku Ile ilikuwa fainal ndo mana kulikuwa na idadi kubwa ya watu nikatafuta sehemu nzuri ili niweze kucheki mechi vizuri ukichek nilikuwa kachalii mdogo nikapata nafasi mbele kabisa nikawa nimekaa chini siunajua sis wengine tumeanza kupenda mpira afu timu

Mpira ukaanza nakumbuka ilikuwa ni mechi Kali Sana kati ya kata moja na kata nyingine zilizofanikiwa kufika fainali nakumbuka mpaka mpira unaisha matokeo ni 1-1 na mshindi alipatikana kwenye penalty Baada mpira kumaliza watu wakaanza kutawanyika kuondoka Sas Mimi kwa akiri za kitoto nikajua nyumbani si nyuma tu hapo kila nikitembea hivi Ile nyuma tuliofikia pale kwa baba mdogo sipaoni nimetokea kwenye mazingira tofauti kabisa na Giza lishaanza kuingia ikabidi nirudi Tena kule uwanjani nikakuta wamebaki watu wachache wanaendelea kujadili Ile mechi.........

Itaendelea...........
Ni simulizi fupi tu wakuu usipitwe na sehemu inayokuja ili ujue nilifika vipi nyumbani pale kwa baba mdogo na kule nyumbani walikuwa na Hali gani na Giza lishaingia na pale nyumbani sijaonekana????
 
Sasa Kuna haja gani ya kutusubirisha wakati simulizi ni fupi pasua yote aiseeh..
 
Back
Top Bottom