Mpoki ukiwa kwenye kipindi cha Ubaoni E-FM unaboa

Mpoki ukiwa kwenye kipindi cha Ubaoni E-FM unaboa

Wanajamii

Radio E-FM imemuajiri bwana Mpoki (mchekeshaji maarfu) kama radio presenter wao wa kipindi kinachoanza saa 10 jioni hadi saa 12 kinaitwa Ubaoni uyu jamaaa namkubali ni comedian mzuri tu anaejua kucheza na maneno ila sasa tunapoelekea anapitiliza.

images
images


Kwa wale mnaosikiliza kipindi icho naamini mtakubaliana na mimi naomba uongozi wa E-FM mumdhibiti uyu jamaa sio mda wote uwe wa masihara na utani na maneno ya kijinga TCRA muda sio mrefu naamini watashusha rungu apo
Huyu kujisahau na kukosa control ni kawaida yake kabisa nakumbuka utoaji wa tuzo flani ulio fanyika miaka michache iliyopita jamaa aliboa mpaka basi.
 
Si mlikuwa mnaisifia EFM hapa juzijuzi tu. Mara ooh Clouds wamepotezwa. "Mara ooh huu mchezo hauhitaji hasira". Kiko wapi sasa! Naona mmeshaanza kumeza matapishi yenu. Ngoma ya watoto haikeshi jamani.
 
...amezidi kwa pumba aisee daah..! alafu anataka aongee yeye tu mpaka naona kama kipindi kinavurugika na kinakosa muelekeo, hata huwezi kujua nani ni kiongozi na nani ni co hosts wa kipindi, ebu mpangeni huyo mpoki bado hajielewi anadhani redio ni sawa na comedy show....
Mathalan Zembwela ni comedian asilia lakini anajua wakati gani achomekee ya kwake lakini muda mzima wa kipindi yuko serious na yanayo husu kipindi na mada zake na amekuwa ni kivutio kwenye fani ya utangazaji na ana imudu vyema.
 
Si mlikuwa mnaisifia EFM hapa juzijuzi tu. Mara ooh Clouds wamepotezwa. "Mara ooh huu mchezo hauhitaji hasira". Kiko wapi sasa! Naona mmeshaanza kumeza matapishi yenu. Ngoma ya watoto haikeshi jamani.

Mkuu mbona kama umekuwa na hasira ghafla?

Hivi mtangazaji mmoja akikosolewa ndo kusema Ngoma ya Watoto Haikeshi.
 
Acha wivu mleta mada, na inaonesha hufahamu kuwa kile kpnd kinapendwa kwa sababu yake.
 
Mimi simuelewagi bikira. Amekaa kujisifia sifia tu. Sijui muhaya yule
 
Nasikia lunch ya watu ile
Basi ana haki ya kujiita bikra ila siku ndugu zake wakigundua wakapitisha mchango wakumpeleka milembe nami nitachangai maana kama sio punguani nini kujiita bikra hii si sawa hivi basata hawajaliona jina hili au chura tu ndo halina maadili
 
Basi ana haki ya kujiita bikra ila siku ndugu zake wakigundua wakapitisha mchango wakumpeleka milembe nami nitachangai maana kama sio punguani nini kujiita bikra hii si sawa hivi basata hawajaliona jina hili au chura tu ndo halina maadili
We acha tu.
Nahisi Basata wana lao....kwa wengine kimya
 
Back
Top Bottom