Mpya: Tume ya Rais ya EPA yalonga

Mpya: Tume ya Rais ya EPA yalonga

MWK, Sheria ilibadilishwa na mafisadi waliopeana ruhusa ya kukupua mali za Watanzania kila kona ya Tanzania. Walikubaliana kwamba watakaposhtukiwa kama wanaiba na kusaini mikataba mibovu basi wakirudisha walichokipata karika ufisadi wao mambo yote yatakuwa shwari.

Huu ni usanii wa hali ya juu, wabunge wa CCM wangechachamaa wahusika wote wa kashfa ya EPA, Richmond n.k. waswekwe rumande wakati uchunguzi unaendelea basi nina hakika hilo lingetokea.

Wabunge wamebwabwaja hakuna chochote kilichofanyika watuhumiwa wote bado wako huru wakiendelea kufaidi mapesa yao ya ufisadi.

Nilishangaa kusikia bunge limeahirishwa hadi April. Mtaahirishaje bunge wakati nchi imegubikwa na kashfa nzito nzito chungu nzima, kwani wasingweza kuitisha kikao cha dharura cha bunge hata cha mwezi mmoja ili kuhakikisha watuhumiwa wote wanaswekwa ndani!? Usanii kila kona, halafu Chiligati atakwambia wao CCM ndio waliwawajibisha mafisadi! wakati bado wako uraiani wanapeta!

Tatizo kubwa ni watu hawaelewi maana ya kufata sheria na kuwa dikteta ndio maana unaona mambo mengi yanawashinda kuyatatua, JK anafata sheria na hawezi kuamka akajitolea maamuzi kichwani, kamata yule weka ndani, huyu kaiba sweka jela. Anafanya shughuli zake kiumakini na kwa utaratibu unaokubalika kimataifa, ndio maana leo hii unaona kina lowassa, ingawa wengi wanaelewa kuwa ni rafiki yake mkubwa, wanasota nje ya uongozi. Unataka kuniambia amkamate amsweke jela wakati tayari kuna tume ya Bunge inashughulikia maswala hayo? Apingane na Bunge? huo utakuwa ni udikteta.

Hali kadhalika kwa EPA, makampuni yanajulikana na humo inawezekana kabisa kuwa wamo waliokopa kwa nia safi na wamo waliokopa kwa nia ya kutorudisha, huwezi ukakurupuka na kuwakamata uwasweke ndani, utapata faida gani ukisha wasweka? Utakosa pesa na utaendelea kuwalisha bure jela. At the same time ukitumia busara kidogo utazipata pesa zitakazoweza kupatikana, utazipata mali utazoweza kuzishika na kuna uwezekano mkubwa wengi wakaanza kurudisha, na hili la kuzipata fedha na mali ndio kipaumble. Na yote hayo lazima ayashughulikie kisheria, akienda kimsobe-msobe kama unavyotarajia, atajikuta hana alichofanya ila ni hasara juu ya hasara.

Tumeona jinsi Mkapa alivyokuwa akikalia maamuzi ya kushughulika na ufisadi kwa makusudi kabisa. Na kwa muda mfupi tu wa awamu ya nne tunaona jinsi JK anavyo yashughulikia masuala ya ufisadi ulioanza mbali sana. Na nani asiyeyaona mafanikio ya uongozi wake?. Asiyeona nadhani ana matatizo, kama si ya nanihii basi ni ya nanihii.

Kama tunaongelea unazi tu, haya tuendelee. Waswahili wanasema nyota njema huonekana alfajiri.
 
Yaani utawaweza,

hakusubiri hata afikishe post 20 ili aanze ufisadi!?!

mimi nashuhudia explosion tu hapa.... maana the first posts tu huyo kishaanza ohhh walongalongaji... mara mwanakijiji ndiye mwafrika wa kike ili mradi explosions tu! grrrrrrrrr

Tazama chini hapo, halafu niambie umeshapata jibu au bado?

.


MWANAKIJIJI acha utoto ukiona unashindwa hoja unakimbilia kubadili jina na kutumia la kike ili upewe huruma(Mwafrika wa Kike)

MKANDARA.

Mwafrika wa kike ni yule yule Mwanakijiji ana utoto wa kuingia na majina mengine kama KOBA, MADELA-WA MADILU, MWAFRIKA WA KIKE n.k

turudi kwenye mada vyombo vyote vya habari vya kimataifa vimesema Bush anakuja Tz ili kufuata masilahi ya nchi yake na kusisitiza kuwa AFRICOM ni agenda kuu ya ziara ya bush.

kwanini yuko Arusha kwenye Tanzanite? Ukimwi uko Bukoba vipi hajaenda uko?

Mwanakijiji au Mwafrika wa kike.


mtafute professor JOEL BARKAN ...
 
Wananchi,

Kwanza nakubali kabisa ni muhimu hela ZIRUDI. Kama watachukuliwa hatua au la hilo litafuatia na sidhani ni jukumu la tume kuwaambia watafanya nini mbeleni.

Ila hatua waliofikia ni ya kupongezwa, Serikali haifanyi mambo kwa kukurupuka. Kumbuka ukisharudisha hela ni ushahidi tosha kuwa uliiba. Sasa tatizo ni nini hapo, au ndo ile dhana yetu kuwa lazima tupinge tuu hata kama ni jambo zuri?.

Lipi la maana kulweka Lupango aliyeiba au kurudisha?, mie naamini kuwa kama ameiba basi akiwa na uwezo wa kurudisha ni nzuri sana tena AKIRUDISHA NA RIBA kuliko kumfunga na watoto wakaendelea kukaa chini mashuleni na wagongwa kufa kwa kukosa madawa mahospitalini.

Asanteni sana

FD
 
Wananchi,

Kwanza nakubali kabisa ni muhimu hela ZIRUDI. Kama watachukuliwa hatua au la hilo litafuatia na sidhani ni jukumu la tume kuwaambia watafanya nini mbeleni.

Ila hatua waliofikia ni ya kupongezwa, Serikali haifanyi mambo kwa kukurupuka. Kumbuka ukisharudisha hela ni ushahidi tosha kuwa uliiba. Sasa tatizo ni nini hapo, au ndo ile dhana yetu kuwa lazima tupinge tuu hata kama ni jambo zuri?.

Lipi la maana kulweka Lupango aliyeiba au kurudisha?, mie naamini kuwa kama ameiba basi akiwa na uwezo wa kurudisha ni nzuri sana tena AKIRUDISHA NA RIBA kuliko kumfunga na watoto wakaendelea kukaa chini mashuleni na wagongwa kufa kwa kukosa madawa mahospitalini.

Asanteni sana

FD

Ur making a point FD...wasi wasi serikali ya kishikaji hawa kawii kusema oooh pesa zimerudi hakuna haja ya kuwapeleka mahakamani hawa...na sisi kwa kusahau tupo makini...si unaona issue ya Dito na Zombe hazipo tena masikioni na midomoni mwa watanzania!!
 
Hivi sasa ndiyo kwanza nimemaliza kusikiliza tarifa muhimu kwamba ile Tume ya Rais ya EPA ya kuchunguza ubadhirifu wa fedha za malipo ya akaunti ya madeni ya nje pale BoT imeeleza kuwa imefikia mahali pazuri kutoa taarifa yake.

Tume hiyo katika taarifa yake imesema imeweza kusaidia kurejeshwa kwa kiasi kikubwa cha fedha zilizolipwa kitapeli kwa kampuni za kisanii.

Imesema kuwa mali zisizohamishika zimekamatwa maeneo mengi ya Dar na miji mingine, kuhusu mali zilizo ne ya Tanzania, tume hiyo imesema kuwa nazo zitapatikana karibuni kabla ya kukabidhi ripoti kamili kwa Rais Jakaya Kikwete..

Mwenyekiti amesema wananchi wote wanaombwa kutoa taarifa kwa tume hiyo kwa kutumia namba za simu zifuatazo

+255 784 994881

+255 784 231928

+255 784 785742


Haya jamani mambo yetu yale, kama mnafahamu mali za mafisadi wale wa BoT semeni ili turejeshe serikalini na ziuzwe kama hazihamishiki ili pesa zinazopatikana zikajenge barabara, kununua dawa, kuboresha elimu na dawa hospitalini.

Nawatakieni kila jema.

Many thanks kwenu Tume ya kuchunguza EPA ila.....

I'm more interested in figures than this ....!!! mahali pazuri inamaanisha nini?? na kiasi kikubwa cha fedha ni asilimia ngapi ya zile 100+ billions??
Naiomba tume kama itatoa tena taarifa basi watupe figures ili na sisi tuwe na imani kwamba kweli wamafikia pazuri na sio tu kwa maneno ya jumla kama ilivyofanya sasa.
 
FD yaani unasema mtu akisahihisha alichofanya asiadhibiwe? au mtu anapoadhibiwa mojawapo ya adhabu ni restitution? Kwanini tutangulize restitution before convictions?
 
Usanii mwingine hata unavuka maelezo ya kawaida. Yaani ni lini sheria za nchi zilibadilishwa na kuruhusu watuhumiwa wa wizi kurudisha mali na sio kupelekwa kwenye vyombo vya sheria.

Ina maana leo wale watuhumiwa wa wizi wa kuku na simu walioko Keko wanaruhusiwa kuachiwa huru as longer as wanarudisha kile walichoiba?

..mwk,

..this will set a very bad precedent!
 
yaani wamerudisha mali ili yaishe kimya kimya. Basi si waambiwe tu warudishe mali yaishe. Maana kutakuwa na umuhimu gani wa kuwafikisha mahakamani wakati wamesharudisha mali?

..inavutia sana. ngoja nami nitapiga deal la trillion 1 halafu nitairudisha baada ya miezi sita!
 
Tuwe 'Optimistic'. Kama sikosei, JK aliipa tume/kamati kazi ya kuchunguza hili na kuhakikisha 1. Fedha zilizoibwa zinarudi, na 2. kuwachkulia hatua wote walihusika na wizi huo wa fedha za umma. Fedha kuanza kurudi kwa 'wenyewe' ni hatua nzuri, na bila shaka hatua hii itafuatiwa na kufikishwa katika sheria wahusika. Huenda kuanza kuwachukulia hatua mapema kutaharibu ushahidi au kuzorotesha upatikanaji wa fedha zetu.

..waliochota pesa na wanaozifuatilia zirudi,wote si wajinga! wanajua kinachoendelea.

..toka mwaka juzi nakula ugali wangu kwa mlenda! nadhani hiki chakula hakitabadilika,wala siwazi kula tofauti!
 
Ahsante JK kwa uongozi wako, wenye macho tunauona na wenye masikio tunausikia. uzi huo huo, tunakuombea Mwenyeezi Mungu akuepushe na mahasidi wasioona unachokifanya kwa roho zao mbaya na akuepusha na fitna na majungu na visasi vya hao unao-washughulikia.

Haya wale wanaolonga longer humu waanze kuonyesha uzalendo wao, namba hizo.

Ahsante JK kazi tunaiona. Wengine waanze kukaa mkao wakula zamu yao inakuja.

Maswali yangu ni machache tu
1: Unapojipatia mali/pesa kwa kutumia nyaraka za kugushi,unakuwa
umetenda kosa la udanganyifu na kujipatia fedha au mali
visivyo halali? hawa wanarudisha fedha,je ndiyo kwamba
wamesamehewa au kuna hatua za ziada? tunaomba majibu
2: Tunampongeza JK kwa lipi katika hili? kwa kuwasamehe
wanarudisha fedha bila kufikishwa mahakamani au kwa vile some
of this money went to CCM campain via kagoda farm.
 
Hivi sasa ndiyo kwanza nimemaliza kusikiliza tarifa muhimu kwamba ile Tume ya Rais ya EPA ya kuchunguza ubadhirifu wa fedha za malipo ya akaunti ya madeni ya nje pale BoT imeeleza kuwa imefikia mahali pazuri kutoa taarifa yake.

Tume hiyo katika taarifa yake imesema imeweza kusaidia kurejeshwa kwa kiasi kikubwa cha fedha zilizolipwa kitapeli kwa kampuni za kisanii.

Imesema kuwa mali zisizohamishika zimekamatwa maeneo mengi ya Dar na miji mingine, kuhusu mali zilizo ne ya Tanzania, tume hiyo imesema kuwa nazo zitapatikana karibuni kabla ya kukabidhi ripoti kamili kwa Rais Jakaya Kikwete..

Mwenyekiti amesema wananchi wote wanaombwa kutoa taarifa kwa tume hiyo kwa kutumia namba za simu zifuatazo

+255 784 994881

+255 784 231928

+255 784 785742


Haya jamani mambo yetu yale, kama mnafahamu mali za mafisadi wale wa BoT semeni ili turejeshe serikalini na ziuzwe kama hazihamishiki ili pesa zinazopatikana zikajenge barabara, kununua dawa, kuboresha elimu na dawa hospitalini.

Nawatakieni kila jema.



KWANZA HIZO MALI/FEDHA ZINATAKIWA KURUDI KWA NJIA YA MAHAKAMA,

1.NAKUMBUKA RAIS ALIUNDA TUME KWAAJILI YA KUFANYA UCHUNGUZI NA KUTOA TAARIFA NA SI KUKUSANYA PESA

2.NANI KATOA MADARAKA KWA HIYO TUME KUWAAMURU WEZI KURUDISHA
FEDHA???

3.HIZI FEDHA ZIMERUDI WAPI. POLICE, KWA AG AU BOT???


KIKWETE HEBU ACHA UHUNI.... HII NCHI SI MALI YA MTU BINAFSI... FUATA SHERIA ZILIZOWEKWA
 
Guys, in Tanzania you can't get coffee and cream at the same time. You have to decide either coffee or cream, and i believe majority of us we will first ask for coffee and then pressurize for cream.

Kuna important factors hapa, wana kamati wametoa namba ya simu, instead ya sisi kucharuka ya kwamba watu wapelekwe mahakami, let use this number to call this commitee people and pressurize that govnt should send those individual to court.

Sasa tukianza kutumia tactic za kwamba we have to be wapinzani on everything that government propose, guess what? we are going to be loosers and they're winners. So, let use those number and call them tiredless kuomba wawapeleke waungwana mahakami.
 
Surely; at this stage, ambapo bado kamati teule inafanya kazi, bado tunaweza kutoa hukumu dhidi yao?
Tumeshapewa hadidu za rejea.
Kama waliambiwa wahakikishe hela zilizochukuliwa zinarejeshwa, how else would the kamati have gone about it?
kinachogomba hapa ni kwa vile hatujui hao watu walikuwa identified vipi; waliambiwaambiwaje warudishe, na wamarushishaje.
Naamini maswali hayo yatajibiwa pindi ripoti nzima ya kamati ikisomwa.

Na ninaamini itasoma hivi..." ..kamati teule iliagizwa kuhakikisha kuwa fedha zinarejeshwa..kwa kuzingatia agizo hilo, kamati ilipata nyaraka husiak kutoka ndani ya BoT na kupata majina ya watu/kampuni zilizopata fedha hizo haramu na kiasi kilichochukuliwa. kamati iliwaandikia wito wahusika ambapo walifika ofisi ya tume mmoja baada ya mwingine na kupatiwa taarifa kamili ya kuhusika kwao. Kisha tume iliwataka warejeshe fedha hizo kama hatua ya kwanza. wahusika walipewa siku... kufanya marejesho. fedha zilirejeshwa na kuwekwa kwenye account maalum iliyofunguliwa na tume kwa ajili hiyo...
Mapendekezo.
Pamoja na ripoti hii, tume inakabidhi kwa Mh Rais vielelezo vyote na nyaraka zote husika na kupendekeza vitumike kuwachukulia hatua za kisheria wahusika..."

Tume haina mamlaka ya kuwafungulia mashtaka hao jamaa; ila ina mamlaka ndani ya hadidu za rejea kuwataka warejeshe fedha. Kama hilo ni kosa basi wa kulaumiwa ni yule aliyewapa hizo hadidu.
Ila kwa msimamo wa kisheria, kurejesha kwao hizo fedha kni sawa na confession; kesi ikifika mahakamani there is no way watakataa kuhusika
So, by far, tume inaenda vizuri
Lets just give them time guys
 
Hali kadhalika kwa EPA, makampuni yanajulikana na humo inawezekana kabisa kuwa wamo waliokopa kwa nia safi na wamo waliokopa kwa nia ya kutorudisha, huwezi ukakurupuka na kuwakamata uwasweke ndani, utapata faida gani ukisha wasweka? Utakosa pesa na utaendelea kuwalisha bure jela. At the same time ukitumia busara kidogo utazipata pesa zitakazoweza kupatikana, utazipata mali utazoweza kuzishika na kuna uwezekano mkubwa wengi wakaanza kurudisha, na hili la kuzipata fedha na mali ndio kipaumble. Na yote hayo lazima ayashughulikie kisheria, akienda kimsobe-msobe kama unavyotarajia, atajikuta hana alichofanya ila ni hasara juu ya hasara.

Mkuu heshima kwako, vizuri tuna freedom of speech hapa JF. Naheshimu mtizamo wako, lakini naomba uniruhusu niwe na maoni tofauti. Kama wewe unaamini kuwa kuna watu walikopa kwa nia njema kupitia EPA, ni vizuri ukiweka wazi tujue kama EPA ilikuwa na mission nyingine ya kukopesha watu wa ndani kisirisiri na sio External Payment Areas. Naamini wewe unajua majina yaliyotajwa kwenye ripoti ya BOT a.k.a EPA, na ukawa hata na nguvu ya kusifu kuwa anafuata sheria, i wonder kama kuna yoyote amefikishwa kwenye mkono wa sheria ili mahakama ithibitishe ukweli. Sasa unaposema anafuata sheria sijui ni sheria ipi mpaka sasa imetumika kwa hao watu, ingekuwa ni vizuri kama ungeeleza wazi.
 
Surely; at this stage, ambapo bado kamati teule inafanya kazi, bado tunaweza kutoa hukumu dhidi yao?
Tumeshapewa hadidu za rejea.
Kama waliambiwa wahakikishe hela zilizochukuliwa zinarejeshwa, how else would the kamati have gone about it?

go to court! wanaoushahidi wa makampuni yote, wanajua ni kiasi gani kimechotwa, wanajua ni kampuni gani imegushi, wanajua ni nani alikuwa ofisa wa hiyo kampuni, wanajua kampuni iliandikishwa vipi n.k kwanini hawaendi mahakamani?

kinachogomba hapa ni kwa vile hatujui hao watu walikuwa identified vipi; waliambiwaambiwaje warudishe, na wamarushishaje.
Naamini maswali hayo yatajibiwa pindi ripoti nzima ya kamati ikisomwa.

Hilo ndilo kubwa. Nje ya Mahakama kinachofanyika ni kujitolea. Vinginevyo tufunge Mahakama kama watu wanaweza kufanya majadiliano na wahalifu without court sanction or jurisdiction. Watu wanapovunja sheria hawapelekwi kwenye kamati, wanapelekwa Mahakamani.


Na ninaamini itasoma hivi..." ..kamati teule iliagizwa kuhakikisha kuwa fedha zinarejeshwa..kwa kuzingatia agizo hilo, kamati ilipata nyaraka husiak kutoka ndani ya BoT na kupata majina ya watu/kampuni zilizopata fedha hizo haramu na kiasi kilichochukuliwa. kamati iliwaandikia wito wahusika ambapo walifika ofisi ya tume mmoja baada ya mwingine na kupatiwa taarifa kamili ya kuhusika kwao. Kisha tume iliwataka warejeshe fedha hizo kama hatua ya kwanza. wahusika walipewa siku... kufanya marejesho. fedha zilirejeshwa na kuwekwa kwenye account maalum iliyofunguliwa na tume kwa ajili hiyo...

Natumaini haitasomeka hivyo.

Mapendekezo.
Pamoja na ripoti hii, tume inakabidhi kwa Mh Rais vielelezo vyote na nyaraka zote husika na kupendekeza vitumike kuwachukulia hatua za kisheria wahusika..."

Hatua gani tena za kisheria? Yaani hatua za kisheria zichukuliwe baada ya adhabu kutolewa? Bado sijaelewa kwanini licha ya ushahidi kuwa uliofanyika ni uhalifu; ripoti ya Ernst and Young siyo tu imeonesha kiasi kilichokombwa lakini pia imeonesha nani amekomba kiasi gani. Kwanini hatuendi Mahakamani?


Tume haina mamlaka ya kuwafungulia mashtaka hao jamaa; ila ina mamlaka ndani ya hadidu za rejea kuwataka warejeshe fedha. Kama hilo ni kosa basi wa kulaumiwa ni yule aliyewapa hizo hadidu.

Ndio maana miezi michache iliyopita kulikuwa na makala inasema "Kwanini Rais hakuamuru hivi?" Kwa sababu siyo kile alichoamuru rais, bali kile asichoamuru ndicho kinanipa ki"dhungudhungu"

Ila kwa msimamo wa kisheria, kurejesha kwao hizo fedha kni sawa na confession; kesi ikifika mahakamani there is no way watakataa kuhusika
So, by far, tume inaenda vizuri
Lets just give them time guys

Hilo laweza kuwa kweli lakini wanarudisha baada ya tishio la hatua za kisheria (legal threat)?; wanarudisha baada ya kupewa kinga ya kutoshtakiwa (immunity deal)?; wanarudisha kama alama ya kukubali makosa ili yaishe; wanarudisha kama alama ya uzalendo wao?

Kimsingi nje ya kuta za mahakama, kinachoendelea ni mazingaombwe ya daraja la kwanza.
 
go to court! wanaoushahidi wa makampuni yote, wanajua ni kiasi gani kimechotwa, wanajua ni kampuni gani imegushi, wanajua ni nani alikuwa ofisa wa hiyo kampuni, wanajua kampuni iliandikishwa vipi n.k kwanini hawaendi mahakamani?



Hilo ndilo kubwa. Nje ya Mahakama kinachofanyika ni kujitolea. Vinginevyo tufunge Mahakama kama watu wanaweza kufanya majadiliano na wahalifu without court sanction or jurisdiction. Watu wanapovunja sheria hawapelekwi kwenye kamati, wanapelekwa Mahakamani.




Natumaini haitasomeka hivyo.



Hatua gani tena za kisheria? Yaani hatua za kisheria zichukuliwe baada ya adhabu kutolewa? Bado sijaelewa kwanini licha ya ushahidi kuwa uliofanyika ni uhalifu; ripoti ya Ernst and Young siyo tu imeonesha kiasi kilichokombwa lakini pia imeonesha nani amekomba kiasi gani. Kwanini hatuendi Mahakamani?




Ndio maana miezi michache iliyopita kulikuwa na makala inasema "Kwanini Rais hakuamuru hivi?" Kwa sababu siyo kile alichoamuru rais, bali kile asichoamuru ndicho kinanipa ki"dhungudhungu"



Hilo laweza kuwa kweli lakini wanarudisha baada ya tishio la hatua za kisheria (legal threat)?; wanarudisha baada ya kupewa kinga ya kutoshtakiwa (immunity deal)?; wanarudisha kama alama ya kukubali makosa ili yaishe; wanarudisha kama alama ya uzalendo wao?

Kimsingi nje ya kuta za mahakama, kinachoendelea ni mazingaombwe ya daraja la kwanza.

Mwaka huu watachoka wenyewe, wanajaribu kupitisha mambo chini ya zulia wakizani watanzania wa leo ni wale wa miaka 47? hapa halali mtu mpaka kieleweke.
 
FD yaani unasema mtu akisahihisha alichofanya asiadhibiwe? au mtu anapoadhibiwa mojawapo ya adhabu ni restitution? Kwanini tutangulize restitution before convictions?

Mwanakijiji,

Ninamaanisha acha warudishe kwanza kisha mambo mengine tutaangalia baadaye. Kwa mtazamo wangu na uzito wa suala lenyewe, wakirudisha na RIBA na kisha biashara zao kutaifishwa ina settle kabisa. Yeah Restitution ni muhimu kabla ya conviction.

Ingawa tunavunja sheria lakini angalia kwa macho mawili huu mfano:

Jamaa wameiba, fedha zipo out of GOVT reach, ukamshitaki na kumfunga miaka 10 nadhani au 30 max. hela billion 130 ukazikosa.
AU
Jamaa wameiba wakasema fedha wamezificha au kuwa na hisa kampuni za nje ambazo hatuna utaratibu wa kubadilishana mali au watu, LAKINI wameamua kuzirudisha na RIBA nzuri tu.

Utaamua lipi kati ya hayo kwa manufaa ya Taifa?
 
go to court! wanaoushahidi wa makampuni yote, wanajua ni kiasi gani kimechotwa, wanajua ni kampuni gani imegushi, wanajua ni nani alikuwa ofisa wa hiyo kampuni, wanajua kampuni iliandikishwa vipi n.k kwanini hawaendi mahakamani?
.

Mkjj unajua court procedure ni ndefu halafu uelewe kuwa hawa watu wana mapesa mengi they will hire the best lawyers in the land na kama ujuavyo there is always a loop hole in judiciary system.

Ni bora govt wa recover hayo mapesa and then take them to court.besides mara wanaporudisha hayo mapesa ni evidence tosha.
 
Mwanakijiji,

Ninamaanisha acha warudishe kwanza kisha mambo mengine tutaangalia baadaye. Kwa mtazamo wangu na uzito wa suala lenyewe, wakirudisha na RIBA na kisha biashara zao kutaifishwa ina settle kabisa. Yeah Restitution ni muhimu kabla ya conviction.

Ingawa tunavunja sheria lakini angalia kwa macho mawili huu mfano:

Jamaa wameiba, fedha zipo out of GOVT reach, ukamshitaki na kumfunga miaka 10 nadhani au 30 max. hela billion 130 ukazikosa.
AU
Jamaa wameiba wakasema fedha wamezificha au kuwa na hisa kampuni za nje ambazo hatuna utaratibu wa kubadilishana mali au watu, LAKINI wameamua kuzirudisha na RIBA nzuri tu.

Utaamua lipi kati ya hayo kwa manufaa ya Taifa?

swali lako zuri lakini lina makosa kidogo.

Adhabu ya kosa haijalishi malipo ya kosa hilo. Endapo mtu anamuua mtu kwa bahati, makusudi au in the "heat of passion" jamii inamuadhibu muuaji yule kwa kiwango mbalimbali cha adhabu. Masharti ya kumuadhibu mtu yule hayatarajii malipo ya kumrudisha aliyeuawa.

Tunafanya hivyo hivyo kwa mtu anayechoma nyumba, n.k na kuteketeza kitu au kutumia kitu. Nilipokuwa boarding mwanafunzi mmoja aliingia ofisi ya walimu akakuta kuna chapati mezani akazifakamia na walimu walipombamba walimuadhibu kwa kula chapati lakini hakukuwa na dalili yoyote ya yeye kukaa jikoni na kupika chapati nyingine.

Sasa, swali la fedha kurudishwa ni zuri na hilo kwangu halina mjadala. Lakini kama hatuna sheria ambazo zinaweza kulazimisha kurudisha fedha zote na riba na pia kuadhibu bila kuangalia sura basi tuna tatizo jingine kubwa zaidi.

Sasa nikijaribu swali lako ni kuwa adhabu ya kosa haitegemei mashartii ya kutengeneza kilichoharibiwa. Kwa sababu hadi hivi sasa kinachofanyika ni extra judicial; Unao ushahidi mkononi wa uhalifu, unayo majina ya wahalifu, unajua wapi wameficha mali ya uhalifu (ndio maana wanarudisha!)na una uwezo wa kuwapata wahalifu wote (wengine umepiga nao picha!), sasa kama unavyo hivyo vyote kwanini usiende mahakamani kupata convictions and still get our money back?

Jibu ni jepesi; hakuna mtu atakayeenda mahakamani; kama atakuwepo watakuwa ni wale wadogo wadogo ambao hata hawajulikani walipo. Trust me, Jeetu Patel hatofunguliwa kesi ya Kughushi, kuhujumu uchumi au ubadhirifu wa mali ya umma kesi wanayoweza kufunguliwa itakuwa ni kama ya Vithlani; giving "misleading statements".
 
Back
Top Bottom