Mr Blue ndiye msanii mwenye uwezo mkubwa kwenye stage kuliko wasanii wote wa bongo fleva Tanzania?

Kwa Sasa hivi ambapo amejikita utimu kiba ndo anakuja kuisha kabisa na amevyonenepeana ana ata pumzi now days.
Nenda katafute clip zake akiwa stageni hivi karibuni uone...
 
Halafu mashabiki wanaimba nae hata akisema sema weeeweee... ila jamaa anayo pumzi kubwa sana stageni
 
Tanzania ndo nchi ya kwanza dunain kwa kusifia vitu vya kijinga
Sijui lini mtaacha ujinga wenu kujikuta wajuaji!.. Ujinga upo wapi hapo!?, usikute ukitoka sana ni mikoa 2 toka sehemu ulipozaliwa!..
 
hahahaha wewe unapenda ligi sana hahaha
 
naona mkuu siasa umestafu umeibukia kwenye bongo flava na bolingo yamobimba....hahaaaaa
sisi tupobize na majonziya ajali mkuu
hahahaha mkuu mimi huku huwa ni makazi yangu na ni mwenyeji wa hili jukwaa kitambo...huwa nakuja kujadili burudani bila stress...
 
The Babylon Biz a.k.a Kabayser.

'PESA' is among of the mostly played track in my music library.

-Kaveli-
 
Hakuna msanii mwenye uwezo mkubwa jukwaani kwa Tanzania hii wa kumzidi Shilole
 
kumfananisha mr. Blue na wasanii wengine wa bongo flabor ni sawa na kufananisha kifo na usingizi, blue kawaacha mbali sana wabongo flavor, kuanzia anaanza mziki blue sio kwenye stage tu hata nyimbo zake na video zake ni tofauti kabisa kama sio wa nchi hii, ukitaka kuona tofauti ya blue na wengine angalia video moja tu ya blue ya mapozi, kawaida kwa wasiojua maana ya video au movie ni kuonesha kwa vitendo, na ndio maana miaka mingi tumeluwa tukiangalia movies za kihindi wala hicho kihindi chenyewe hatukijui, lakini ukitaka mtu akutafsirie atakupa picha kwa usahihi kuliko huyo muhindi mwenyewe, ukiangalia video ya mapozi kuanzia mwanzo hadi mwisho alichokiimba ndio alichokicheza kwenye video, na ndio kwenye video na ngoma zake zote yuko hivyo, kuna watu wanasema blue ni mzuri kwenye kolabo lakini nyimbo alizoimba mwenyewe blue ndio zimemtangaza yeye kama yeye, msanii wa kibongo aliemfuatia kwa karibu na nahisi angeliweza kumchalenji blue ni snoop lee, ila sijui alipotelea wapi maana mara ya mwisho nilikutana nae sinza club sansiro kwenye staight music hip hop talent search mwaka 2008, tulikuwa naye pamoja na AY tukicheki vipaji sijui kapotelea wapi.
 
Huwenda nitakuwa na roho mbaya, Mr Blue ni moja kati ya wasanii ambao siwezi hata kuhudhuria show yake hata iwe sebuleni kwangu mimi nikiwa Chumbani.
 
Mbwa koko hawang'atiiiiiiiiii,SIMBA OG. BYSER HIMSELF yupo vizuri stejini (hachoshi,anaamsha vibes).Ila singeli ndiyo siku hizi wanashika hatamu kwenye kuamsha vibe wanapoperform stejini (watu hulipuka na kisingeli).Blue ni legendary hivyo anajua nini mashabiki zake wanataka.
 
Binafsi namuona Blue kama nabii wa muziki.ukitazama hapo nyuma Blue alikuwa anavaa kinyamwezi sana watu walikuwahawamuelewi time imepita Leo anavaa casual sana na anatokelezea fresh.wasanii wengine Leo hii ndo wanavaa kama Blue kipindi hicho wanajihisi wao wako na peak ya stly kumbe jamaa alishapita huko.
Na sio staging tu hata kwenye chorus za kibabe jamaa ni hot sana
 
Blue hata uumpe jukwaa kubwa vip utaliona dogo hata kama yupo pekee yake
 
Wekeni ufafanuzi vizuri mnaposema Tanzania nzima na ipigwe kura isiyo na upendeleo

Diamond ana show muda sawa na Mr Blue na jijini, wangapi watakwenda kwa Blue?

In no particular order, nyimbo za Mr Blue nazosikiliza ni (+collabos);

1. Pesa
2. Tuko Pamoja
3. Mboga saba (Ali Kina)
4. Tabasamu (Steve R & B)
5. We ni wangu (Belle 9)
6. Dhahabu (Dully + Joselyn)
7. Nilikataa (TID + Q Chief)

Hizo ndo ambazo mara nyingi sana nasikiliza siku nikitaka kumsikiliza Byser
 
Diamond atapata wengi sana na si jambo LA kushangaza ila Kwa Mr blue ni habari nyingine anaamshaamsha kwenye jukwaa.jaribu kupitia show za fiesta uone mini Blue anafanya na anapandishwa pale msanii aliepita kapiga bila mavibe yakutosha so watu wanatakiwa kupata vibe ndo blue anapanda.
Imagine nyimbo kama Tabasamu jamaa anapiga mavibe wakati ni nyimbo ya slow.
So jamaa ni mzuri kumiliki jukwaa hata kama yupo pekee ake
 
Niukweli Mr. Blue anamiliki jukwaa.

Fid Q anasahau mistari.

Roma anajitahidi saana tena saana.
Wakali wa hizo fani unawatambua vyema.
Hebu chana kidogo mkuu,
Ujuzi haupotei[emoji23][emoji23]
 
Acha leo nami niwe shabiki.

Hatuongelei kujaza nyomi ila amsha amsha ya msanii na kulimiliki jukwaa lake.

Diamond ni msanii mkubwa ana nyimbo nzuri zinazosikilizwa kila mahali.

Ni msanii ambaye akiwa na show atajaza kumzidi msanii yeyote Tanzania.

Lakini jukwaa halimiliki kama Blue. Jamaa ingia Youtube angalia show ya Diamond akiwaZimbabwena Jah wakiperform Watora mari.

Audience ina mzuka lakini hawakuweza kuimaliza kiu au matarajio yao.

Ingia youtube angalia show ya Fiesta mwaka jana Dar blue akiperform...ana pumzi, anaamsha amsha na analimiliki jukwaaanaimba na watu hadi mwisho.

Roma pia chemistry yake na audience akiwa jukwaani ni kubwa saana sema kwa hivi maika ya karibuni imeshuka.

Mtambo mwingine ulikuwa Nature.
 
Wakali wa hizo fani unawatambua vyema.
Hebu chana kidogo mkuu,
Ujuzi haupotei[emoji23][emoji23]
Niaje upo?

Fid Q huyu jamaa anasahau mistari jukwaani...Sijui shida yake nini.

Ni sawa na Saigoni naye...wanakaza lyrics wakifika jukwaani wanakuna vichwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…