Mrakibu Msaidizi wa Polisi Fatuma Kigondo afunguliwa shtaka la kutuma vijana kufanya ukatili kwa binti wa Yombo

Mahakama Ya Police Imemaliza Sehemu Yake
 
uzuri jeshi la polisi ni makini

uchunguzi bado unaendelea rai yangu kwa watanzania kuacha kuwasikiliza wazushi na kuepuka kuendeshwa na mihemko
 
Sielewi labda. Kwa mfumo wa Tanzania ofisi ya mwendesha mashtaka (DPP) si ina mamlaka ya kukataa kuendesha hii kesi?

Kuna point nilizitoa huko kwingine:

Kikubwa ni kupata ushahidi kwamba kweli walitumwa, mara nyingi anaetoa contract au kuwatuma anarekodiwaili kutiwa hatiani. Ataachiwa pale ambapo kunakuwa hakuna ushahidi mahili kwamba alitoa maagizo. Huyo afande alituma watu wakabake, akikana na kusema si kweli, kuna ushahidi gani kwamba aliwatuma? Haiwezi kuwa suala la their word against her word, lazima kuwe na kitu kinaitwa substantiating evidence kwamba aliwatuma, mfano malipo, au walimrekodi nk. La sivyo huwezi kumfungulia mashitaka, anachomoka.

Nyerere alimuuliza mwandishi wa habari Nairobi, tu akikuambia mimi ni baba yako, kwamba nilitembea na mama yako ndio ukazaliwa, utamuamini kwa kuwa tu amesema hivyo?
 
Sijui sheria zipoje lakini ,,, kama mimi ndiyo huyo afande nawakana wausika ,, nasema hivi
" Mimi hao watu siwajui na wala sihusiki na walichofanya kama kuna ushahidi wowote ambao wanao juu ya wao kunihusisha mimi na walichofanya basi waulete na mimi nipo tayari kushirikiana na serikali juu ya chochote itakacho itaji ili kukomesha vitendo vya ubakaji kama vilivyofanywa na watuhumiwa asante "
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…