Mrakibu Msaidizi wa Polisi Fatuma Kigondo afunguliwa shtaka la kutuma vijana kufanya ukatili kwa binti wa Yombo

ukitaka ujue wino ni hatari
chukua kalam andika kitu chochote,halafu tunza sehem yako njeti yenye docment zako nyeti.kisha kaa hata miaka 30.siku itaikuata hiyo karatasi na hutokumbuka uliiandika lini.
sasa mfano huu uhamishie kwenye vifaa vyetu tunavyovitumia kizazi hiki cha sasa. naamin mambo ya kalam yanaendea mwisho. tumebaki na vifaa tu vya kuhifadhia picha,maandishi,na vidio. naamini hata hapa jf kuna baadhi ya mabandiko yako ushayasahau na hata siku ikitokea ukaaonyeshwa badhi utayakataa.

sasa hawa vijana pamoja ni askari lakini hawana usmart wowote. wangekua smart wasinge rekod picha za video kwenye vifaa vyao.wakijua kabisa huu ni ushahidi kwa baadae.
tukio lilitokea mwezi wa 5.linakuja kujulikana mwezi wa 7 miezi miwilibaadae.. hii inaonekana wamejisahau wakaona watumiane picha na vidio.na inawezekana hata aliepost hizo video mtu mwingine ambae hajahusika ,baada ya kuona video kutoka kwenye simu za rafiki zake. askari wa kitanzania smart ni 10% tu.
 
Lakini ,, nionavyo na kufikiria mimi ,, kunitambua tu peke yake haitoshi kunitia hatiani
Vipi kama muhusika tunafamiana kitambo tu labda kwasababu tunaishi pamoja mtaa mmoja au tumekuwa tukiona mahala fulani mara nyingi ,, na kwasababu anazozijua yeye kaamua kushirikiana na hao majamaa kunichafua kwa kunitaja katika sekeseke hili ??..

Ni ushihidi gani utakuwa na nguvu ya kumtia hatiani huyu aliowatuma ?? Je ni wa sauti ? Picha au maandishi ?? ,, Vipi kama aliyewatuma alikuwa too smart kiasi kwamba katika aina zote tatu za ushahidi niliojiuliza hapo juu (maandishi (mesegi ) picha au sauti ) hakuacha alama yeyeto mfano

Wakati anawatuma hakupiga simu kusema walimrekodi akiongea ,,au pindi walipokutana mahala kupanga mikakati ya tukio hili hakuna picha ilipigwa ,, au hutumia jumbe yeyeto kuwapa maelekezo wahausika ,, je bado kutakuwa na ushahidi wenye nguvu kumuweka hatiani katika kesi hii ??? Nimejaribu kuwaza tu ntashukuru sna ukinipa ufafanuzi juu ya maswi yangu haya
 
Kuna wanaharakati wapo kwa maslahi ya umaarufu wao hivi akiambiwa aithibitishie jamii kama huyo mama ndiye ataweza?
 
Hii kesi sahvi inakoelekea 😄
Acha sahv tuwe watizimaji na wasikilizaji

Ova
Inaelekea pazuri. Polisi nao wanakomaa kukwepa mishale ya wananchi. Ila naona itabidi wamtoe tu huyo kamanda wao ili kujisafisha.
 
Kumtia hatiani ni rahisi sana kama kilamtu atamdondokea yeye yani shaidi wa kwanza mpaka walalamikiwa wa kosa tajwa.

Ila kama afande hatabainishwa na woteee hata walofungua kesi wataitoa wenyewe
 
Kumtia hatiani ni rahisi sana kama kilamtu atamdondokea yeye yani shaidi wa kwanza mpaka walalamikiwa wa kosa tajwa.

Ila kama afande hatabainishwa na woteee hata walofungua kesi wataitoa wenyewe
Hapo nimekuelewa,,,
 
Kama alikuwapo eneo la tukio aya binti alivyoambiwa omba msamaha afande mbele yake atoweza mtambua uyo mtu
 
Niliwahi kukaa na Polisi kwenye kituo kimoja cha Polisi mwaka 2010 kwa muda wa masaa yasiyopungua 36 na kuanzia pale ndiyo nilipoweza kupata angalau picha ya namna ambavyo Polisii huwa wanayofanya kazi

Ilikuwa ni experience yangu ya kwanza na ya mwisho ya mimi kuwepo kwenye mazingira ya kazi zao, tangu pale sijawahi tena hadi leo

Niliingia pale Ijumaa jioni na nilitoka J2 mchana wa baada ya saa 7
Sikuwa mhalifu lakini nilwekwa ndani kwa muda wa masaa yote hayo
Nilinyimwa maji na chakula kwa angalau masaa 12 na pale maji na chakula vilipoletwa, vilikuwa ni vya ku-share na wahalifu wengine waliokuwa wapo sero

Niliriripoti pale kituoni kwenye mazingira ya kutatanisha

Baada ya maelezo hayo namba niulize maswali yafutatayo kwako

Mosi: Unaweza kuhisi ni kwa nini niliwekwa ndani na wakati sikuwa mhalifu?
Pili: Unadhani ni kwa nini ninawasifu kwamba wako smart, wakati niliwekwa ndani wakati sikuwa mhalifu? Katika hali ya kawaida niltakiwa niwaponde kwa kuniweka ndani bila kosa

Tatu: Unadhani ni kwa nini nilinyimwa maji na chakula kwa muda wote huo?

Wewe raia unayekaa umejiachia kwa masa 24, huwezi ukasema kuwa Polisi hayuko smart wakati yeye yuko alert every second, 24 hours a day, 366 days a year. Hawa watu wako kwenye mode ya "chonjo" every second

Wewe uko smart?
 
Fesibuku siendi.

Nina swali hapa.
Hivi kifungu cha criminal law kinasemaje, kuhusu polisi mwenye cheo kikubwa cha ACP kama alivyo Fatuma Kigondo kutuma watu waende kumfira binti?
 
Fesibuku siendi.

Nina swali hapa.
Hivi kifungu cha criminal law kinasemaje, kuhusu polisi mwenye cheo kikubwa cha ACP kama alivyo Fatuma Kigondo kutuma watu waende kumfira binti?
ACP hana kinga ya kushtakiwa hivyo anashtakika vzuri sana.

Ubaya ni kwamba wanaotakiwa kumshtaki wapo chini yake ndo maana wao wanapata tabu kumshtaki mkubwa wao.

Ila katika sheria ana kesi ya kujibu kama kweli ni yeye amewatuma, kingine jamii inatakiwa kujua kuwa kuplan kutenda kosa au kusaidia kosa kutendeka nako ni kosa.

ALL IN ALL katika Jicho la Sheria, NYUNDO NA WENZAKE WATAACHIWA HURU KWANI USHAHIDI UNA CHANGAMOTO NA HII KESI KAMWE JAMHURI HAIWEZI SHINDA.

Niko Paleeee...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…