Mramba na Yona, Wakabidhiwa vifaa vya usafi Hospitali ya Palestina

Hongera tanzania.nchi ya upendo na aman.ukiiba billions of money unafagia hospital.ukiiba kuku miaka mitano jela na kaz ngumu.usawa uko wapi??wangeafilis hiyo hela watafutwe vibarua wafanye usafi wa hizo hospital.hii ni kama kaole sanaa group
 
Tukitaka tuelewe zaidi tujiulize je kama wafanyakazi hatujawahi kufanya errors katika kutoa maamuzi yetu?!?!?

Umesema kweli
 
Acha ifikie hapo, pamoja na makosa yao yapo pia waliyoyafanya mazuri enzi zao.
nashangaa kwanini Mkapa wamemuweka mbali na hizi tuhuma anyway,ccm ya majipu,magamba n.k since 1995 tunaongozwa kwa mizaha na matukio
 
Huu ni usanii wa hali ya juu. Taifa kuingia hasara ya bil 11.7 ilitakiwa majaji wetu wajiulize tunali-cover vipi hasara hii. Kwa maana kwamba pamoja na kifungo ingelibidi wafilisiwe mali zao.
Ila kwakuwa nchi ni ya wasanii hata hao majaji watakuwa wamefaidika na mgao wa haya mabilion.
 
Mramba na Daniel Yona hawakupaswa kabisa kutumikia kifungo nje ya jela kwa wizi wa billion 11.7 ambao wao walisababisha.

Lakini kwa kuwa waliwahi kuwa watu fulani basi wanakubaliwa kabisa kwenye hii.

Halafu Basil Mramba ana rekodi isio nzuri kabisa na suala la fedha, alipokuwa DG wa enzi hizo THB (Tanzania Housung Bank) ambayo ilikuwa ni benki ilokuwa ikitoa mikopo ya nyumba, benki hio ilikuja kufilisika kabisa ikiwa chini yake.

Je wafungwa wengine hasa wa hivi karibuni ambao wamesababisha hasara kwa serikali kupitia Bandarini na TRA wakifungwa baadae wanaweza kuomba watumikie vifungo vyao nje?

Hivi ya yule mtuhumiwa mwingine Gray Mgonja yaliishia wapi?

Wanasheria na mahakama wasicheze na akili za watu.
 
Daaah! Natamani niwaone wakiinama na kudeki, hivi hawaruhusiwi kuajiri watu wa kuwasaidia kufanya usafi?
Wachukue uzoefu mwaka 2020 watajiunga kudeki bsrabara za wagombea urais wa vyama watakavyo viunga mkono.
 
Nchi hii raha sana umelamba billion kadhaa unasubil kwenda kisafisha hosp ukimaliza unaludii kula bata kama kawa!!
 

Bingo ya aina hii kweli kuna mtu atakuja kuhofu kushitakiwa?
Kwa staili hii ufisadi na majipu hayawezi kuisha-maana kwa umri wao hakuna maumivu yoyote mapene si yapo tu kwenye akaunti zao!
Tena adhabu hiyo ni sawa na kuwaweka fiti kiafya!
 
Hivi ishu ya pension zao ikoje.. wanaendelea nazo au baada ya hatia ndo basi tena? nauliz a tu!​
 
Nime notice Mramba hajanyolewa nywele yaelekea 'walihudumiwa' tofauti na. wafungwa wengine
 
Ila kuna FEDHEHA kiasi chake,mtu uliye zoea ofisi yenye viyoyozi na kukaa kwenye executive chair kiasi cha kuwa na jeuri ya kuwakebehi Watanzania kuwa ikibidi wata kula nyasi leo hii unashika fagio na rake una wafagilia hospitali yao Watanzania wale wale huku waki kutizama tuli ambiwa lakini, ajidhanie ame simama aangalie asi anguke,MUNGU HUYU,MUNGU HUYU basi tu.
 
Mnyonge mnyongeni....." haki yake mpeni!! " Hii ndo TZA ina mazuri yake na Mabay yake!!
 
Acha ifikie hapo, pamoja na makosa yao yapo pia waliyoyafanya mazuri enzi zao.
Mazuri waliyofanya ni mengi kuliko hilo walilohukumiwa nalo. Kuna wengi wapo njee wameliibia taifa huku akilindwa na chama pamoja na mfumo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…