Mrejesho wangu katika jitihada na mchakato wa kufungua biashara, kutafuta vibali katika Mamlaka mbalimbali

Hii ya leo kali ndio kwanz nasikia kutoka kwako, kwa nijuavyo mimi ukienda kuomba TIN unapigwa maswali juu ya biashara unayotaka kuifanya tgen unapewa TIN bureeee
Ni kweli mkuu, hapo kwenye TIN kadanganya, ila kwenye leseni kasema ukwel. Ngoja tusubiri mwendelezo tuone utamalizika vipi
 
Huyo mtu wa TRA alitaka umpe rùshwa bila shaka
 
Ni kweli mkuu, hapo kwenye TIN kadanganya, ila kwenye leseni kasema ukwel. Ngoja tusubiri mwendelezo tuone utamalizika vipi
Hamna kitu nilichodanganya hapo mkuu, ninaandika kile nachokutana nacho katika huu mchakato lengo ni kuwashirikisha watu wengine experience ya mchakato na changamoto ninazo/nitakazopitia na pia hapa hapa napata ushauri ninapokwama.
 
Hamna kitu nilichodanganya hapo mkuu, ninaandika kile nachokutana nacho katika huu mchakato lengo ni kuwashirikisha watu wengine experience ya mchakato na changamoto ninazo/nitakazopitia na pia hapa hapa napata ushauri ninapokwama.
Mkuu hata sisi tumepita tumepita huko, lengo lako unataka kuwaaminisha wanaJF kuwa TRA tanzania nzima wako hivyo, jaribu na ofisi nyingine ya TRA ili uthibitishe research yako
 
Mkuu hata sisi tumepita tumepita huko, lengo lako unataka kuwaaminisha wanaJF kuwa TRA tanzania nzima wako hivyo, jaribu na ofisi nyingine ya TRA ili uthibitishe research yako

Ndugu unakosea kudhani kuanzisha uzi huu nina lengo la kuharibu taswira ya TRA. TRA kama taasisi naamini hivi karibuni imekuwa ikifanya kazi vizuri, na hata huo mfumo wa kuomba TIN online uko vizuri sana nasikitika sikuwa naufahamu hadi nilipofahamishwa hapa, bila kuanzisha uzi huu ningeendelea kukomaa na huyo mtumishi mmoja aliyekuwa na malengo yake maovu. Kwa hiyo unadhani sikupaswa kuandika kuhusu hicho kisa cha huyo mtumishi wa TRA? kwanini?
 
nje kidogo ya maada,je? ni kiwango kipi cha mtaji mtu anatakiwa awe na TIN na lesini ya biashara.kuna mtu anauza vitu vidogo sana eneo la shule hata mtaji haufiki laki tano ,tuseme anatengeneza vitu wanafunzi wanakula.huyu anayo frame.
lakini kuna mtu anamwaga vitu chini kkoo mzigo wa 2m,huyu analipia kitambulisho cha ujasiliamali
hii inakaaje
 
Hilo swali angekuwepo yule Jamaa Charles Mwijage angesema hicho ni kiwanda
 

Ndugu kwa uelewa wangu kupitia huu mchakato nnaoendelea nao, kupata Leseni ya aina ya biashara yangu (Uwakala) hawahitaji kufahamu mtaji (hamna mahali kwenye form panapokutaka ujaze ukubwa wa mtaji wako).
Labda katika TIN, huko watasaidia wataalamu na wazoefu wengine hapa
 
sasa mfano hawa mam lishe unakuta amechukua frame ndogo tu inameza na viti 5,huyu anakuwa kwenye kudni lipi,mjasiliamali au mfanyabiashara mwenye TIN na leseni....
 
Jiang Yang

hawa jamaa wasumbufu sana aisee yaan kaline tu ndo mnasumbuana hivyo?? ndomana watu hununua kuepusha red-tape hii
 
Ofisi gani hiyo walikupa bila usumbufu? Labda tuanzie hapo
sio kweli mkuu mimi nilienda kuomba TIN no. nikapewa siku hiyohiyo na sikupeleka kitu, huyo mhudumu ni kanjanja
 
Ndugu kwa mwenendo huu, nahisi ufahamu unakoelekea. Hapo unahangaika upate TIN na leseni ndio unaenda kulipa frem hata line huna. Hivi unafahamu muda utakao tumia kupata hizo line kutoka kwa hayo makampuni?

Usione watu wanatumia line watu wengine ukahisi wanapenda, kwa mwenendo huu hii biashara unaweza kuichukia mapema kwa mizunguko utakayo pitia.

Nakushauri utakapo lipia frem tafuta line za majina ya watu wengine uanze biashara baada ya kupata leseni na TIN utapata line za majina yako, vinginevyo miezi 6 kodi unaweza isha na line usipate.
 

Mkuu asante kwa kulizungumzia hili. Suala la kuchelewa kupata line nimefikiria, lakini kama nilidhamilia kufuata taratibu zote nitajitahidi kukimbizana na muda ili niweze kuanza biashara hata kwa line moja, kwani si line zote nitachelewa kuzipata. Lakini nikishindwa kabisa basi option uliyoisema ya kutumia line zenye majina tofauti itakuwa haiepukiki na itakuwa kimbilio la mwisho kabisa na nitaleta report hapa pia.
 
Kila LA kheri mkuu
 
Nadhani hata ukinunua line kwa mtu itakuwa rahisi kuibadilisha nakusoma majina yako kwa kuwa tayari unayo tin namba yako.
 
Nadhani hata ukinunua line kwa mtu itakuwa rahisi kuibadilisha nakusoma majina yako kwa kuwa tayari unayo tin namba yako.

Asante kwa idea mkuu. Nikikwama kabisa nitairejea, lakini kwa sasa lengo kuu ni kufanikisha zoezi zima kwa kufuata taratibu rasmi kufahamu ugumu/urahisi wake.
 
Nimeupdate uzi, Stage 3. Nimefanikiwa Kupata TIN na Tax Clearence Certificate.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…