Mrisho Gambo acha Unafiki

Mrisho Gambo acha Unafiki

Watu msilielie chamuhimu tubadili katiba ili Rais asigeuke mfalme!! Kwasasa ningumu kumkatalia Rais na ukabaki salama hata supika alisema mkubwa akishasema wao hawawezi kumbishia wanakaa kimya...
hasahasa rais asiependa mawazo mbadala kama mwenda!!
 
Ila Magufuli mimi huwa naamini kabisa alikuwa na ugonjwa fulani wa akili. Hivi watu kama kina Gambo, Kigwangala, Makonda, Sabaya, Muro etc mbona ukiwatazama na kufuatilia aina ya uongozi wao unajua kabisa hapa hamna kitu, ni watu wanafiki wanaoishi kijanja janja? Si walisema alikuwa ameweka wana usalama kila mahali? Yule baba aliharibu sana hii nchi. Naona na mamayetu naye kuna majaribio ya kuwekwa ''mtu kati'' na wapambe hivyo asipoangalia atapotea vibaya sana. Ogopa sana watu wanaokusifu kupitiliza.
Isipokuwa kwa ugonjwa wa akili siko pamoja na wewe...Mengine yote nakubaliana nawe
 
Hiki ndicho alichokiongea Mrisho Gambo kweli? Mzaramo aliyesoma kwa kubahatisha hapo Kibaha, kisha kupewa ukuu wa mkoa Arusha na kutetewa pamoja na kushambuliwa na aliyekuwa mbunge G Lema leo hii anadaia alikuwakuwa anapewa maagizo kutoka juu kutekeleza halafu anasema hadharani siri aliyoapa kutoitoa popote ila kwa utekelezaji wa majukumu yake, huku watu tayari walishaumia kwanini hakujiuzulu kuonesha kutoridhika na mwenendo wa kiuongozi uliopita kama sio unafiki na uzandiki, majungu , chuki na dharau zinazohitaji.

Huyu ni msaliti, mwenye tamaa na ndumila kuwili anayetaka uteuzi wa cheo cha uwaziri tu kwa kutweza na kumdhalilisha aliyekuwa kiongozi wake na mamlaka ya uteuzi.

Je alijaribu kuzuia utaratibu wa nguvu kazi (Task-force) wa TRA wa ukusanyaji mapato kisha akatishwa na mtu yeyote?

Amtaje hadharani kama ilivyoandikwa kwenye mtandao wa kijamii, redio au TV ili kila mmoja amfahamu moja ya watu waliokuwa wanafiki kwa JPM ni nani?
Watu Kama Hawa hata mama Rais Samia awe nao Makini Sana asije akawateua kuwa mawaziri Ni wanafiki Sana watakuja kumgeuka nayeye pia.Tena uyu hata ubunge hajapata kwa Sanduku la kura leo anamshambulia boss wake wa zamani.
 
Ivi mnadhani kwenye utawala wa yule dhalimu Kuna mtu ambae angethubutu kwenda kinyume chake?? Au mmesahau yaliyomkuta Nape Nnauye na wengineo wengi
Angeomba kupumzika nafasi yake sio taaluma Ile watu wapo wengi wanaweza kuwa wakuu wa mkoa kwanini aliendelea kutii maagizo ambayo anaona ni kandamizi? Uyu ni cheo tu anataka apewe uwaziri ndo target yake
 
angejiuzulu watoto zake ungewalisha wewe mkuu??au kuongea Ni Rahisi sana!,
Yaan we imekuuma sana Gambo kusema uovu ambao walitendewa watanzania wenzenu kwa kuporwa fedha zao kwenye berue de change??? Ivi nyie mandondocha ya mwendazake mna tatizo gani??!
Uovu wa kupora ubunge wa Lema mbona hauongelei.Aachie ubunge ili tumuone kweli anachokiongea anakimaanisha na hapendi dhuluma.
 
Msimuonee Gambo kujifanya hamtambui Hali halisi..pr ya Gambo chuga Ni njema..huwez kumfananisha na sabaya..

Kazi take ilikuwa kuioiga chadema ili achukuwe ubunge....

Hakuwahi kuwaumiza watu personally...

Binafsi simchukii
 
Kama kuna mambo yanachukiza basi ni huu unafiki wa kiwango cha SGR. Moderator naomba msifute.

Hivi karibuni huyu kijana ameonekana "akijaribu" kwa kiwango kikubwa sana kujitenganisha na Utawala katili na dhalimu wa Magufuli, kitu ambacho hakijui ni kwamba hawezi kukwepa sehemu udhalimu huo.

Jana alisikika "akikandia" uporwaji wa Bureaus uliofanywa na serikali ya Magufuli huku yeye akiwa Mkuu wa Mkoa husika na akakaa kimya kwa wakati huo! Jana anadai kuwa kitendo hicho hakikua cha kibidamu.

Leo ameibuka tena baada ya watu wenye akili kuhoji kauli zake hizo, Leo anadai kuwa UTAWALA ule haukumpa nafasi yeye kama RC kutenda haki na majukumu yake yalitekelezwa na "Junior" wake kwa kisingizio cha "maelekezo kutoka juu".

Namkumbusha Gambo kuwa, hata huo Ubunge alionao Leo hapo anajua fika kuwa hakustahili kuwepo hapo, hivyo namshauri AJENGE HOJA aache kutukumbusha machungu ya ndugu zetu waliofilisiwa na Utawala dhalimu wa mwendazake



View attachment 1819779

Kama kuna mambo yanachukiza basi ni huu unafiki wa kiwango cha SGR. Moderator naomba msifute.

Hivi karibuni huyu kijana ameonekana "akijaribu" kwa kiwango kikubwa sana kujitenganisha na Utawala katili na dhalimu wa Magufuli, kitu ambacho hakijui ni kwamba hawezi kukwepa sehemu udhalimu huo.

Jana alisikika "akikandia" uporwaji wa Bureaus uliofanywa na serikali ya Magufuli huku yeye akiwa Mkuu wa Mkoa husika na akakaa kimya kwa wakati huo! Jana anadai kuwa kitendo hicho hakikua cha kibidamu.

Leo ameibuka tena baada ya watu wenye akili kuhoji kauli zake hizo, Leo anadai kuwa UTAWALA ule haukumpa nafasi yeye kama RC kutenda haki na majukumu yake yalitekelezwa na "Junior" wake kwa kisingizio cha "maelekezo kutoka juu".

Namkumbusha Gambo kuwa, hata huo Ubunge alionao Leo hapo anajua fika kuwa hakustahili kuwepo hapo, hivyo namshauri AJENGE HOJA aache kutukumbusha machungu ya ndugu zetu waliofilisiwa na Utawala dhalimu wa mwendazake



View attachment 1819779

Inawezekana kwa mtu mwenye imani na roho ya ubinadamu kama yeye roho yake ilikuwa inaumia kwa uovu waliokuwa wanafanyiwa wananchi na hasa wale ambao aliteuliwa kuwaongoza

shida ni kwamba yeye kwa nafasi yake Kama mkuu wa mkoa kwa wakati huo alitumwa kusimamia utekelezaji wa mipango ya Bwana mkubwa bila kujali kwamba yataumiza wanaotakiwa kuutumikia mpango wenyewe ama laa na tusisahau ya kwamba ingemgharimu sana kupoteza kazi ama hata maisha au kuishia magereza kama angepingana na mipango ya bwana mkubwa ambaye ni bosi wake kwa wakati huo

hivyo tuelewe tu ya kwamba watu ama viongozi kama Gambo walikuwa wanaumia sana kwa uovu uliyokuwa ukitendeka na kama alivyosema ama kuandika yeye mwenyewe kwamba bwana mkubwa angeweza hata kumtuma mtu wa chini yako kwenda kufanya mambo ya ajabu bila hata ya kukuripotia wewe ambaye ndiye mkuu wake wa kazi
 
Inawezekana kwa mtu mwenye imani na roho ya ubinadamu kama yeye roho yake ilikuwa inaumia kwa uovu waliokuwa wanafanyiwa wananchi na hasa wale ambao aliteuliwa kuwaongoza

shida ni kwamba yeye kwa nafasi yake Kama mkuu wa mkoa kwa wakati huo alitumwa kusimamia utekelezaji wa mipango ya Bwana mkubwa bila kujali kwamba yataumiza wanaotakiwa kuutumikia mpango wenyewe ama laa na tusisahau ya kwamba ingemgharimu sana kupoteza kazi ama hata maisha au kuishia magereza kama angepingana na mipango ya bwana mkubwa ambaye ni bosi wake kwa wakati huo

hivyo tuelewe tu ya kwamba watu ama viongozi kama Gambo walikuwa wanaumia sana kwa uovu uliyokuwa ukitendeka na kama alivyosema ama kuandika yeye mwenyewe kwamba bwana mkubwa angeweza hata kumtuma mtu wa chini yako kwenda kufanya mambo ya ajabu bila hata ya kukuripotia wewe ambaye ndiye mkuu wake wa kazi
Kama aliumia na akakaa kimya, tutaaminije kuwa hatakuja kuumia na kukaa kimya tena?
 
Tuna vijana vigeu geu na wasiokuwa na misimamo thabiti, vijana wa aina hii sio wa kuamini na wanaweza kuuza nchi kabisa
 
Una hoja nzuri sana. Unafiki unaitafuna Tanzania. Hawa wote walitakiwa wasiwepo tena kwenye uongozi wa aina yoyote. Sikumpenda Magufuli kwa sababu ya uongozi wake ila nimebaki kumuonea huruma sana kwani alidhani kina Lema ndiyo maadui zake akafanya kila hila ili wasipate tena ubunge na kuwapa sampuli ya kina Gambo, kumbe ndiyo walikuwa wabaya wake. Ila huyu jamaa kwa wale wanaojua kusoma haiba za watu kila nikimwangalia naona kabisa ni mpigaji fulani aliyejiingiza kwenye siasa tu. Hana sifa za kuwa kiongozi kabisa.

..nakubaliana 100% na ulichokisema.

..lakini KATIBA yetu inawapa nguvu MADHALI kuliko watetezi wa haki.

..kwenye nchi zenye katiba nzuri Mrisho Gambo angeweza kupinga hayo ma-task force na sheria ikamlinda yeye na kumuadhibu aliyeunda ma-task force.

..Kwa mfano, msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Georgia alikataa mashinikizo ya kupika matokeo toka kwa Donald Trump. Na aliweza kufanya hivyo kwasababu wenzetu wameandika katiba na sheria zao kwa namna ambayo haitoi mwanya kwa madhalimu kuwaadhibu wapenda haki.
 
Mfano mzuri ni huu...hapa bosi ni nani? Mtazame Majaliwa na hiyo body language, kapoa kama maji kwenye mtungi akipokea maagizo kutoka kwa bosi wake Bashite!

Pamoja na hilo, Gambo hawezi kukwepa lawama...analalamika nini hivi sasa? Kwa nini hakujiuzulu? Tatizo ni unafiki na tamaa ya madaraka na hata huo Ubunge wake kabebwa tu!
Sasa bosi ni nani? Huyu unayemuita bosi waty wanamsubiri kwa hamu huko gereza la segerea 😂
 
Kama kuna mambo yanachukiza basi ni huu unafiki wa kiwango cha SGR. Moderator naomba msifute.

Hivi karibuni huyu kijana ameonekana "akijaribu" kwa kiwango kikubwa sana kujitenganisha na Utawala katili na dhalimu wa Magufuli, kitu ambacho hakijui ni kwamba hawezi kukwepa sehemu udhalimu huo.

Jana alisikika "akikandia" uporwaji wa Bureaus uliofanywa na serikali ya Magufuli huku yeye akiwa Mkuu wa Mkoa husika na akakaa kimya kwa wakati huo! Jana anadai kuwa kitendo hicho hakikua cha kibidamu.

Leo ameibuka tena baada ya watu wenye akili kuhoji kauli zake hizo, Leo anadai kuwa UTAWALA ule haukumpa nafasi yeye kama RC kutenda haki na majukumu yake yalitekelezwa na "Junior" wake kwa kisingizio cha "maelekezo kutoka juu".

Namkumbusha Gambo kuwa, hata huo Ubunge alionao Leo hapo anajua fika kuwa hakustahili kuwepo hapo, hivyo namshauri AJENGE HOJA aache kutukumbusha machungu ya ndugu zetu waliofilisiwa na Utawala dhalimu wa mwendazake



View attachment 1819779

Rais Samia amerithi mihimili iliyotengenezwa kuishi KINAFIKI....!

Ni jukumu lake kurejesha ustaarabu na uungwana katika mihimili hiyo.
 
Kama kuna mambo yanachukiza basi ni huu unafiki wa kiwango cha SGR. Moderator naomba msifute.

Hivi karibuni huyu kijana ameonekana "akijaribu" kwa kiwango kikubwa sana kujitenganisha na Utawala katili na dhalimu wa Magufuli, kitu ambacho hakijui ni kwamba hawezi kukwepa sehemu udhalimu huo.

Jana alisikika "akikandia" uporwaji wa Bureaus uliofanywa na serikali ya Magufuli huku yeye akiwa Mkuu wa Mkoa husika na akakaa kimya kwa wakati huo! Jana anadai kuwa kitendo hicho hakikua cha kibidamu.

Leo ameibuka tena baada ya watu wenye akili kuhoji kauli zake hizo, Leo anadai kuwa UTAWALA ule haukumpa nafasi yeye kama RC kutenda haki na majukumu yake yalitekelezwa na "Junior" wake kwa kisingizio cha "maelekezo kutoka juu".

Namkumbusha Gambo kuwa, hata huo Ubunge alionao Leo hapo anajua fika kuwa hakustahili kuwepo hapo, hivyo namshauri AJENGE HOJA aache kutukumbusha machungu ya ndugu zetu waliofilisiwa na Utawala dhalimu wa mwendazake



View attachment 1819779

Mkuu kwa kauli hizo amenajisi integrity, uaminifu wake katika mamlaka za kuteua anakosa sifa sasa na hata milele, inahitaji mjadala wa kifalsafa kuhusu ukatili na udhalimu kumuhusu Magufuli. Mungu ampe pumziko jema na lenye heri huko aliko hasa tu kama aliofanya yalikuwa kwa nia njema kwa Tanzania na Watanzania wa sasa na wa baadae, Kwenye socio-economic transformation nayabeba mabaya yake when i see europe, asia, amerika, kinshasa, south africa, it will take presumably 20-50yrs kutakuwa na misafara ya Hija kwenda kaburi la Magu na siku ya kifo chake itaadhimishwa kwa kumbukumbu ya fahari. Sitakuwa na objection na mtamzamo kinzani wa aina yoyote ila maana mawazo mbadala ni afya na tanuri jema
 
Back
Top Bottom