Mrisho Mrisho: Meli zitenganishwe Muda wa kuwasili ili kupunguza foleni ya abiria

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Your browser is not able to display this video.


Baada ya Mdau kueleza juu ya kero ya foleni kwenye Bandari ya Dar es Salaam hasa kwa abiria wanaotoka Zanzibar, Mamlaka ya Bandari umeeleza kuwa changamoto hiyo imemalizika baada ya kufungwa kwa mashine mbili kubwa za kukagua mizigo "scanner".

Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Mrisho Mrisho amesema "Kwa siku tunahudumia abiria 6,000 hadi 7,000, mashine tulizofunga zina uwezo mzubwa na zinaweza kubeba mzigo hata wa Tani 3."

Ameongeza "Changamoto iliyopo ni Meli kutotofautiana muda wa kuwasili, zinapofika kunakuwa na watu wengi kwa wakati mmoja, nadhani tutazungumza na Mamlaka zinazoratibu safari kuhusu muda wa Meli kuwasili angalau wawaachanishe kidogo."
 
Mkurugenzi kastuka mapema angechezea PDF la Zuhra Yunus chezea wazee wa Zanzibar?
 
Z'bar imeshakuwa kubwa. TPA wafikirie kuhamisha bandari ya meli za abiria kwenda Z'bar Kigamboni. Wajenge bandari kubwa ya maana ianze kutumika in the next 5 years.
 
Ili jambo la ukaguzi kwa watu wanaotoka Zenji litazamwe vyema. Yaani abiri hasiangaliwa kama smuggler ndani ya inchi moja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…