Msaada: Bata wangu wanakufa, niwapatie dawa gani?

Msaada: Bata wangu wanakufa, niwapatie dawa gani?

[ ninao wadogo wana wiki sasa je yanipasa kuwanyoosha shingo?QUOTE="kamwamu, post: 33176020, member: 227017"]
magonjwa ya Bata wakubwa nami hunitesa, hasa ya kushindwa kusimama. Ukitotolesha wadogo tuwasiiane, dawa ipo nitakuelekeza bure.
[/QUOTE]
weka kwa faida ya wote
 
Pole sana kiongozi, japo nimechelewa kuona uzi huu ila naimani mchango wangu utakua na manufaa hata kwa siku zijazo.

Nimesoma maoni ya wadau wengi wakizungumzia upungufu wa madini Calcium na Phosphorous yanayopatikana kwenye Chokaa na Unga wa mifupa kwa wingi (Upungufu wa viini lishi hivyo haviwezi kuleta madhara yenye kuonesha dalili hizo mpaka kupelekea kifo cha bata vifaranga) Bali kuna mambo mawili niliyonayo hakika yanaweza kuleta athari zenye dalili hizo tajwa na mleta uzi

Mosi: Upungufu wa madini aina ya Selenium(Se) na Vitamin E (Huathiri kundi dogo na vifo huchukua muda kutoa, maana wanakua kama mgonjwa wa kifafa(Seizure), kinamshika atarukaruka,kujipiga chini baadae kinamuachie na anakua kawaida.

Pili: Ugonjwa hasa wa Virusi ujulikanao kwa jina la kitaalamu kama Duck Viral Hepatitis (DVH), Ugonjwa huu ni hatari ni kama Kideri/Mdondo kwa kuku, huwapata Vifaranga wa bata Wasiozidi Umri wa wiki 6, mara chache sana wiki 8.

Vifo ni vya haraka sana mara dalili zinapojionesha.

Dalili kuu ni kujipigapiga chini huku amekunja shingo, kurusha rusha/kunyoosha mabawa na miguu(Kifafa)

Vifo huweza kufikia asilimia 100 ndani ya siku chache tangu dalili kuonekana Japokua kupona kunawezekana ila sio kwamba kuna dawa, TIBA MBADALA (SUPORTIVE TREATMENT YAWEZA KUMNASUA KWENYE MIKONO YA ISRAELI JAPO SIO GUARANTEE)

Mazingira machafu ni chanzo kikuu cha maambukizi kwa vifaranga.
Ugonjwa huu HAUNA DAWA BALI HUKINGWA KWA CHANJO ambayo bata hupatiwa na umri wa siku moja, Usafi wa sehemu ya kulalia(Kiota/kiatamizi) na mazingira wanayoshindia vifaranga.

Tambua huu ni ugonjwa wa vifaranga walioko chini ya 8.
Maoni na ushauri mzuri ingawa hujataja ni chanjo gani hiyo anayopewa bata wa siku moja!!Ukienda duka la dawa za mifugo utakuta chanjo za kuku na si za bata!
 
Maoni na ushauri mzuri ingawa hujataja ni chanjo gani hiyo anayopewa bata wa siku moja!!Ukienda duka la dawa za mifugo utakuta chanjo za kuku na si za bata!
Mkuu, bata, kuku, kanga wote ni ndege na chanjo ni hiyo hiyo. Kifaranga akitotolewa anapewa chanjo ya mareks (mahepe) siku ya kwanza, then Newcastle siku ya 7 na gumboro siku ya 14
 
Back
Top Bottom