Msaada; Biashara ya kusafirisha abiria

Kwa hapa Dar hesabu ya siku sio chini ya 90,000 kwa costa
Na rafiki yangu yuko nayo inapiga Makumbusho-Gerezani via Mabibo hesabu kwa siku 110,000
 
Kwa hapa dar hesabu ya siku sio chini ya 90,000 kwa costa
Na rafiki yangu yuko nayo inapiga makumbusho gerezani via mabibo hesabu kwa siku 110,000
Asante mkuu, vipi unaweza ukawa unajua bei ya Costa na gharama za kusajili hadi ikae kibiashara?
 
Asante mkuu,vp unaweza ukawa unajua bei ya Costa na gharama za kusajili hadi ikae kibiashara?

Siyo taarifa sana ila used hadi 19m unapata, nitauliza mpya zina bei gani kwa mdau then i will give you feedback
Gharama sio kubwa, shida iko kupata vibali vya sumatra (njia ya kutembelea daladala) maana sahivi wanatoa most route za nje ya mji, Mloganzila, sso hadi uwe na mkono mrefu.
 
OK nitashukuru kama utaleta mrejesho mkuu
 
Ok Nitashukuru kwa mrejesho mkuu
 
Changamoto kubwa kuliko zote ni dereva au mtu anayetakiwa kukurudishia hesabu.

Dereva
1. Hawajali kazi, anachojali amekula siku hiyo basi. Ukimfukuza wala hasikitiki na kuleta hesabu pungufu hata haogopi.

2. Kupata dereva anayefanya kazi yake kisawa sawa ndio mtihani mgumu kwenye biashara ya daladala.

3. Kama gari linarudisha hesabu, matengenezo sio issue wala gharama za sumatra sio issue ila kama hesabu hairudi nakwambia utaichukia sana biashara hii maana utakuta matengenezo yanazidi kipato.
 
Asante mkuu kwa ushauri wako, vipi kuhusu bei za Costa kama unafahamu pamoja na uimara wake
 
Achana na biashara hiyo, hutopata pesa yoyote ya maana zaidi ya kuhangaika na kulia lia huku na kule. Pesa utakayopata kwenye hiyo buznes haijustfy effort na mtaji utakaouweka. Jaribu kuangalia biashara ya kuziba magap kwenye soko kwa kuuza bidhaa au kutoa huduma kwenye nafasi ambazo hazijatiliwa maanani na wafanyabiashara.

Mfano wa kwanza kampuni nyingi za taka zinatoa huduma kwa maofisi makubwa na viwandani na ku neglect soko la taka upande wa households(ayani majumbani) kuna watu wana uwezo wa kulipia huduma hiyo ila kwa sababu haipo basi wanakausha wanaumia chini kwa chini kwa kukosa watoa huduma.

Mfano wa pili: wauzaji wengi wa maduka ya reja reja wanapata tabu sana kwenye manunuzi ya mzigo wa dukani. Kuna bidhaa ambazo wanapata moja kwa moja kutoka kwenye kampuni inayozalisha bidhaa hiyo hasa bidhaa hizi za vinywaji kama azam, jambo, etc. lakini pia kuna bidhaa nyingi tu ambazo wauzaji wa maduka ya reja reja wanalazimika kwenda kwenye masoko makubwa kama Kariakoo kwa Dar es salaam na Ribet kwa Mwanza(kwa sababu ndo mikoa niliyo na uzoefu nayo mingine wakazi wa huko wanajua masoko makubwa yalipo)kununua mzigo wa kuuza dukani.

Ukiweza kuwarahisishia hiyo process ukanunua mzigo kutoka kiwandani au kwa suppliers wakubwa na kuwauzia , kuwapelekea mpaka madukani kwao, (sio duka la jumla eti wao wakufate wewe hapo hutokuwa umejitofautisha na na wauzaji wengine wa maduka ya jumla, which is of course a very common business)kwa kuanzia wale walioko maeneo ya jirani huwezi kukosa faida nzuri.

Achana kabisa na biashara za kuiga mkuu-1

Usiingie kwenye biashara kwa sababu umeona flani anafanya-2

Usiingie kwenye biashara kwa sababu tu una ka mtaji benki unataka ukazalishe chap chap-3.

Biashara ya usafirishaji naturally ni biashara kichaa duniani kote-4.

Jenga tabia ya kufikirisha kichwa ( ku brain storm) unapotaka kufanya biashara kuepusha akili yako kujituliza
kwenye vitu vya kawaida vilivyozoeleka-5.

Ukiingia kwenye hiyo biashara utakuja kulia usave huu uzi utaukumbuka🙂
 
Mkuu nashukuru kwa kuchangia na kuja na wazo mbadala lakini nina maswali kadhaa

1.Nini changamoto za biashara niliyoweka hapo juu ili hata nikiamua kuachana nayo kama ulivyoshauri niwe nimepata majibu ya kile nilichouliza na hizo changamoto hakuna namna ya kukabiliana nazo?

2.Ni kweli biashara inaweza isiwe mpya lakini bado uhitaji wake ukawa mkubwa hasa maeneo ya vijijini huduma kama afya na usafiri bado tuachane nazo?

3.Umesema huduma ya kukusanya takataka lakini kumbuka huduma hii ipo mjini tu,huko vijijini hakuna hii huduma maana watu huchimba mashimo na kuzichoma,huku mjini pia inahitaji mtaji mkubwa kwa ajili ya vifaa vya kazi tofaut na mtaji mdogo tofauti na mtaji nilionao Mimi?

Mwisho nakushukuru kwa mchango wako wa mawazo mbadala ingawa pia hujaweka mchanganuo na changamoto ya kila mojawapo maana siamini kama kuna biashara isiyo na changamoto kabisa
 
Biashara nzuri saana boss kama unakaa kwenye uskani mwenyewe na ikibidi ukawa tajiri wakusubiri uwe unaletewa pesa daily inabidi uwe na coaster atleats 2 hapo safi, nilifanya hiyo kazi back in days naifahamu saana nilianza kuwa conducter badaae nikawa dereva na ibidi usiweke bus lako liwe linaenda mkoani labda kwa special moment kama umekodiwa fanya mpango iwe ya mjini tu ndo inakua imara na haichoki harakaaa ,!!
 
Nashukuru kwa mawazo yako mkuu, vipi kwa siku inalaza kiasi gani?
Je nikipeleka mkoani kwa route ya Km 100 au chini ya hapo kwa Barabara ya lami ni sawa?
Vipi bei ya Nissan civilian na Costa ni kiasi gani?
 
Nashukuru kwa mawazo yako mkuu,vipi kwa siku inalaza kiasi gani?
Je nikipeleka mkoani kwa route ya Km 100 au chini ya hapo kwa Barabara ya lami ni sawa?
Vipi bei ya Nissan civilian,na Costa ni kiasi gani?
Hapo nitakuwa muongo kabsa mana kitambo siko kwenye faini hiyoo, nenda kwenye vituwo uwatafte jama wanaofanya kazi hizo watakupa experience sio hapa JF hapa labda uweze kumpata alie kwenye biashara hiyoo!!!
 
Pia mkuu nimekupata
Apo nitakua muongo kabsa mana kitambo siko kwenye fani hiyoo ,,nenda kwenye vituwo uwatafte jama wanaofanya kazi hizo watakupa experience sio hapa jf hapa labda uweze kumpata alie kwenye biashara hiyoo!!!
 
Asante mkuu
Pia jaribu kutembelea hizi nchi za SADC nako kuna gari nyingi tu za aina hii, kwa mfano ukipata Tayota Quatum yenye uwezo wa kubeba abiria 16 kwa 200,000 Botswana Pula na ukaiendesha mwenyewe from Botswana hadi hapa kwetu, gharama zitapungua mno(labda ushuru na vibali) ila ni mabasi imara mno na spears zake zitakuwa haziko mbali na hapa nyumbani. Good luck
 
Asante mkuu hizo hela ni kama Sh ngapi za kibongo(Botswana Pula 200,000)?
 
Asante mkuu hizo hela ni kama Sh ngapi za kibongo(Botswana Pula 200,000)?
Zidisha mara 170 hadi 180 but elewa hakuna tofauti kubwa kati ya Pula na ZAR, kwa hiyo ukitumia rate ya ZAR ni safi tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…