Habari wakuu,
Nina wazo la kufanya biashara ya kusafirisha abiria kwa kutumia basi ndogo aina ya Costa ambayo nategema kufanyia mkoani lakini bado nafanya utafiti nijue ni route ipi nzuri hasa itakayo kua na Barabara ya lami
Naomba kujua mambo yafuatayo kutoka kwa wazoefu wa hii biashara
1.Bei ya Costa hasa(Nissan Civilian)ni kiasi gani kwa kununua hapa nchi au kuagiza na inakua imetembea km ngapi?
2.Costa hii ina uwezo wa kubeba wastani wa watu wangapi(level seat)?na vp kuhusu uimara wake
3.Gharama za kulipia bima na usajili kwa ajili ya kutumia kwa biashara ni kiasi gani
4.Kwa route ya kwenda km 100 naweza kuingiza kiasi gani kama itaenda Mara 2 kwa siku ukitoa gharama za mafuta nk
5.Pia kwa hapa Dar Costa ya namna hio inalaza sh.ngapi kwa siku?
6.Chochote ninachohitaji kujua kuhusu biashara hii ikiwemo changamoto zake kwani sijawahi kabisa kuifanya
N:B
Safari ya km 100+makadirio ya nauli ni sh. 5000
Karibuni kwa msaada wa mawazo
View attachment 1079420