Msaada: Biashara yangu inapata Mauzo hafifu

hii kitu ya mitandaoni imekaka vipi ndugu
 
Hama location fasta,mtu akikwambia vuta subra mambo huwenda yakabadilika achana nae nyota njema huonekana asubuhi
na mambo siku hizi yalivyo tait kodi lipia miezi mitatu na sio sita ili kuangalia muelekeo
 
hahaha kutoka singida vipi nikikuletea mayai ya kienyeji kwa jumla 15k,haya ukiyavunja ni njano midhili ya yebovyebo
 
Unachosema ni kweli hata Kariakoo sasa ni mwendo wa kuchukua ODA kwa simu, Lipa Namba, mzigo unaletewa..

Wauza Bidhaa za majumbani unaagiza mzigo wanauleta unawalipa cash mzigo ukifika
 
Chochote utakachoamua ni sawa ila hakikisha unaondoka na funzo fulani la marketing.

Well, tengeneza mtandao wa wateja, jiwekee mikakati ya jina la aina ya bidhaa unazouza.

Nilifanya hatua hizi kuwa na mtandao wa wateja hasa kwenye WhatsApp contacts list / Facebook na Insta.

1.
Nilikuwa nalipia facebook ads inatangaza, insta na facebook, naweka settings accordning to aina za wateja/watu naotaka kuwafikia.

2.
Nahakikisha kuna namba za simu, na picha nzuri za bidhaa,ilikuwa mtu akipenda aki click inampeleka kwenye namba zangu za simu akitext namba inakuwa kwenye phonebook yangu

( provided contact synchronised kwenye clouds ili siku ukipoteza simu unazi recover).

3.
Nilikuwa na mpango kazi wa 3 months naruka week mbili mbili kupandisha ads.

4.
Network ikakua na hata sometime unauza lakini unaweza act kama middle man kipindi huna mzigo, mtaji ni contacts list uliyo nayo.

Fanya haya hata ukihama ulipo unaweza hama na baadhi ya wateja wako hii ina kuwa unapiga miguu yote, ila kuhusu kuhama liangalie kwa umakini hata huko uendako pia, kupiga one two za maombi/dua, ndumba ziwepo kama extras [emoji28].

Tyrone KG
 
unafanya biashara gani ndugu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…