Msaada: Daktari kaniambia mke wangu hawezi kupata mtoto kwa sababu tunatofautiana rhesus factor

Hapana mkuu ela sio kitu kwny uzma wa mtu ila ilikuwa kitu kgeni kwa upande wng ndo maana nikaja huku mnipe mawazo yanayoendana na tatzo ila nashukuru sana wadau zng wa humu kwa kunipa mawazo chanya
 
Asante kwa mawazo God Heals
 
sijui ila maelezo yake sio ya mtu ambae hana elimu hiyo
Rhesus ni aina ya antigen ambazo hupatikana kwenye chembe chembe nyekundu (red blood cells) za watu wenye Rh+ blood group. Hivyo watu hawa hawana Antibody kwenye damu yao dhidi ya Rh positive antigen.

Watu wenye Rh -ve blood group hawana hizi antigen, hivyo wakiwekewa damu kutoka yenye Rh +ve wnatengeneza Antibody ambazo hushambulia chemechembe nyekundu zenye Rh+. Vivyo hivyo kwa mama mwenye Rh -ve blood group akizaa na mwanamume mwenye Rh + blood group, na ikatokea mtoto akawa na Blood group ambayo ni Rh +ve, basi damu ya mtoto ikichanganyika na ya mama itasababisha mama atengeneze antibody dhidi ya chembe chembe nyekundu zenye Rh +ve antigen. Kwa bahati nzuri damu ya mama na ya mtoto haichanganyiki wakati wa ujauzito, ila wakati wa kujifungua damu ya mtoto inaweza kukutana na damu ya mama, hivyo mama anaweza kutengeneza antibody dhidi ya chembe nyekundu zenye RH +ve za mtoto, antibody hizi hazina madhara kwa mtoto huyu kwa kuwa zimetengenezwa wakati akizaliwa.

Hizi antibody hubaki mwilini kwa mama, na zina uwezo wa kupenya na kwenda kwa mtoto, hivyo mtoto wa pili naye akiwa ni Rh +ve, anibody hizi hupenya katika placenta na kwenda kushambulia chembe nyekundu za damu (red blood cells) za mtoto aliye tumboni, hivyo kusababisha upungufu wa damu kwa mtoto aliye tumboni na hata kusababisha kuharibika kwa mimba.

Natumai nimetoa maelezo ya kuelezea Rhesus incompatibility na mdahara yake kwa mtoto ambaye hajazaliwa.
 
Rhesus ni aina ya antigen ambazo hupatikana kwenye chembe chembe nyekundu (red blood cells) za watu wenye Rh+ blood group. Hivyo watu hawa hawana Antibody kwenye damu yao dhidi ya Rh positive antigen.

Watu wenye Rh -ve blood group hawana hizi antigen, hivyo wakiwekewa damu kutoka yenye Rh +ve wnatengeneza Antibody ambazo hushambulia chemechembe nyekundu zenye Rh+. Vivyo hivyo kwa mama mwenye Rh -ve blood group akizaa na mwanamume mwenye Rh + blood group, na ikatokea mtoto akawa na Blood group ambayo ni Rh +ve, basi damu ya mtoto ikichanganyika na ya mama itasababisha mama atengeneze antibody dhidi ya chembe chembe nyekundu zenye Rh +ve antigen. Kwa bahati nzuri damu ya mama na ya mtoto haichanganyiki wakati wa ujauzito, ila wakati wa kujifungua damu ya mtoto inaweza kukutana na damu ya mama, hivyo mama anaweza kutengeneza antibody dhidi ya chembe nyekundu zenye RH +ve za mtoto, antibody hizi hazina madhara kwa mtoto huyu kwa kuwa zimetengenezwa wakati akizaliwa.

Hizi antibody hubaki mwilini kwa mama, na zina uwezo wa kupenya na kwenda kwa mtoto, hivyo mtoto wa pili naye akiwa ni Rh +ve, anibody hizi hupenya katika placenta na kwenda kushambulia chembe nyekundu za damu (red blood cells) za mtoto aliye tumboni, hivyo kusababisha upungufu wa damu kwa mtoto aliye tumboni na hata kusababisha kuharibika kwa mimba.

Natumai nimetoa maelezo ya kuelezea Rhesus incompatibility na mdahara yake kwa mtoto ambaye hajazaliwa.
 
Asante.jf

Kumbe girls tuliowajaza.huko tunatakiwa tukapime na mama mtoto kabla ya hajajifungua

Sikujua.haya aisee,nilidhan.wanazaa tuu,

Thanks.waungwana
 
Pole sana! Kachome hizo sindano, mimi ninawajua waliochoma na wana watoto sasa. Ni muhimu sana kuchoma hiyo vinginevyo mtoto anakufa.
 
Alichosema yeye kwmb kuna sindano ya dawa anatkiwa achome itagharimu laki 4

Itagharimu 400K??? Huyo Sio Daktari Bali Ni Tapeli Huyo... Hiyo Sindano inapatikana Kwa <100K...
 
Dah
asante kwa elimu mzuri kumbe na raina aina ya blood group mm najua zile za kawaida n
Asante kwa majibu mazuri kumbe kuna blood group inaitwa Rh? Umeeleza vizuri Dah nawakubaliga sana ma dr
 
Chunguza elimu ya huyo daktari, utakuta ni Clinical officer. Kwa dunia ya leo nadhan hiyo siyo issue tena. Mambo ya Rh factor yana treatment yake hospitali, google uone
 
sindano ya ant D inachomwa masaa 72 tangu KE ajifungue il kwa mimba ya kwanza.....kwenye tatizo husika...

huo utaratibu wa sindano unabadilika kwa mimba zinazofuata kwa kuchoma sindano ya ant D kabla ya kujifungua au utaratibu ni ule ule wa saa 72 baada ya kujifungua...??..

msaada hapo kdg wataalamu...!!!...
 
Kwanza nikushukuru mtoa post kwasababu Tatizo lako ninafanana na langu isipokuwa mwenzio nimeshapoteza mimba mbili mpaka sasa kwa kutokujua, nimejua tatizo baada ya kuharibika kwa mimba ya pili. Pia niwashukuru wachangiaji wote kwasababu mmenisaidia kwa mawazo yenu. Lakini naomba kwa anayefahamu kama huduma hii inatolewa kwa wenye bima ile ya wafanyakazi, au hospitali ambayo huduma hii IPO hasa kwa mkoa wa geita au Mwanza. Ikiwezekana mnisaidie hata Namba ya mtaalamu wa huduma hii. Ahsanteni
 
Jaribu kuenda kucheck hospital zingine kama majibu yanafanana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…